Sisi hatutaki tatu wala mbili wala moja.

Zanzibar irudi kwa wenyewe, mengine tutajuana baadae.
Sasa ndugu yangu Makaimati, kazi yenu mbona ni rahisi? Wamobilize Wazanzibari wote mtoe waraka wa azimio lenu kwa rais wa muungano kwamba Wazanzibari wanataka waondoke kwenye muungano. Hakuna atakayewazuia kama hayo ndiyo matakwa ya majority.
 

Ndugu pokea thanks zangu kwa maelezo mazuri. Ukisoma vizuri habari ya huyo jamaa utagundua keywords hizi: Turabi, Oman, Qaboos, Osama, bin Laden, al-Qaeda, uislamu, sultan.

Anasema, Turabi "alimwambia" Muungano ilikuwa mbinu ya Nyerere kudhoofisha Uislam A/Mashariki ila haelezi ni kwa vipi muungano huo ungedhoofisha huo uislamu! Hivi Zanzibar au Tanganyika ikisimama peke yake ina nafasi gani kwa ustawi wa Uislamu kuliko zikiwa kwenye Muungano? Kimsingi mimi nadhani ni kinyume chake, kwamba zikiungana hata Uislamu (pengine na dini nyingine pia) ungestawi zaidi; jamani si inafahamika kwamba Umoja ni Nguvu? Zanzibar ikiwa peke yake ina siri gani ya uislamu kukua zaidi? Huyu ndugu aliyeanzisha hii thread inaelekea ana siri nzito kuhusu Zanzibar, Uislamu, Al-Qaida na hao jamaa zake wengine aliowataja.
 
Zanzibar ni tajiri sasa, beach zao wamejaa watalii, uwanja wao wa ndege zinatua midege mikubwa mpaka 10 kwa siku toka Europe moja kwa moja, dola na euro unatumia kwenye duka lolote jinsi zilivyokuwepo mittani, wazanzibari walioko bara sasa wanarudi kwao kidogokidogo kwa sasa uchumi kwao smart kabisa sio kama zamani walikimbilia bara walipokuwa na uchumi wa karafuu tu, sasa wanabaki mawaziri wao wanaitawala bara na kuiibia, huku wakitucheka, wajinga ndio waliwao, kwani zenji hamna wabara katika kazi yoyote, Dr Bilali akiwa waziri kiongozi aliwahi kumfuata mzungu wa hoteli ya Venta Mawimbini na kumwamuru kuwafukuza wafanyakazi wa bara, leo tumempa cheo kikuu kabisa kwetu, kweli wameshiba wazanzibari sasa sisi mzigo! waamue wao wakubwa, wasitupige tu kijeshi manake naona Rais wao na baraza lake la mawaziri amealikwa Uturuki, kikwete hakutakiwa wa mawaziri wa Muungano, waliyoyaongea siku nne ni siri kali, tunaiogopa Uturuki kwani ni wakali kivita na kisilaha, lina jeshi lilooogopwa sana na Israel, na ni waislamu suti yaani wasomi, huwadanganyi lolote.....
mimi sipo...
 
Sasa ndugu yangu Makaimati, kazi yenu mbona ni rahisi? Wamobilize Wazanzibari wote mtoe waraka wa azimio lenu kwa rais wa muungano kwamba Wazanzibari wanataka waondoke kwenye muungano. Hakuna atakayewazuia kama hayo ndiyo matakwa ya majority.

Ndugu yangu JASUSI,

Huu "muungano" umejichimbia sana na Viongozi wetu wanaendelea kung'ang'ania kwa sababu wanafaidi matunda ya Mapinduzi na Muungano kwa hali yoyote ile.

Kwa kutegemea viongozi hawa, hii kazi ni kubwa mno. Hata hivyo, wananchi wenyewe tumeanza kuchukua hatua kali kuwapelekea ujumbe ili watuelewe.

Kinachotukwaza ni pale Serikal ya JMT (soma Tanganyika), wanapojitia kati kuwasaidia kubaki na mfumo huu wa sasa.

Kwa hivyo vuta subra kidogo, mambo mazuri hayataki haraka.
 
Mwandishi anajinasibu kuwa karibu na Turabi na Osama. Hawa watu wawili ni classmate na tunaona cheche zao za udhalimu.
Kama Nyerere alitaka kuua uislam, Turabi angetueleza nini kinatokea nchini kwake na nani yupo nyuma yake.
Mwandishi amejihusisha na uzanzibar, Turabi, Osama sidhani kuwa amekamilisha orodha kama hajamtaja Gaidi Ghailan wa znz.
Wasichojua wznz ni kuwa kujihusisha na ugaidi si uislam zaidi ni kuuchafua uislam. Znz ni bora kwa mila na tamaduni zake bila Qaboos, Turabi au Osama. Tafadhali tendeni haki kwa uislam na waislam wema duniani. Haja zenu za kisiasa zisiudhalilishe uislam.

Mwandishi ameonyesha uzanzibar na Sulatan Qaboos katika dhana ile ile ya wznz wasiotaka kuisema hadharani, yaani wao ni sehemu ya Oman na kuwa karibu na Oman ni ubora kibinadamu. Hili wana hiari nalo maana asili na heshima ya mwanadamu inatengenezwa na mwanandamu mwenyewe.

Kinachosikitisha sana ni kuwa mwandishi kama wznz wengine wanalalamika na hawatoi suluhu. Nilidhani ilikuwa wakati muafaka kwa mwandishi kuhamasisha wznz waanze maandaman Dar walipo wengi halafu znz wakidai kujitoa katika muungano.
Kama alivyosema mmoja wetu hakuna mbara ambaye angewazuia kwa hili, lakini hakuna hata mmoja anayethubutu.
Kama wznz wengi walivyo, mwandishi ametoa hoja ya serikali tatu, lakini hajibu maswali muhimu niliyo na ninayoyauliza kila siku. Katika thread moja nimeuliza na wznz wote wakaingia mitini, hawataki kujibu. Narudia hapa tena.

Kwa vile znz inataka kuwa na kiti umoja wa mataifa, EA, SADC na uwakilishi na mashirika ya kimataifa moja kwa moja kama nchi huru,
A) Serikali ya shirikisho itakuwa inasimamia mambo gani?
B) Mamlaka ya serikali ya shirikisho yatakuwa katika sura gani ? rais mtendaji (executive) au mapambo (ceremonial figure)
C) Kama kutakuwa na nchi mbili na serikali ya shirikisho
i) Gharama za kuendesha serikali ya shirikisho zitagawanywa vipi?
ii)Ni mfumo gani utatumika kuhakikisha kuwa gharama hizo zinalipwa na wahusika bila hila.

Haya ndiyo mambo ya kujadili endapo mtu atataja seriakali tatu.Kutaja tu haitoshi ni lazima mtu mwenye uelewa aende mbali zaidi ya hapo.
 
Waliipokea Tanganyika walipokuwa wanahitaji, sasa pesa za Utalii zinawafanya wavimbiwe, bara inabana kwao sasa, haihitaji, wanataka kurudi arabuni, lakini huyu jamaa anaitaja vizuri Sudan je anaijua vizuri History ya Sudan? uoneva mkubwa uliowahi kitendewa kwa mwafrika katika ardhi ya na mwarabu katika historia ya afrika iliyohuru, uonevu huo umefanyika Sudan anaisifu huyu mzanzibari, mawazo yangu baada ya kuona mawazo ya wanzibari hawa, tukitengana, yaani muungano ukivunjika, hatumalizi miaka 5 nchi mbili hizi zitapigana vita tena vita mbaya, labda mungu awabadilishe wazanzibari, wasideke sana kama sasa, wapunguze ndotouzembe, waelimike ili ushamba upungue, waache mara moja mikwara mbuzi nyau, na la mwisho wamwombe mungu ikulu ya Tanganyika asiwepo mtu wa kutoka mikoa ya nyanda za juu abaki ****** mpole na mcheshi.
 
Uislam wa Tanzania is not synonymous with Zanzibar. Huwezi sema lengo la kuiunganisha Zanzibar na Tanganyika lilikuwa kuua uislam. That is political crap. Naamini wakati nchi hizi zinaungana, Jumla ya waislam zanzibar walikuwa si zaidi ya laki 5. At any time, Waislam walioko Bara ni wengi saaaaana kuliko wanzanzibari wote. Tatizo ni kwa wazanzibari kujipa ujiko kuwa wao ndio kitovu cha uislam afrika mashariki. So what? Je kila mzanzibari ni muislam safi kuliko waislam wote wa ujiji, upareni, na bukoba, kyela, kondoa, tabora, lindi, tunduru? Sasa utauuaje uislam wa watu laki 5 zanzibar wakati Tanganyika wako zaidi ya 13M?. Ni mawazo ya kichovu hayo uliyonayo bwana Abusahaf na Turabi wako.

Nikirejea kwenye swala zima la muungano, ninaungana na mtazamo wa Baba wa Taifa wa kuwa na serikali hizi mbili tukitazamia kuwa na serikali moja. Ila kama nyie wazenji hamtaki, basi sawa tu. Tuvunje muungano. Swala la serikali tatu linawezekana kimantiki. Lakini ukitazama mbali na kwa kutilia maanani asili yenu wazenji ya ulalamishi, muungano wa serikali tatu utakufa haraka. Nasema hivi kwasababu, kwenye muungano wa namna hiyo, nchi hizi mbili zitatakiwa kuchangia gharama kwa usawa katika serikali ya muungano. Na jinsi mlivyo wabinafsi na wabishi, kuna siku mtakataa kuchangia serikali ya muungano na ndipo huo muungano wa serikali tatu utakuwa mwisho wake.
 


Sisi hatutaki muungano wa moja, mbili wala tatu, tunaitaka Zanzibar yetu mlioipora na kuikalia kwa mabavu mpaka leo.

Zanzibar for Zanzibaris and we cant wait to see your backs.



 
Sisi hatutaki muungano wa moja, mbili wala tatu, tunaitaka Zanzibar yetu mlioipora na kuikalia kwa mabavu mpaka leo.
Zanzibar for Zanzibaris and we cant wait to see your backs.
View attachment 29568

Kumbu kumbu zangu zinaonyesha ulishawahi kuongelea serikali tatu!! Leo umebadilika ndugu yangu!!!! Tulishawahi kujadili na nikakuuliza unataka seriakli ya Tanganyika ili iweje? Kama mumebadilika na hamtaki serikali tatu ambayo sisi wengine tumeikataa kila thread(ushahidi ni maswali hapo juu ya thread yangu) ambayo hakuna anayejibu. Basi kuna njia rahisi ya kuirejesha nchi ya neema ya asali na maziwa.

Anzeni maandamano kushinikiza kuvunjwa muungano, tena muanzie hapa Dar maana ndipo mlipo wengi kuliko sehemu nyingine duniani.
Halafu sambazeni sumu znz na Uingereza mumalizie marekani.
Wakati haya yakiendelea pelekeni mswada BLW mpitishe kama mlivyofanya wimbo wa taifa, bendera, mlivyojitoa shirikisho la mpira, bandari n.k. Wakati BLW likifanya hayo, nanyi kuonyesha hasira zenu fungeni virago, acheni ajira huku bara, fungeni biashara rejeeni nyumbani.
Haya yanawezekana ndani ya mwezi mmoja. Hakika atakayewafuata huko katika nchi ya kanaani atakuwa mgonvi.
 
Sisi hatutaki muungano wa moja, mbili wala tatu, tunaitaka Zanzibar yetu mlioipora na kuikalia kwa mabavu mpaka leo.

Zanzibar for Zanzibaris and we cant wait to see your backs.
View attachment 29568


Good!
Wasi wasi wangu ni kuwa inawezekana mnaopiga hizo kelele za kutaka kujitenga hamko wengi kama mnavyotushawishi. Inawezekana watu 2000 kila mmoja ana user names kama tatu kwenye forums mbali mbali, mnaandika yale yale kwa kutumia majina tofauti halafu mnaonekana kweli mnataka kuvunja muungano.

Kama ni kweli wengi wenu hamtaki muungano, basi inanisikitisha sana kuona mko "myopic" kiasi hicho. Ina maana mpaka sasa hamuoni faida za muungano hasa kwa upande wenu? Na suala la undugu je? Au ndugu zenu wapo Oman tu? Undugu uliopo kati yenu wazenji na watanzania bara ni mkubwa kuliko undugu uliopo kati ya wazenji na waarabu wa Oman. Nakubali, kuwa kuna watu wenye ndugu Oman, lakini pia wapo wenye ndugu bara, na asili ya wengi wenu ni bara. It makes more sense kuwa kitu kimoja na bara kuliko kuwawazia waarabu wa Oman. Wengi wenu mnafikiri mpo karibu zaidi na waarabu kwa sababu ya dini. Lakini nawaaambia, Wewe kama mzenji muislam, THAWABU YAKO KWA MWENYEZI MUNGU HAIONGEZEKI eti kwa sababu ya kuwa karibu na mwarabu na wala HAIPUNGUI kwa kuwa karibu na Muislam wa Nzega! Ninawafahamu sana waarabu na nimeishi nao ughaibuni, wao wanachukuliana kama ndugu kwanza kwa kufuata uarabu, hata kama WANA DINI TOFAUTI. Sasa iweje nyie mjione mna undugu nao zaidi kuliko hata WAISLAM WENZENU WA BAGAMOYO na TUNDURU?

For your information, Mwarabu akiwa ana shida, kama vile kibano kutoka nchi za magharibi au Israeli hapo ndipo anaanza kutafuta support ya waislam wote. Kama hamna kibano, ndugu zake huwa ni waarabu wenzake. Sasa na nyie kwanini msichukulie waafrika wenzenu kuwa ndugu zaidi na mkae nao kwenye muungano?

Grow up you people!
Msifanye maamuzi mtakayo jutia baadaye. Of course, kama Nguruvi3 alivyosema hapo juu, kama wengi wenu hamtaki muungano, uamuzi upo mkononi mwenu. Acheni kupiga piga kelele na kugombana na keyboards na kutuletea stories za Turabi et al., Mwambieni hata Shein au Maalim Seif watangaze kujitoa kwenye muungano. Hilo ni suala la dakika chache tu. Wanatangaza na tunaanza kuubomoa kuanzia hapo.
 
Nanren safi sana, kweli Zanzibar kuna fikra zilizotokana na BRAINWASH za kiarabu, unakuta kila mwenye kijirangi anaitwa mwarabu na kupishwa siti pa kukaa popote pale, na hao waarabu wa kweli hawakai foleni hata siku moja, kuna siku mimi nimemtoa nishai mmoja bank, znz wanamwabudu mwarabu... mara nyingine hata mweusi kama mkaa anaijiita mwaarab na ukitaka muelewane mwiite mwaarab...
 


Wengine tunachangia kwa mujibu wa thread!!
 

Wale wanaojiita waarabu, na kujiona bora kuliko wengine ni kwa sababu hawajawahi kubaguliwa na waarabu wenyewe. Ujiko wao unaishia hapo hapo Zenji na labda wakija bara. Wakienda kwenye nchi zenyewe za waarabu kule wataambiwa wao sio waarabu, ni waafrika tu.
 
...Muungano wa Tanganyika na Zanzibar unaweza tu kuokolewa endapo katiba ya Muungano itafanyiwa marekebisho ili pawepo mfumo wa serikali tatu.
Umeongelea options nne zilizopo: kubaki na Muungano kama ulivyo, kuunda serikali moja, au tatu au kuuvunja. Umesahau moja nyingine: muundo mwingine wowote ambao hatuujui bado.

Kwa hiyo kuna options tano:

1. Serikali moja

2. Serikali mbili

3. Serikali tatu

4. Serikali 26 au muundo mwingine mpya kabisa.

5. Kuvunja Muungano.

Ukasema lifanyike kongamano la kitaifa kuhusisha rai wote na taasisi zao, tujadili nini cha kufanya. Halafu ukahitimisha kwamba serikali tatu ndio zinatufaa! Sasa kongamano lako la nini? Wewe ni msanii.

Tuachie options zote on the table. Tunataka options zote on the table, ikiwemo kuvunjulia mbali Muungano.
 
Hivi matokeo ya hii poll yalifikia wapi?
Kwasababu bado naona threads za Muungano zikianzishwa tu hata mara baada ya the so called muafaka wa cuf na ccm...
 
"we vipi bwana, tuvunje muungano kwani tuliungana lini?"......Ndoto

Kwa wana Jf wenzangu natumai kwa mnaonifahamu hamtabisha juu ya haiba yangu ya kupenda kushiriki mijadala mbalimbali ya kisiasa na elimu, Hata hivyo naomba nikiri kuwa siku za hivi karibuni nimekuwa na tabia ya kuota ndoto kuhusiana na maswala mbalimbali ambayo huwa nashiriki kujadili.


Mfano usiku wa kuamkia leo nimeota ndoto nikiwa kwenye mdahalo mkali kuhusu Muungano na ghafla katika kupinga mawazo ya mwenzangu mmoja kuwa
ni heri kuvunja muungano , mimi nikamjibu kuwa tuvunje muungano kwani tuliwahi kuungana lini? ni lini Watanganyika na Wazanzibar tuliwahi kuungana? au ni Nyerere na Karume ndiyo waliungana? nikaendelea kusema kuwa kuiita Tanganyika kwa jina la Tanzania bara ni uchochezi na pia kutuita Watanganyika eti ni Watanzania bara ni uhuni uliokubuhu, ghafla nikashtuka usingizini...... Mpaka sasa bado nawaza maana ya ndoto hii, ina maana gani?

www.novakambota.com
 
Utakuwa ulilala na mpemba kitanda kimoja,
hembu jitazame vizuri maungoni mwako.
 
hebu pitia mambo ya economic integration utajua kama tuliungana au la.
Mambo ya kuturudisha f2 sasa hivi nani anataka
 
Mkuu inaamana mpemba ni mcameroon au?

kwani hukupata kusikia tale ya mpemba na mchaga waliolala chumba kimoja gesti?
Mpemba akawa anaogopa kuibiwa, na Mchaga akawa anaogopa kuliwa tiGO...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…