Ewe mola ulieumba ardhi na mbingu na vyote vilo ndani yake ujaalie muungano huu uvunjike kwani hauna faida kwa wengi ila wachache tu ndio wanaofadika nao wengi ukiwaacha katika umaskini uliotokana na mfumo mbovu wa muungano huu, AAMIN.
 
Baada ya kuona minyukano ya kila namna na kila kona tukishambulia waasisi wa muungano na mitizamo yao ya serikali 2 huku wengine wakienda mbali na kumsema karume kuwa aliburuzwa na Nyerere huku wakina Ally Salehe wa Zanzibar wakimshsmbulia Rais Kikwete nashauri haya yafanyike.
1.Rais avunje bunge la Katiba ili maaisha yaendelee na yeye amalize kipindi chake salama bila kuingia historia ya ugobachev.
2.Aache bunge la KATIBA liendelee na inavyoelekea Mwisho ni kuuvunja muungano mana watu wa Zanzibar washakuwa na msimamo wao wa mamlaka kamili.
Mawazo yako na muungano sasa uvunjike na kama hoja ni ulinzi tuanzishe kambi ya jeshi Chumbe ili kuulinda mpaka wetu wa bahari.Halafu tuone mwenye shida na muungano na aliekuwa anafaidika na muungano ni nani?
 
Ngoja CDM wachukue Tanganyika na CUF wachukue Zanzibar

Wazo lako litatimia kwa mkataba lakini/shirikisho
 
hueleweki. mara kwenye 1 unasema rais avunje bunge la katiba, no2 aache bunge la katiba liendelee. sasa tushike lipi?
 
Ndoto ya alinacha hiyo! Muungano hauwezi kuvunjika kamwe chini ya CCM ...Nje ya CCM labda utatikiswa kidogo...
 
Kwanini usivunjike kwani ukivunjika tutakufa au wao watakufa? maisha si yataendelea kama kawaida? mimi napendekeza serikali moja tu sio tatu wala mbili....zanzibar iwe ni mkoa wa unguja na pemba ndani ya tanzania.
 
Hivi hawa akina Jokakuu,mwanakijiji ,jasusi wanapatikana wapi siku hizi manake walikuwa wanahoja za msingi ukisoma unaelimika ,angalia hawa CHADEMA na CCM hawana hoja bure kabisa
 
Warioba aliwauliza maswali Kikwete na Pinda kwamba ni lini wameshakanyaga Zanzibar kukagua au kushiriki shughuli za kimaendeleo?Ikizingatiwa wao ni viongozi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa mujibu wa katiba,hadi leo hakuna kati ya hao aliyejibu swali hilo tofauti na kuja na vioja na mipasho mipya kila siku.Kwakuwa hadi leo hawajajibu,Hivyo wao ni viongozi wa Tanganyika.Vilevile Zanzibar ina rais na viongozi wake wengine.SWALI LANGU NI JE RAIS WA TANZANIA NI NANI?.MUUNDO WA MUUNGANO:Wakati Tanzania haina Rais ila kuna rais wa tanganyika(JAKAYA M KIKWETE),CCM inatuambia tanganyika haipo bali kuna Tanzania na Zanzibar.KAMA TANGANYIKA HAIPO KWANINI TANGANYIKA INA RAIS? KAMA TANZANIA IPO,RAIS WAKE NI NANI?KAMA NDIYE HUYU JK,JE KWANINI HANA MAMLAKA YOYOTE KWA MAMBO YA ZANZIBAR?Hivi Prof SHIVJI we unaona hili ni sawa na uprofesa wako?CCM mnaliona hili sawa?HUU MUUNGANO UNA MASWALI MENGI KULIKO MAJIBU,KARIBUNI KWA MJADALA!
 
Wengi wanapagawa wanaposikia neno "Tanganyika" na wamekuwa hawaambiliki! Kibaya sana utakuta wengi wamezaliwa Tanzania na hiyo Tanganyika wanasikia tu kwenye Historia! Kwa kifupi wao ni Watanzania!! Nyerere mwenyewe aliiongoza Tanganyika kwa MIEZI 14 tu na aliikuta "Tanganyika feki" sio ile original ya Mjerumani! Ile ya Mjerumani ilikuwa na Rwanda na Burundi. Kama ni kudai Uhuru basi mzee Julius alikosea step, aliuziwa mbuzi kwenye gunia. Tuidai ORIGINAL TANGANYIKA ili kiu ya Utanganyika iweze kukatika kabisa. Kama Kagame ataleta upinzani tutamwambia tu ukweli aturudishie kilicho chetu!
Sioni kwa nini tudai nusu keki wakati tunao uwezo wa kudai nzima? Haya shime tujipange, ORIGINAL TANGANYIKA should be back!!
 
Haya Washabiki wa "Serikali 3/Nchi 3" leteni maoni ya namna ya kutwaa kilicho chetu!!
 
Huyo Siviji ni mnafiki na tamaa yake inamponza! CV yake imeshaporomoka, siku hizi anatukanwa hata na kajamba nani!
 
Muungano utavunjika hivi karibuni maana mengi yaliyojificha yanaanza kujitokeza kila kukicha.kinachofichika ni mimba ndogo ya mwezi mmoja kamwe siyo mimba ya miezi tisa hata kama mama ni kibonge kiasi gani.
 

Wengi hamjui Katiba ya Jamhuri ya Muungano, 1977 inasemaje kuhusu Mambo ya Muungano. Haya tuambie juu ya Ibara yoyote inayosema kuwa "Shughuli za Maendeleo" ni jambo la Muungano! Ndio maana JK hajaona umuhimu wa kujibu maswali ya mzee wenu Warioba kwa kuwa hiyo Katiba ya sasa inampiga chenga huyo mzee Warioba!
 
Ndugu Buchanan, shughuli zisizo za muungano zinasimamiwa na serikali gani kwa upande wa bara?
 

"Huwezi kuilinganisha akili yako na ya mzee Warioba!Pili kama shughul za maendeleo si za muungano kazi ya Rais wa muungano ni ipi kwa upande wa huko zanzibar?"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…