R.I.P mwamba.....Le mutuz.
 
Wapo walioapa kuilinda na kuitetea katiba lakini wanasema muungano uvunjwe. Haya ni madhara ya mtu kuapa dhidi ya kitu asochokielewa.

Mtu anaapa kuilinda katiba je hiyo katiba anaielewa?

Nimara kadhaa hata viongozi waandamizi wameshukiwa kuvunja katiba. Nivyema wakapata hata elimu kuhusu kilichomo ndani ya katiba. Hata mtu awe Rais au Waziri Mkuu, Mawaziri ma RC, RPC, DC nk, wafundishwe katiba siotu kuwa na washauri wa masuala ya sheria.

Nimeandika hivyo kwani mittandaoni kuna habari mbunge mmoja kutoka Zanzibar ametaka watanganyika waingie Zanzibar kwa passport. Huyu kwa lugha nyingine anataka watu wagawane mbao.

Mtazamo wangu endapo muungano utavunjika yanaweza kutokea yafuatayo.

1: Watavurugana kuhusu suala la ajira. Waondoke wawaachie wanatanganyika ajira zao. Wapo mawaziri,ma DC nk wameshikilia nafasi za bara. Waondoke.

2: Kupunguza garama za serikali hata kuhudumia wabunge. MuUngano ukivunjwa wabunge kutoka zanzibar watatuepusha na matumizi yasiyo ya lazima. Hata wasiwepo bungeni hakuna pengo litakaloonekana.

3: Mapigano ya wazanzibar wenyewe. Wakijitengatu itakua ni ngumi mkononi maana historia ina tabia ya kutoongopa.
 
Japo mpangilio wako wa uandishi ni mbovu ila una hoja. Huu muungano una faida kubwa sana kwa wazanzibari kuwa keep peaceful kwa walivyo na roho ya mbaya wakiaanchiwa hivyo visiwa vyao mapigano ya waunguja na wapemba yatatamalaki.

Ni bora Zanzibar wakajua namna ya kutulia kwenye huu muungano. Watanganyika hatuna cha kupoteza kwao hata wakiondoka leo.
 
Ninakushukuru kwa mambo mawili mkuu. 1: Kuona umuhimu wa hoja yangu
2: Kunikosoa juu ya uandishi mbovu. Yote nimeyapokea ahsante
 
Hoja za design hii ndo sababu kwanini tumeendelea kuwa katika muungano wenye kero nyingi sana kwakuwa si hoja zinazoongelea matatizo ya kweli ya muungano badala yake ni hoja za vitisho dhidi ya wanaohoji mapungufu yalilopo.

Ni wazi muungano ni jambo jema na linalopaswa kuwa na faida kwa pande zote, lakini kwa uwasilishaji wako hapo ni kama unasema wanaofaidi muungano ni Zanzaibar peke yake wakati Tanganyika wapo ndani ya muungano ili kuwasaidia wazanzibari, hii ni hoja ya kitoto sana.

Kuhusu hayo matokea uliyoyanongelea, namba moja na mbili yawaweza kuwa na ukweli lakini hasara si ya Zanzibar peke yake, Tanganyika pia itapata loss kubwa sana (rejea kutazama tena wawekezaji wakubwa katika biashara hapa Tanzania i.e. Bakhressa n.k). Hata ndoa ikivunjika sio upande mmoja tu unapata athari, ni pande zote mbili pamoja na watoto.

Ama kwa matokeo namba tatu katika mtiririko wako, hii ni hoja nyengine ya kijinga na yenye kupandikiza uongo na chuki usiokuwepo! wapi historia ilikuambia wapemba na waunguja waliwahi kupigana? na kama unautaka ukweli hasa basi unapaswa kutambua kuwa hizo chuki zinazoongelewa ni zao pandikizi la wanasiasa waouvu wasioutakia wema Zanzibar.

Muungano ni jambo jema ila unaonaje kama utakuwa ni muungano wa pande mbili zenye mamlaka kamili kila upande? nini khofu ya kuwapa Zanzibar mamlaka yao? ikiwa khofu ni kuvunjika kwa muungano basi huu si muungano bali ni ukoloni.

Kama kero za kweli za Muungano zitatatuliwa basi naamini hakuna atakayeukataa muungano.
 
Zenji hawajawahi kuwa na vita vya wenyewe , vita kule imeletwa na chama cha CCM. Hata huyu Rais wa sasa hawamtaki kama pandikizi kutoka bara
 
Na waislamu kupigana ni kitu Cha kugusa tu , Mana na dini yao unawapa inferiority so wao kupigana ndio solution kutetea Imani yao.
Yaani Mungu wao inabidi walazimishe wengine wamfuate ama wamkubali
 
Hao wafanya biashara unaowasema wengi utajiri wemeupata kwakuiba au kwakupitia rasilimali za Bara(Tanganyika)
 
Samahani nilikuwa nje ya nchi, sijui yanyoendelea.
Kwani Muungano unaelekea kuvunjika?
 
Jiandaeni kupoteza visiwa na ukanda wa pwani maana ni sehemu za zanzibar..
Kijana ni hivi znz haina eneo lolote bara wa pwani ya bara kutokana historia hakuna nchi itabadilisha ramani yake zaidi ya ramani iliyoachwa mwaka 1919 baadae vita ya kwanza

So ndo maana unaona nchi zote africa ziko hivyo ...

Shida yenu ni elimu ya madrasaa sana
 
4.Muungano ukivunjika Zanzibar itajitangaza kuwa Dola ya kiislam, Tanganyika ndo tutakuwa wahanga wa kwanza wa ugaidi na mashambulizi kutoka makundi yenye itikadi kali
 
Hili la wazanzibari kupigana umelitoa wapi au ni hisia zako?
 
Mtu atakuwa na hiali yake ya wapi abakie ,kuna nchi kibao zimevunja muungano hatukusikia ya wananchi ,niliyoyasikia ni wale viongozi wa serikali juu ya hatma yao.

maana inabidi walio kwenye madaraka ndio wahusika na sio wananchi,
Serikali ya Muungano ikivunjika mimi kama mchadema sitokubali aliepo madalakani wakati wa Uhai wa Muungano aendelee kubanisha hapo itabidi ang'atuke.

Na ndio ukaona MaCCM yanachomekea kwa wananchi ,eti wanamiliki mali mashamba na mambo mbalimbali. Uhalisia wanawaburuza watu kwengine kabisa ,ili wananchi waone watapoteza vitu vyao ,ukweli ni kuwa MiCCM viongozi serikalini watapoteza ulaji,si mnaona wanavyokula keki ya Taifa peke yao.

Mimi kama Mchadema Muungano ukifa mwananchi haguswi kabisa ,tuna watu wetu ndio itabidi waachie madalaka na kuitishwa Uchaguzi wa Tanganyika mpya.
CCM msiwatishe wananchi kabisa ,acheni hizo njama na hila tayali zimeanza kushitukiziwa,mnalinda ulaji na utawala wenu chini ya kivuli cha huyu mzanzibari na Mtanganyika anaemiliki hiki na kile upande wa pili.
Yaani Muungano unavunjwa na nyie ndio mjua hamna uongozi wa nchi unapigwa uchaguzi wa Kwanza wa Tanganyika ,mnapigwa na chini aafu tunapiga mahesabu ya na mkuu wa mahesabu, kama umeiba kimbia kabla ya uchaguzi ,msituletee mambo ya mwananchi wa huku na kule anamiliki nini, Nyie viongozi ndio wa kutazamwa mmeiba milihoni ngapi ?
 
4.Muungano ukivunjika Zanzibar itajitangaza kuwa Dola ya kiislam, Tanganyika ndo tutakuwa wahanga wa kwanza wa ugaidi na mashambulizi kutoka makundi yenye itikadi kali
Ugaidi unasababu zake. Wanaohofiwa kuwa magaidi ni wazanzibar au magaidi watatokea wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…