Unaposema Mapinduzi lazima uwe unajua ni nani alipinduliwa ?

ndio maana wanahitaji mjadala juu ya mapinduzi kwa sababu aliyepinduliwa hawezi kutambua mapinduzi na aliyepinduliwa hajaondoka kama historia inavyofundisha.sasa mistake inayofanyika ni kwamba watu wanajadili mambo ambayo siyo yale yanayowauma moyoni.
 
Zanzibar: Uhafidhina, Visasi na Miafaka isiyodumu (2)

Joseph Mihangwa Mei 21, 2008



UCHAGUZI wa Januari 1961 uliposhindwa kupata mshindi ilibidi urudiwe Juni 1961 ambapo liliongezwa Jimbo moja la Mtambwe huko Pemba kufanya majimbo ya uchaguzi kuwa 23. Hatua hiyo ililalamikiwa na ASP (kama jinsi CUF ilivyoilalamikia CCM kuongeza majimbo mawili Unguja mwaka 2005) kwamba iliipendelea ngome ya vyama vya ZNP/ZPPP.

Matokeo ya uchaguzi huo uliogubikwa na ghasia yalikuwa kama ifuatavyo:- ZNP/ZPPP viti 13 na ASP viti 10. Hivyo, kwa mara nyingine, matokeo hayo hayakutoa mshindi na machafuko makubwa na ghasia kuzuka ambapo karibu watu 70 waliuawa, zaidi ya 1,000 kujeruhiwa na wengine 1,000 kukamatwa na serikali.

Wakati huo huo, ulizuka mtafaruku na migongano ndani ya chama cha ZNP kati ya viongozi wake wakuu Ali Muhsin, aliyekuwa na kundi kubwa la wafuasi, na Abdulrahman Mohamed Babu, Katibu Mkuu wa chama na mwenye kundi dogo la wafuasi; juu ya mwelekeo wa Zanzibar kuhusu itikadi na sera za uchumi za kufuata baada Uhuru.

Rais wa ZNP (Mwafrika), Vuai Kitoweo, kwa uwezo wake duni kiuongozi hakuweza kuzuia athari za ugomvi huo ndani ya chama. Wakati Muhsin alitetea sera na siasa za mrengo wa kulia za kihafidhina (conservative policies) na utii kwa Sultani, Babu kwa upande wake alikuwa muumini mkubwa wa sera/itikadi za Karl Marx, mbinu za ukomunisti wa China na chuki kwa ukoloni mkongwe na ukoloni mamboleo.

Wakati Muhsin alitetea uchaguzi kwa misingi ya ubaguzi wa rangi kwa maana ya watu kupiga kura kwa kuzingatia asili na utaifa wa mtu (racial compartmentalization), Babu alitaka kura zipigwe kwa kapu moja bila ubaguzi wa rangi au asili na utaifa wa mtu. Wakati huo huo alikitaka ZNP kisisahau asili yake kwamba kilikuwa Chama cha Waafrika wakulima, akashinikiza ateuliwe angalau mmoja wa waanzilishi wake kugombea kiti kwenye jimbo salama kuonyesha mtazamo wa kizalendo. Mapendekezo ya Babu yalikataliwa na viongozi wa ZNP na hivyo Babu na wenzake wawili wakajiengua kutoka chama hicho na kuunda Umma Party.

Umma Party kiliungwa mkono na sehemu kubwa ya jamii ya Kizanzibari kwa mtazamo wake wa kumjali mtu wa chini. Kilipigiwa upatu pia na Shirikisho la vyama vya Wafanyakazi Zanzibar (FPTU na ZPFL ), Umoja wa Waandishi wa habari, wamiliki wa vyombo vya habari na Wanaharakati wa siasa za mrengo wa kushoto ndani ya ASP.




ABDULRAHMAN Mohamed Babu

Babu mwenyewe aliingia Umoja wa Waandishi wa habari na Wamiliki wa vyombo vya habari kama Mhariri wa gazeti la “ZANEWS” na aliweza kutoa msukumo na mchango mkubwa ndani ya vyombo hivyo na kuweza kuichonganisha serikali ya ZNP/ZPPP na wananchi. Ingawa Chama cha Babu hakikuweka mgombea /wagombea kwa nafasi yeyote katika uchaguzi wa Julai 1963, lakini kilikuwa mpinzani mkubwa na mwenye nguvu kwa serikali ya ZNP/ZPPP, ambapo kati ya kipindi cha kuundwa kwake 1962, na Mapinduzi ya Januari 12, 1964 kilikuwa mwiba mkali (kuliko ASP) kwa serikali madarakani kiasi cha Babu kuwindwa na serikali ili akamatwe kwa kosa la uhaini.

Matokeo ya Juni 1961 yaliyowapa ushindi ZNP/ZPPP ndiyo yaliyotumika kama kigezo cha kuitishwa kwa mkutano wa Katiba mjini London (the Constitutional Conference) Machi na Aprili, 1962, ili kupitisha katiba ya Uhuru. Babu alihudhuria mkutano huo kinyemela baada ya kunyang’anywa na Serikali hati yake ya kusafiria lakini akapewa hati nyingine na Serikali ya Tanganyika.

Katika mkutano huo, Waingereza walipendekeza iundwe serikali ya mseto Zanzibar ikihusisha vyama vyote, yaani ZNP/ZPPP, na ASP, ambamo ASP ingepewa nafasi tatu kati ya nafasi tisa za uwaziri na kura turufu (casting vote) juu ya maamuzi yote ya Baraza la Mawaziri.

Lakini hata hivyo, ASP walikataa pendekezo hilo, wakataka nafasi za uwaziri zigawanwe nusu kwa nusu, na kwamba uchaguzi mwingine ufanyike kabla ya uhuru, na wakapendekeza uwe katikati ya mwaka 1964. Ombi hilo lilikataliwa na Mkutano ukavunjika.

Baada ya kuvunjika kwa mazungumzo ya London, Serikali ya Uingereza ilimtuma mjumbe wake, Duncan Sandy, Zanzibar kujaribu kwa mara ya mwisho kutatua tatizo hilo la kikatiba kwa njia ya serikali ya mseto. Sandy aliwakutanisha viongozi wa pande zote mbili lakini hakuna maridhiano yaliyofikiwa.

Serikali ya Uingereza iliamua iundwe serikali ya ndani Juni 1963, na kufuatiwa na uchaguzi mwingine wiki mbili baadaye ambao matokeo yake yangetoa picha ya mwelekeo wa uhuru kamili kwa nchi.

Uchaguzi wa Julai 8, 1963, ulifanyika kwa majimbo ya uchaguzi 31 ambapo Muungano wa ZNP/ZPPP walishinda kwa viti 18 na ASP viti 13. Na kwa ushindi huo ZNP/ZPPP walipewa jukumu la kuunda Seikali na Mohamed Shamte wa ZPPP aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu wa kwanza wa Zanzibar.

Kufikia hapo, viongozi wa ASP walifungua mazungumzo na ZNP/ZPPP wakiomba iundwe serikali ya mseto na pia kuona uwezekano wa kugawana kwa usawa nafasi za uwaziri. Ombi hilo lilikataliwa na ZNP/ZPPP kwa madai kwamba nafasi kama hiyo ilitolewa kwenye Mkutano wa Katiba wa London, lakini ASP wakakataa. Kwa kauli ambayo haikutarajiwa, Waziri Mkuu Shamte alijibu kwa jeuri kwamba “siasa si kugawana mateka” na akatamka Karume avunje ASP na wanachama wake wahamie ZPPP.

Ndani ya ASP nako mambo hayakuwa shwari ambapo kambi tatu ziliibuka na kupingana vikali kuhusu mtazamo na maana ya uhuru kufuatia ushindi wa ZNP/ZPPP na kupewa jukumu la kuunda Serikali, huku viongozi wakilaumiana kila mmoja kwa chama chao kushindwa.

Kundi la kwanza lilitaka ASP ifuatilie kwa nguvu na kwa gharama zozote kuhakikisha kwamba inaundwa serikali ya mseto ikishirikisha vyama vya ZNP, ZPPP, na ASP kama njia pekee ya muafaka wa kisiasa Zanzibar.

Kundi la pili la viongozi, likiongozwa na Rais wa ASP, Abeid Amani Karume, lilipendelea upinzani makini na wa kistaarabu na utii mkubwa bungeni uendelezwe ili kuepuka Serikali kutumia sheria na nguvu za dola dhidi ya chama hicho na wanachama wake.

Hii inamaana kwamba Karume hakutaka matumizi ya ghasia au malumbano na Serikali madarakani nje ya Bunge. Ndiyo kusema kwamba aliitambua Serikali madarakani na kwamba demokrasia ilipaswa kufanyakazi ndani ya Bunge pekee kwa maendeleo ya Wazanzibari

Kundi la tatu la viongozi wa ASP lilitaka kuwapo kwa upinzani wa nguvu na wa wazi wazi dhidi ya Serikali kwa kushirikiana na Umma Party cha Babu, na kwa kutumia mbinu za chini kwa chini kuihujumu Serikali, miundombinu na mipango yake.

Kwa mgawanyiko huu kiuongozi ASP kilidhoofu na kujiendesha kwa kupapasapapasa gizani. Viongozi wake hawakuweza kuzika tofauti zao kuweza kukiokoa nacho kikapoteza morale kisiasa, na hivyo hakikuweza tena kujiratibu kama chama makini na chenye nguvu kuweza kutoa changamoto kwa Serikalil ya ZNP/ZPPP.

Zanzibar ilipewa uhuru kutoka kwa Waingereza Desemba 10, 1963 katika sherehe zilizohudhuriwa na mwana wa Mfalme (Prince) wa Uingereza na Prince Agha Khan. Viongozi wote wa nchi za Afrika Mashariki hawakuhudhuria. Vyama vya ASP na Umma vilihudhuria kama waalikwa na kutoa salaamu za uhuru.

Ni Abdulrahman Babu wa Umma Party, aliyeuacha umma mdomo wazi bila kumwelewa, aliposimama kutoa salamu za chama chake na kusema, “ Salaam…. Vyama vya ZNP/ZPPP vimeunda Serikali kuingoza Zanzibar bila ridhaa ya waliowengi. . Lakini nawambieni kuwa Wazanzibari, chini ya uongozi wa Chama chao cha Umma Party wanasubiri kunyakua madaraka ya Nchi saa itakapowadia muda si mrefu.”

Serikali ya Shamte haikudumu madarakani, kwani ilipinduliwa siku 32 tu tangu ishike madaraka na wanaharakati wa Umma Party wakishirikiana na wanaharakati wa siasa za mrengo wa kushoto walioziasi sera za ASP.

Msomaji, unaweza kuuliza, kuna ukweli gani kwa hilo? Jibu liko wazi. Angalia sehemu mbalimbali Visiwani zilizopewa majina ya Wanamapinduzi wa Kisoshalisti/ Kikomunisti kufuatia mapinduzi kama, Uwanja wa Mao-Tse-Tung, Chuo cha Fidel Castro, Hospitali kuu ya Serikali ya V.I. Lenin, Chuo cha Ualimu cha Patrice Lumumba, n.k

Itakumbukwa pia kwamba, Babu, mwanasiasa mwenye upeo mkubwa wa kuona mbali, wakati akiwa Katibu Mkuu wa Chama cha ZNP aliwahi kupeleka vijana Cuba na China kwa mafunzo ya kijeshi na mbinu za kivita ya msituni, na ambao siku chache tu kabla ya Mapinduzi ndio kwanza walikuwa wanarejea Zanzibar kutoka mafunzoni.

Vivyo hivyo siku chache baada ya Mapinduzi, Mwanamapinduzi na shujaa wa vita vya msituni kwa nchi za dunia ya tatu na mkombozi wa Cuba, Che Guevara, alitembelea Zanzibar “kuja kusalimu, ndugu, jamaa na marafiki.” Ndugu hao walikuwa kina nani kama si wanamapinduzi wa Zanzibar?. Siku chache tu baada ya kutoka ziara ya Zanzibar, Che Guevara alikamatwa (kwa msaada wa CIA) na majeshi ya Marekani na kuuawa nchini Bolivia.

Yote haya ni kielelezo thabiti juu ya nani, au kina nani waliopanga na kuendesha Mapinduzi ya Januari 12, 1964 Zanzibar. Hili limeelezwa mara nyingi katika makala zangu nyingi zilizopita.

Kama tulivyoona ndani ya makala haya, ni kwamba chaguzi zote Visiwani zimetumika kufufua na kutonesha vidonda vya kale na hivyo kuzua uhasama wa kale. Hapajawa na viongozi makini, wenye busara na hekima kuweza kuwaunganisha Wazanzibari na kuponya vidonda hivyo vya kale. Na ingawa ni Wazanzibari hao hao waliotaka Mwingereza aondoke, wakachagua viongozi wao kuwaongoza hadi leo, ni bahati mbaya kwamba viongozi wanaopata madaraka ni watu wanaoishi jana, wafitini na wenye kutazama nyuma badala ya kutazama na kuona mbele.

Kiongozi makini ni yule anayeweza kufanya maamuzi au kuchukua hatua ambazo si lazima ziwe kwa manufaa kwa chama chake, au zenye kuwafurahisha makada wake, lakini ni maamuzi au hatua sahihi na za manufaa kwa taifa; kwa maana ni taifa kwanza, Vyama vya siasa nyuma. Kushindwa kuelewa ukweli huu ni ulofa na ubinafsi wa hali ya juu.

Tunapenda kuamini kwamba viongozi wa CCM na CUF Zanzibar wataweka mbele maslahi ya Zanzibar na Wazanzibari, badala ya kuweka mbele maslahi yao binafsi au yale ya vyama vyao vya siasa na marafiki zao.

Ubabe, jeuri na kupotosha historia ili kujijengea umaarufu bandia na Usultani ni sumu kwa demokrasia, utawala bora na kwa maendeleo ya nchi.



0713-526972

jmihangwa@yahoo.com
 
Nilipoandika Screw Muungwana, nilihoji kauli ya Kikwete kuleta Muafaka wa Zanzibar.

Muafaka ulipotangazwa, tulishangilia mpaka "Wateule" walipokwenda Butiama na kubadili msimamo wa Kamati ya Muafaka kuunda Serikali ya MSeto, na kusema kuwepo kura ya maoni.

Majuzi Wapemba waliungana na kuwasilisha Barua UNDP kutaka kuwa na Serikali yao. Tumebaini juzi kuwa hata Wapemba ambao ni CCM waliungana na wenzao wa CUF kutia sahihi wakitaka Serikali yao ndani ya Serikali ya Muungano.

Chadema, walipokuja na Sera ya majimbo, tulihoji sana dhamira yao na kuuliza sehemu ya Zanzibar.


Kuangalia hizo factor nne, naridhika kusema Muungano hauna Tatizo maana ule woga wetu wa kuvunjika kwa Muungano, umeondoka kutokana na nia na kauli za Wapemba (CUF na CCM) kutaka kuwa na Serikali yao ambayo ni huru kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Kinachohitajika ni kuunda vyema mfumo wa Muungano, hili lawezekana kwa namna kadhaa.

Kuwepo Serikali ya Tanganyika, Serikali ya Unguja na Serikali ya Pemba (this means end of Serikali ya Zanzibar), na kuwepo kwa Serikali ya Muungano wa Jamhuri wa Tanzania.

Kuwepo Serikali moja ya Muungano ambayo itaongoza serikali za Majimbo, Jimbo la Pemba, Unguja, na majimbo mengine yatakayoundwa ambayo yatakuwa na Serikali za Majimbo ambazo zitachaguliwa na Wananchi.

Ukifuatilia tunachokisikia kutoka Pemba, kinabainisha kuwa badala ya kuvunja Muunganoo, moja ya njia za kusitisha malalmishi kuhusu mfumo na muundo wa Muungano ni kuzitenganisha Pemba na Unguja kuwa na Serikali zao zitakazo chaguliwa na wananchi wao.

Ukweli ni kuwa kamwe, Muunguja hatakubali kuongozwa na Mpemba, na Mpemba hataendelea kukubali kuburuzwa na kukongozwa na Muunguja.

Je hii itakuwa ni kulitusi tukio la Mapinduzi 1964? Inategemea upo upande gani wa Shilingi. Wako ambao mpaka leo wanasema Mapinduzi yalikuwa haramu, na wengine wanasema yalikuwa halali.

Mimi si Mtaalamu wa mambo ya Zanzibar, lakini kwa kusikia kauli za umoja za Wapemba, naona kuna haja ya kuwa na suluhisho la kudumu na litakaloshirikisha wananchi na si maamuzi ya Chama. Kauli na kilio cha wananchi kisikilizwe na si kudhihakiwa.

Kama Pemba wanasema, tunataka Serikali yetu ndani ya Serikali ya Muungano, je hilo si tosha kutuonyesha Wapemba nia yao si kujitoa kwenye Muungano bali ni kutaka Sauti zao zisikilizwe na kuondokana na kero za kuwa Watumwa wa Waunguja na kuburizwa na Wahafidhina wa CCM Unguja?

I could be wrong, and I could be right and save Muungano and blood of thousands.
 
Hapa hakuna Cha Pemba wala Unguja wala Tanganyika ,yote hii kukuru kakara ni ubunifu wa mbinu chafu zinazofanywa katika Uchaguzi Mkuu na hili si kwa upande wa Zanzibar tu hata upande wa Pili wa Muungano ambao ni Tanganyika nako huku minu kali zilitumika zaidi ya zile za Zanzibar.
inajulikana wazi kuwa Chaguzi zote zilizofanyika Zanzibar zilibadilishwa matokeo na hili sio siri ni jambo la wazi na linajulikana Kimataifa tatizo la Tanganyika ni kwa mawakala wa vyamakutumika na Chama cha CCM kwa kukatiwa donge nono na kuondoka sehemu ya kuhesabia kura na hapo ndipo mahesabu ya ubadilishaji wa kura unapofanywa ,Zanzibar mawakala ni wagumu na hawabanduki na dhamira yao ni kufuata maelezo ya Chama hivyo mbinu wanayotumia ni kubadili matokeo katika utangazaji tu .
Sasa kuondoa msukumano huu wa Unguja ,Pemba ,ushirika mseto ni kuitishwa Uchaguzi utakaosimamiwa kidete na Umoja wa Mataifa kama ilivyofanyika Zaire kwa Kabila ,hakuna wala tusijidanganye kama walivyodanganyana CCM kule Butiama eti waitishe kura ya maoni ,hivi walisahau kama tatizo la yote haya ni hilohilo la kura ? Vipi utaitisha kura wakati mazinge yote ya miafaka chimbuko lake ni kura ,so uamuzi wa CCM Butiama ni nonesense ndio ukawasikia CUF hawatorudi mezani kujadili suala la kura ya maoni.
Hivyo ndugu kama mnaushawishi basi ni kuzishawishi jumuia za Kimataifa za ndani na nje ziusimamie uchaguzi wa Zanzibar chini ya jukumu la UN uone kama kutatokea watu wanaotaka kujitenga au shirikisho.
 
Hapa hakuna Cha Pemba wala Unguja wala Tanganyika ,yote hii kukuru kakara ni ubunifu wa mbinu chafu zinazofanywa katika Uchaguzi Mkuu na hili si kwa upande wa Zanzibar tu hata upande wa Pili wa Muungano ambao ni Tanganyika nako huku minu kali zilitumika zaidi ya zile za Zanzibar.
inajulikana wazi kuwa Chaguzi zote zilizofanyika Zanzibar zilibadilishwa matokeo na hili sio siri ni jambo la wazi na linajulikana Kimataifa tatizo la Tanganyika ni kwa mawakala wa vyamakutumika na Chama cha CCM kwa kukatiwa donge nono na kuondoka sehemu ya kuhesabia kura na hapo ndipo mahesabu ya ubadilishaji wa kura unapofanywa ,Zanzibar mawakala ni wagumu na hawabanduki na dhamira yao ni kufuata maelezo ya Chama hivyo mbinu wanayotumia ni kubadili matokeo katika utangazaji tu .

Mpaka hapo hata JK anafahamu haya. Yote anayojaribu kusema ni kujibaraguza tu! Wizi uliofanyika pamoja na udanganyifu anajua vizuri tu.
 
Posted Date::6/9/2008
Shirika la Umeme Z'bar lazuia wataalamu wa TANESCO

Tausi Mbowe Dar na Salma Said, Zanzibar
Mwananchi

SHIRIKA la Umeme Zanzibar (Zeco), limewarudisha wataalamu wa umeme kutoka Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), ambao walikwenda visiwani humo kwa lengo la kuokoa jahazi baada ya visiwa hivyo kukosa umeme, imeelezwa.

Habari za uhakika ambazo Mwananchi imezipata, zinaeleza kuwa wataalamu hao kutoka Tanesco walifika siku moja baada ya tukio la kukatika kwa umeme visiwani humo, lakini Zeco walikataa kuwapokea wataalamu hao na kusema kuwa walishaagiza wataalamu wao kutoka nje ya nchi.

Chanzo hicho kiliongeza kuwa wataalamu hao ambao walitumia ndege maalum ya kukodi, walifika visiwani humo kwa lengo la kusaidiana na wataalamu wa Zeco lakini hawakupokelewa.

Baada ya tatizo la umeme kutokea visiwani humo timu ya wataalamu, kutoka Makao Makuu ya Tanesco iliagizwa kwenda visiwani humo kushirikiana na wahaandisi wa Zeco, lakini cha ajabu Zeco waliwakataa na kudai kuwa, wangefanya kazi hiyo wenyewe kwa kuwa tayari walishaagiza wataalamu wao kutoka nje ya nchi na tayari wataalamu hao wamethibitisha kuja,? kilisema chanzo hicho ndani ya Tanesco.

Mwishoni mwa wiki iliyopita, Wabunge wa Kamati ya Nishati na Madini, waliokuwa wakikutana katika vikao vya kamati za Bunge walihoji kwanini Serikali ya Jamhuri ya Muungano kupitia Tanesco haliingilii kati suala hilo visiwani humo.

Wakijibu hoja hiyo Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Dk Idrisa Rashid, walisema kuwa Tanesco walionyesha nia ya kusaidia visiwa hivyo, lakini Zeco walidai kuwa walishaagiza wataalamu wao.

Habari kutoka ndani ya kikao hicho zinasema kuwa baada ya tatizo hilo kutokea, Tanesco walituma jopo la wataalamu wake ambao walikodishiwa ndege maalum, kwenda kuokoa jahazi lakini cha kushangaza walipofika walishindwa kupokelewa na Shirika la Umeme la Zanz�r, hivyo kurudi jijini Dar es Salaam siku hiyo hiyo.

Habari zaidi zinasema hata hivyo, wataalamu hao kutoka nje ya nchi walioalikwa na Zeco kufika siku chache baadaye, walishindwa kufanya kazi peke yao hivyo kuwalazimu wenyeji wao kuomba mtaalamu kutoka Tanesco ili waweze kushirikiana ili kutatua tatizo hilo.

Chanzo hicho kinaongeza kuwa ombi hilo lilikubaliwa na Tanesco na kuwatuma wahandisi wake, ambao walikwenda kusaidiana na wataalamu hao kutoka nje ya nchi.

Ngeleja alithibitisha Tanesco kutuma wataalamu wake ambao wamekwenda visiwani humo, kwa lengo la kusaidiana na wataalamu hao kutoka nje ya nchi sambamba na wataalamu wa Zeco.

Kwa zaidi ya wiki mbili sasa, visiwa vya Zanzibar vimekuwa giza kutokana na kukatika kwa umeme, hali inayoelezwa kudumu kwa zaidi ya siku 90 tangu tatizo hilo kutokea.

Wakati hayo yakitokea, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, ametangaza suala la kukosekana kwa umeme kwa zaidi ya siku 19 visiwani humo kuwa ni janga na kwamba, viongozi wanapaswa kujiuzulu kutokana na tatizo hilo ambalo limewaathiri wananchi wote wa visiwani humo.

Seif ambaye alikuwa akihutubia mamia ya wanachama katika Jimbo la Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja, alisema ni jambo la kushangaza kwa wahusika kukataa kujiuzulu wakati Serikali iliyo makini na yenye kufuata misingi ya utawala bora jambo la kujiuzulu, haliwezi kuepukika hasa kwa kuzingatiwa linatokana na uzembe wa watendaji.

Amelaani baadhi ya askari wanaowakamata watu ambao wanasema au kutangaza kwamba, Zanzibar hakuna umeme wala maji na kuongeza kuwa yeyote anayefanya hivyo aende kumkamata yeye kwani haogopi kusema hivyo. ?Serikali njooni munikamate mimi nasema popote pale kwamba, hakuna maji wala umeme maana nasikia ukisema hivyo eti unaibughudhi Serikali sasa mimi nishasema waje kunikamata,? alisema.

Katibu Mkuu huyo pia amewatupia lawama viongozi wakuu wa nchi kwa kitendo chao cha kuondoka nchini, hali ya kuwa kuna tatizo katika nchi yao. Alisema kitendo cha Rais Abeid Karume na Waziri Kiongozi, Shamsi Vuai Nahodha kwenda nje ya nchi si cha kiungwana na kionaonyesha ni jinsi gani serikali isivyowajali wananchi wake.

Seif alisema serikali iliyo makini katika suala hilo ingepaswa kuwapunguzia mzigo wananchi wake kwa kuwapunguzia bei ya mafuta ya taa na mishumaa, kwa kuwa hivi sasa bidhaa hizo zimepanda bei kwa kiwango kikubwa huku serikali ikishindwa kuwajibika kwa wananchi.

Serikali ingekuwa makini ingepunguza bei ya mafuta na mishumaa, lakini wapi nyinyi mnataka kipimo gani tena mjue kama Karume hafai? Huyu hafai ..hafai, alisema Seif huku akishangiliwa na wafuasi wake.

Seif pia aliitupia lawama Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushindwa kuisaidia Zanzibar kutokana na tatizo hilo, hasa kwa kuwa nchi hizo zimeungana na zina udugu wa muda mrefu.

Alisema Rais Kikwete angepaswa kuliingilia kati suala hilo bila ya kuombwa na Zanzibar, kwa kuwa ana wajibu wa kufanya hivyo hasa kwa kuwa tatizo lenyewe ni kubwa na tayari limeshaathiri sekta mbali mbali, ikiwemo vijana kupoteza ajira huku mabilioni ya serikali yakipotea kutokana na tatizo hilo.

Tokea kutokea tatizo hili hatujasikia Rais Kikwete kusema lolote, huu ni muungano gani jamani wakati wa dhiki watu hawasaidiani? Rais Kikwete alipaswa kusaidia sio mpaka aombwe kwa sababu Wazanzibari pia ni Rais wao wamemchagua kwa kura,? alisema na kuongeza: ?Ningekuwa Rais ningemtuma waziri wangu kwenda kwa Kikwete kutaka majenereta mawili na huku nikimpa mwengine kupeleka barua nchi mbali mbali kutaka msaada,? alisema.

Hata hivyo, Maalim Seif alishangazwa na Serikali ya Zanzibar kushindwa kununua jenereta la Sh 60 milioni na kulifunga Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja, ambapo baadhi ya wananchi wanashindwa kufanyiwa matibabu kutokana na kukosekana jenereta, baada ya umeme kukatika visiwani humo.
 
Mkiambiwa hawa wahafidhina hawana masilahi na Muungano zaidi ya kujiona wao ni wababe na hawamwogopi Muungwana & Co. ,kama mnavyoona katika hiyo habari uzembe wao unasababisha kuzidisha athari na kero za Muungano ,kuwarudisha mafundi wa tanesco ambao walipewa amri na Waziri wa Muungano ni kitendo cha dharau , Ona hii......."...Wakijibu hoja hiyo Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Dk Idrisa Rashid, walisema kuwa Tanesco walionyesha nia ya kusaidia visiwa hivyo, lakini Zeco walidai kuwa walishaagiza wataalamu wao.
Hapa huyu Waziri Ngeleja inaonyesha ameshindwa na kuzidiwa nguvu na watendaji wa ZECO ,kama Waziri kusingekuwepo na urudishwaji wa wataalamu aliowapeleka kwani wametumwa na Serikali ya Muungano kwa ajili ya wananchi wa upande wapili wa Muungano ambao ni sehemu ya Tanzania ,ameshindwa kuonyesha Uwaziri wake au hajui nini maana ya cheo cha Waziri inaonyesha hawa mawaziri wa Muungano wana matatizo wanashindwa na rank za kipolisi au kijeshi ambazo wa chini hana amri ya kupinga ila kufuata linatoka juu.
 
mwiba kunchelewa, balahau kunsikia alivyokua akichowea makunduchi ? ataka nseto sasa chooko kawa nazo ?
 
mwiba kunchelewa, balahau kunsikia alivyokua akichowea makunduchi ? ataka nseto sasa chooko kawa nazo ?


Mtu wa Pwani sasa hiki Kizegua, Kitumbatu au lahaja gani tena yakheee?

Mboni watutahini?
 
Jamani ndugu zangu leo nakuja tena na duku duku moyoni, hili ni swali ambalo nimekua nikijiuliza kipindi kirefu sana bila kupata majibu yoyote...

Najua hili jambo linaweza likawa limeshajadiliwa huko nyuma..(sina uhakika) na naelewa kabisa kua kwa baadhi ya watu litawaudhi..ila kama ukitaka kujua jitu basi ujiandae kwa lolote liwe chungu au tamu...

Ok niende kwenye mada.. nimejaribu kutafakari huu muungano wetu..na hasa baada ya umeme kukatika zanzibar kwa siku kadhaa na kusababisha kero kubwa ambayo kwa namna moja au nyingine ime affect uchumi wa zanzibar in micro and macro level....

Najiuliza maswali ambayo naelewa na na uhakika kua hapa JF ndipo nitakapo pata picha halisi na majibu yote niliyokua nahitaji kufahamu.....

Wana JF je kwanini watu wa bara/ serikali inauthamini sana muungano wakati watu wa zenji wanaonyesha dhahiri kuwa hawaupendi na wako tayari mda wowote kujitenga..??? kwanini huku bara waung'ang'anie huu muungano wakati kwa mawazo yangu naona Bara haiitegemei sana zenji kama Zenji inavyoitegemea Bara... leo bara wakate umeme usifike zenji..zenji watapata wapi nishati mmbadala ya kuendesha uchumi wao kwa kipindi kifupi?????

chakula asilimia kubwa wanategemea toka bara na vitu vingine vingi vya muhimu lakini still bara wanaona kuwa zenji ndio wanaumuhimu kushinda zenji inavyowaona wao......ukifikiria sana unaweza ukaishia kuona ni vituko......au labda Bara wana Interest kubwa huko zenji ambayo wananchi tumenyimwa kujua..au labda vizazi vya mbele sana vya bara ndio vitakuja kuifaidi vizuri zenji..sisi hatujui??? au labda tunawaogopa nyerere na karume waasisi wa muungano..tunaona tuvumilie tu ili kulinda heshima ya hao wazee????

Jamani ndugu zangu wana JF naomba majibu yenu katika hili.................''KWANINI BARA WAUNG'ANG'ANIE MUUNGANO ZAIDI KULIKO WENZAO WA ZANZIBAR???''

Is there any secret behind????




'' Ni mtazamo tu waungwana msijenge chuki''

@ Wakunyuti
 
Swala la Zanzibar ni la kiusalama zaidi kuliko wengi wanavyoweza fikiria
 
Kama Z'bar hawataki kulipa, basi JK alipe toka hazina. Ukosefu wa pesa TANESCO unaosababishwa na serikali zote mbili kutolipa madeni yao makubwa pamoja na mikataba mibovu ndiyo unachangia mno kuiangamiza TANESCO na kuwabebesha Watanzania gharama kubwa za umeme ukilinganisha na nchi jirani.

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), yasisitiza deni la Tanesco bilioni 22/- lilishafutwa
Maulid Ahmed, Zanzibar
Daily News; Wednesday,July 02, 2008 @20:06

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), yasisitiza deni la Tanesco bilioni 22/- lilishafutwa

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imesema haitaki kuwa mzigo kwa Serikali ya Muungano na kueleza kutofurahishwa na vitisho vilivyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Idris Rashidi, kwa kuwapatia barua ya kuwakatia umeme iwapo hawatalipa deni la Sh bilioni 22.

SMZ imesema haidaiwi deni hilo la Sh bilioni 22 kwani lilishasamehewa kupitia mpango wa nchi zilizo masikini wakati wa utawala wa Rais Benjamin Mkapa.

Waziri wa Maji, Ujenzi, Nishati na Ardhi, Mansoor Yussuf Himid alisema Zanzibar haiwezi kuwa mzigo kwa Tanzania na haipendi kuwa na deni, na kusisitiza kuwa deni hilo lilishafutwa.

Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kulieleza Bunge kuwa Zanzibar inadaiwa na Tanesco Sh bilioni 22.

“Waheshimiwa wajumbe tumepata mshituko mkubwa sana mtu hawezi kuamka tu na kusema naongeza bei ya umeme, tena unaiongezea nchi nyongeza ya uniti moja ya Sh 168 wakati Bara wanauziwa unit moja kwa Sh 21.7 sio haki,” aliwaambia wajumbe wa Baraza la Wawakilishi.

Alisema Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) ni mteja mkubwa wa Tanesco ambapo wamekuwa wakinunua umeme kwa fedha taslimu kati ya Sh milioni 700 hadi 900 kila mwezi.

“Kwa masikitiko makubwa baada ya kukaa giza kwa zaidi ya wiki tatu tunaandikiwa barua ya kukatiwa umeme…ati Juni 27 walitaka kutukatia, hili limeshapelekwa kwa Waziri Kiongozi ikiwa kama ni sehemu ya hizo kero za Muungano,” alisema.

Himid alisema nyongeza ya bei ya umeme inaiumiza Zanzibar kiuchumi, kwani suala hilo lilionekana pia wakati wa aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa alipoagiza Mamlaka ya Udhibiti wa Maji na Nishati (EWURA) kufuta bei yake mpya kwa Zanzibar.

Alisema wameshangazwa na kitendo cha Tanesco na Ewura kutotekeleza agizo la Waziri Mkuu aliyepita na badala yake taasisi hizo zimeendelea kuitaka Zanzibar kununua umeme kwa bei mpya.

“Tunashangazwa na Ewura kushindwa kutekeleza agizo la Waziri Mkuu na kuona Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco Idris Rashidi amewaandikia Ewura namna ya kutafuta mshauri mwelekezi wa kuangalia bei ya umeme kwa Zanzibar pamoja na kufungwa mkataba mpya kati ya ZECO na Tanesco,” alisema.

Akitoa ufafanuzi wa suala hilo, Waziri Kiongozi Shamsi Vuai Nahodha alisema ni kweli barua walioandikiwa kutoka Tanesco ilikuwa na lugha kama za vitisho kwa serikali.

Alisema suala hilo hivi sasa lipo katika ngazi ya waziri kiongozi na Waziri Mkuu kutokana na suala lenyewe kuwagusa wananchi na kuongeza kuwa iwapo bei hizo zilizotajwa zitalipwa, huenda uchumi wa Zanzibar ukayumba.
 
Pinda: Zanzibar si nchi, ni sehemu ya Muungano

Basil Msongo, Dodoma
Daily News; Friday,July 04, 2008 @00:03

Waziri Mkuu Mizengo Pinda amelieleza Bunge kuwa Zanzibar siyo nchi bali ni sehemu ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania yenye Serikali mbili, ambazo ni Serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ).

Waziri Mkuu alitoa msimamo huo alipojibu swali la Mbunge wa Chwaka, Yahya Kassim Issa (CCM) wakati wa muda wa wabunge kumuuliza maswali ya papo hapo jana. Mbunge huyo alihoji sababu za Zanzibar kutokuwa nchi wakati ina serikali yake, wimbo wake wa taifa, bendera yake, mihimili yake na ina Rais wake na kwamba, bila Zanzibar kusingekuwa na Tanzania.

“Hii ni nchi moja ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni nchi moja lakini yenye Serikali mbili,” alisema Pinda wakati akimjibu Issa bungeni kabla ya kuanza kwa kipindi cha kawaida cha maswali na majibu. Waziri Mkuu alilieleza Bunge kuwa, hakuna suala la Zanzibar kuwa nchi labda katiba itakapobadilishwa.

Wakati akijibu maswali ya wabunge wengine, Waziri Mkuu alisema atamuagiza Mkuu wa Polisi nchini, Said Mwema na wasaidizi wake wachunguze sababu za wanawake kuuawa kwa kukatwa makoromeo wilayani Tandahimba mkoani Mtwara.

Mbunge wa Tandahimba, Juma Njwayo (CCM) alilieza Bunge jana kuwa, hadi sasa wanawake sita wameuawa jimboni humo kwa kukatwa makoromeo wakiwamo kutoka kijiji cha Milidu na kwamba wananchi wanaishi kwa hofu.

Kwa mujibu wa Njwayo bungeni wakati Pinda akijibu maswali ya wabunge, Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa imeshindwa kukomesha mauaji hayo. Waziri Mkuu alisema hafahamu kiini cha mauaji hayo kwa kuwa wapo wanaouawa kwa sababu za imani za uchawi, na wengine kwa sababu za kupata madini, hivyo suala hilo litachunguzwa.

Hata hivyo, alisema mauaji hayo ni jambo jipya. Wakati akijibu swali kuhusu suala la ujenzi wa maghorofa, Waziri Mkuu alisema anakubali wazo la kuendeleza miji kwa kujenga maghorofa, lakini kuna tatizo la usimamizi wa ujenzi wa majengo hayo.
 
..wazanzibari wanachokozwa hapo, i wish ningekuwa maskani za michenzani jioni hii!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…