BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,165
Date::7/24/2008
Waziri Mkuu Pinda akiri hoja ya Zanzibar ni nzito kwake
*Asema wanaoendeleza hawamtakii mema
*Aitwisha CCM mzigo ili itoe tamko rasmi
*Spika atumia kiti chake kuzima mjadala'
Ramadhan Semtawa na Michael Uledi, Dodoma
Mwananchi
HOJA kwamba Zanzibar si nchi imemfika shingoni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda; na sasa amekiomba chama chake, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuitolea kauli kwa sababu kwa jinsi linavyochukuliwa kwa watu hawamtakii mema.
Pinda ambaye mara mbili ametoa kauli katika Mkutano wa Bunge wa 12 unaoendelea kwamba Zanzibar si nchi, jana hakutaka kusema lolote juu ya maswali matatu yaliyokuwa yanamwelekeza kwenye hoja hiyo kwa kile alichosema kwamba, "Mheshimiwa Mnyaa hanitakii mema."
Kauli ya Pinda ilitokana na swali la Mbunge wa Mkanyageni (CUF), Habibu Juma Mnyaa, aliyeuliza swali la mtego kwamba: "Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa kuwa una uzoefu wa kufanya kazi Ikulu kwa muda mrefu na kwa kuwa wewe ni mwanasheria, hivi Katiba ya Jamhuri ya Muungano na Article of Union (Mkataba wa Muungano) kipi kiko juu?"
Baada ya swali hilo, Pinda ambaye amejizolea umaarufu kwa kujibu maswali ya wabunge kwa utulivu na umakini, alianza kushusha pumzi kisha akasema: "Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mnyaa hanitakii mema, leo (jana) nimesikia Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imezima maandamano dhidi ya Pinda, sasa sikutaka sana kuliendeleza hili.
"Chochote nitakachokujibu nitakuwa nikizidi kuendeleza malumbano juu ya jambo hili, tayari niliagiza wanasheria wakuu wakae na kuliangalia hili, sasa kuanza tena kulijadili, ahaa?"
Hata hivyo, Pinda alisema kutokana na mwelekeo wa mjadala huo kuchukua taswira tofauti, ni vema sasa CCM ikalichukua na kulijadili kisha kulitolea kauli.
Baada ya hayo, Mnyaa alisimama tena kutaka kuuliza swali la nyongeza ndipo Spika alipoingilia kati na akasema: "Unataka kuuliza swali hilo hilo, kama unataka kuuliza hilo itakuwa ni sawa na vurugu, kwani tayari Waziri Mkuu amekwishasema linashughulikiwa na wanasheria wakuu."
Kama watu waliokuwa wameagana kuibua hoja ya Zanzibar si nchi, baada ya Mnyaa, aliibuka Mbunge wa Konde (CUF), Dk Ali Tarab Ali, alisimama na kuhoji mantiki ya kauli ya Pinda ya kuagiza CCM ichukue suala hilo na kulitolea kauli kwani si la kisiasa bali ni la wananchi.
Dk Ali pia aliuliza kwamba kwa kuwa suala hilo ni la wananchi kwa nini kusiwepo mjadala wa kitaifa kuhusu Muungano kabla ya mambo hayajaharibika huko mbele?
Baada ya swali hilo, kabla ya kumpa Waziri Mkuu nafasi ya kujibu, Spika alizima tena mjadala huo akisema kanuni ya 53 (8) iko bayana kwamba, jambo likishaamuliwa katika mkutano uliopo, mbunge haruhusiwi kulijadili tena.
Spika aliongeza kwamba Waziri Mkuu alipojibu swali kama hilo wiki iliyopita na kuagiza wanasheria wakuu wa SMZ na Bara, walichukue suala hilo na kuliangalia kisha kutoa tafsiri ya kisheria wabunge walipiga makofi wakishangalia wakionyesha kuunga mkono na kuongeza kwamba: "Kwa hiyo ruling (uamuzi) yangu ni kwamba hilo nalo haliendelezwi tena."
Pamoja na Spika kuzima mjadala huo, aliibuka Mbunge wa Chambani (CUF), Salim Hemed Khamisi, akijaribu kuibua suala hilo kwa mlango wa nyuma, lakini hoja yake ikaonekana kushindwa kugusia suala la Muungano hasa kama Zanzibar ni nchi au la.
Aliuliza maniki ya wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na Baraza la Wawakilishi Zanzibar, kuuunga mkono kwa kiwango cha theluthi mbili katika mambo mazito yanayohusu Muungano.
Baada ya kuulizwa swali hilo, Spika alisema ni jambo zuri kabla ya kumwita Pinda ambaye naye alisema: "Hilo ni jambo zuri tu, kwani inapofika katika mambo mazito lazima kuwe na uungwaji mkono wa kiwango cha theluthi mbili kutoka kila upande."
Kufuatia majibu hayo, Khamisi aliuliza tena kwamba kutokana na hali hiyo nafasi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliingizwa kinyume cha katiba mwaka 1994 kwa kile alichodai kwamba wakati wa kufanya mabadiliko hayo ilichukuliwa theluthi mbili ya wabunge wote badala ya kila upande.
Hata hivyo, kauli hiyo ilipingwa na Spika ambaye alisema si kweli kwamba ilifanyika hivyo kwani wakati wa mabadiliko hayo alikuwa ni Waziri wa Katiba na Sheria.
Tangu Pinda atoe kauli kwamba Zanzibar si nchi, umeibuka mjadala mkali ambao unaonyesha kuutikisha Muungano, kutokana na baadhi ya wanasiasa kutaka Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Amani Abei Karume, atoe kauli juu ya utata huo.
Kabla ya kufikiwa kwa kauli hizo, tayari Mwanasheria Mkuu wa SMZ, Iddi Pandu Hassan alikwisha kutoa kauli kwenye Baraza la Wawakilishi kwamba akimjibu Pinda kwamba Zanzibar ni nchi.
Hassan alisema kwamba Pinda alikuwa ameteleza kwa kauli yake, lakini Pinda aliirejea bungeni kwamba hakuteleza ili aliitoa kulingana na sheria za nchi zilivyo. Pinda alisema anafahamu utata unaozungumziwa kuwa ni suala la dola (sovereignty) na kuwataka wanasheria wa SMZ na Muungano kukutana kujadili suala hilo.
Miongoni mwa wanasiasa kwa upande wa CCM waliojitokeza kuzungumzia suala hilo njia ya Bunge ni Mkuu Kitengo cha Propaganda, Hizza Tambwe, aliyemuunga mkono Waziri Mkuu kwamba Zanzibar si nchi bali ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hadi sasa Wazanzibari bila kujali itikadi zao za vyama wameungana kumjia juu Pinda kwa kusema ameshusha hadhi ya visiwa hivyo huku wengine wakienda mbali wakimtaka Rais Karume aitoe Zanzibar kwenye Muungano.
Tayari hali hiyo imefanya pia baadhi ya Wazanzibari kupanga kufanya maandamano kulaani kauli ya Pinda, lakini SMZ imeyazima. Ingawa yalipata kibali cha polisi, Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho, alikataa kuyapokea kwa maelezo kwamba eneo la Baraza linahitaji utulivu wakati huu wa kujadili na kupitisha bajeti ya serikali ya mwaka 2008/09.
Kutoka Zanzibar, Salma Said, anaripoti kuwa baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wamesema Zanzibar sio taasisi ya Tamisemi na wala haitakuwa hivyo kwa kuwa ni nchi yenye mamlaka yake kamili na ndio Kituo Cha Afrika Mashariki na Kati Cha Utafiti wa Simulizi za Asili na Lugha za Afrika (EACROTANAL) Zanzibar.
Wakichangia makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo ya mwaka wa fedha wa 2008/09 katika kikao cha Baraza la Wawakilishi wajumbe hao walisema suala la Zanzibar kuwa nchi haliwezi kuepukwa kwa hali yoyote ile hadi hapo tamko rasmi litakapotolewa.
Mwakilishi wa Jimbo la Koani (CCM) Haji Mkema Haji, alisema kutoka na kuwa Zanzibar kuwa nchi ndiyo maana jengo la EACROTANAL likajengewa Wazanzibari kwa kuwa wanafahamika kuwa wao ni watu wenye nchi kamili yenye mamlaka yake bila ya kuingiliwa na mtu yeyote.
?Mheshimiwa mwenyekiti Zanzibar ni nchi yenye mamlaka na sio Taasisi ya Tamisemi na wala haitakuwa na ndio maana tukatoa nyumba ile ya EACROTANAL haikujengwa Msumbuji wala Comoro imejengwa hapa kwa Wazanzibari,? alisema Haji. Tamisemi ni Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.
Haji alisema hakuna haja ya kutafutwa mambo ya kisheria kuhusu suala la Zanzibar kwani kila jambo linafahamika, hata suala la kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki linajulikana undani wake kwa kuwa wenyewe ndio walijitoa.
Akitilia mkazo kauli hiyo, Mwakilishi wa Jimbo la Gando (CUF), Said Ali Mbarouk, alisema katika suala la Zanzibar kuwa ni nchi au siyo, hilo halina mjadala linafahamika na Wazanzibari hawatataka kusikia lolote kwa kuwa wanajua Zanzibar ni nchi kamili.
''Katika suala la Zanzibar nchi au sio nchi hilo Mheshimiwa Mwenyekiti hatuna compromise (suluhu)'' alisema Mbarouk huku pande zote zikiwa zinapiga makofi na kuaza mazungumzo ya chini chini.
Kwa upande wake Kiongozi wa Kambi ya Upinzani, Abubakar Khamis Bakari, alisema tatizo la kudhalilishwa Wazanzibari linatokana na wenyewe kwa kushindwa kuheshimiana.
''Tunajidhalilisha wenyewe na hili nalizungumza kwa nia safi kabisa ndio haya yanatotokea?.tunaambiwa Zanzibar sio nchi jamani haya mambo tuyaangalie,'' alisema Abubakar ambaye ni Mwakilishi wa Jimbo la Magogoni (CUF).
''Sio mara moja nimeshawahi kumwambia Waziri Kiongozi kuwa yeye sio Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, lakini yeye ni Waziri Kiongozi wa Zanzibar ni wa Wazanzibari wote hili nalisema kwa nia safi kuanzia sasa aitwe Waziri Kiongozi wa Zanzibar,'' alisema Abubakar.
Waziri Mkuu Pinda akiri hoja ya Zanzibar ni nzito kwake
*Asema wanaoendeleza hawamtakii mema
*Aitwisha CCM mzigo ili itoe tamko rasmi
*Spika atumia kiti chake kuzima mjadala'
Ramadhan Semtawa na Michael Uledi, Dodoma
Mwananchi
HOJA kwamba Zanzibar si nchi imemfika shingoni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda; na sasa amekiomba chama chake, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuitolea kauli kwa sababu kwa jinsi linavyochukuliwa kwa watu hawamtakii mema.
Pinda ambaye mara mbili ametoa kauli katika Mkutano wa Bunge wa 12 unaoendelea kwamba Zanzibar si nchi, jana hakutaka kusema lolote juu ya maswali matatu yaliyokuwa yanamwelekeza kwenye hoja hiyo kwa kile alichosema kwamba, "Mheshimiwa Mnyaa hanitakii mema."
Kauli ya Pinda ilitokana na swali la Mbunge wa Mkanyageni (CUF), Habibu Juma Mnyaa, aliyeuliza swali la mtego kwamba: "Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa kuwa una uzoefu wa kufanya kazi Ikulu kwa muda mrefu na kwa kuwa wewe ni mwanasheria, hivi Katiba ya Jamhuri ya Muungano na Article of Union (Mkataba wa Muungano) kipi kiko juu?"
Baada ya swali hilo, Pinda ambaye amejizolea umaarufu kwa kujibu maswali ya wabunge kwa utulivu na umakini, alianza kushusha pumzi kisha akasema: "Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mnyaa hanitakii mema, leo (jana) nimesikia Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imezima maandamano dhidi ya Pinda, sasa sikutaka sana kuliendeleza hili.
"Chochote nitakachokujibu nitakuwa nikizidi kuendeleza malumbano juu ya jambo hili, tayari niliagiza wanasheria wakuu wakae na kuliangalia hili, sasa kuanza tena kulijadili, ahaa?"
Hata hivyo, Pinda alisema kutokana na mwelekeo wa mjadala huo kuchukua taswira tofauti, ni vema sasa CCM ikalichukua na kulijadili kisha kulitolea kauli.
Baada ya hayo, Mnyaa alisimama tena kutaka kuuliza swali la nyongeza ndipo Spika alipoingilia kati na akasema: "Unataka kuuliza swali hilo hilo, kama unataka kuuliza hilo itakuwa ni sawa na vurugu, kwani tayari Waziri Mkuu amekwishasema linashughulikiwa na wanasheria wakuu."
Kama watu waliokuwa wameagana kuibua hoja ya Zanzibar si nchi, baada ya Mnyaa, aliibuka Mbunge wa Konde (CUF), Dk Ali Tarab Ali, alisimama na kuhoji mantiki ya kauli ya Pinda ya kuagiza CCM ichukue suala hilo na kulitolea kauli kwani si la kisiasa bali ni la wananchi.
Dk Ali pia aliuliza kwamba kwa kuwa suala hilo ni la wananchi kwa nini kusiwepo mjadala wa kitaifa kuhusu Muungano kabla ya mambo hayajaharibika huko mbele?
Baada ya swali hilo, kabla ya kumpa Waziri Mkuu nafasi ya kujibu, Spika alizima tena mjadala huo akisema kanuni ya 53 (8) iko bayana kwamba, jambo likishaamuliwa katika mkutano uliopo, mbunge haruhusiwi kulijadili tena.
Spika aliongeza kwamba Waziri Mkuu alipojibu swali kama hilo wiki iliyopita na kuagiza wanasheria wakuu wa SMZ na Bara, walichukue suala hilo na kuliangalia kisha kutoa tafsiri ya kisheria wabunge walipiga makofi wakishangalia wakionyesha kuunga mkono na kuongeza kwamba: "Kwa hiyo ruling (uamuzi) yangu ni kwamba hilo nalo haliendelezwi tena."
Pamoja na Spika kuzima mjadala huo, aliibuka Mbunge wa Chambani (CUF), Salim Hemed Khamisi, akijaribu kuibua suala hilo kwa mlango wa nyuma, lakini hoja yake ikaonekana kushindwa kugusia suala la Muungano hasa kama Zanzibar ni nchi au la.
Aliuliza maniki ya wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na Baraza la Wawakilishi Zanzibar, kuuunga mkono kwa kiwango cha theluthi mbili katika mambo mazito yanayohusu Muungano.
Baada ya kuulizwa swali hilo, Spika alisema ni jambo zuri kabla ya kumwita Pinda ambaye naye alisema: "Hilo ni jambo zuri tu, kwani inapofika katika mambo mazito lazima kuwe na uungwaji mkono wa kiwango cha theluthi mbili kutoka kila upande."
Kufuatia majibu hayo, Khamisi aliuliza tena kwamba kutokana na hali hiyo nafasi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliingizwa kinyume cha katiba mwaka 1994 kwa kile alichodai kwamba wakati wa kufanya mabadiliko hayo ilichukuliwa theluthi mbili ya wabunge wote badala ya kila upande.
Hata hivyo, kauli hiyo ilipingwa na Spika ambaye alisema si kweli kwamba ilifanyika hivyo kwani wakati wa mabadiliko hayo alikuwa ni Waziri wa Katiba na Sheria.
Tangu Pinda atoe kauli kwamba Zanzibar si nchi, umeibuka mjadala mkali ambao unaonyesha kuutikisha Muungano, kutokana na baadhi ya wanasiasa kutaka Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Amani Abei Karume, atoe kauli juu ya utata huo.
Kabla ya kufikiwa kwa kauli hizo, tayari Mwanasheria Mkuu wa SMZ, Iddi Pandu Hassan alikwisha kutoa kauli kwenye Baraza la Wawakilishi kwamba akimjibu Pinda kwamba Zanzibar ni nchi.
Hassan alisema kwamba Pinda alikuwa ameteleza kwa kauli yake, lakini Pinda aliirejea bungeni kwamba hakuteleza ili aliitoa kulingana na sheria za nchi zilivyo. Pinda alisema anafahamu utata unaozungumziwa kuwa ni suala la dola (sovereignty) na kuwataka wanasheria wa SMZ na Muungano kukutana kujadili suala hilo.
Miongoni mwa wanasiasa kwa upande wa CCM waliojitokeza kuzungumzia suala hilo njia ya Bunge ni Mkuu Kitengo cha Propaganda, Hizza Tambwe, aliyemuunga mkono Waziri Mkuu kwamba Zanzibar si nchi bali ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hadi sasa Wazanzibari bila kujali itikadi zao za vyama wameungana kumjia juu Pinda kwa kusema ameshusha hadhi ya visiwa hivyo huku wengine wakienda mbali wakimtaka Rais Karume aitoe Zanzibar kwenye Muungano.
Tayari hali hiyo imefanya pia baadhi ya Wazanzibari kupanga kufanya maandamano kulaani kauli ya Pinda, lakini SMZ imeyazima. Ingawa yalipata kibali cha polisi, Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho, alikataa kuyapokea kwa maelezo kwamba eneo la Baraza linahitaji utulivu wakati huu wa kujadili na kupitisha bajeti ya serikali ya mwaka 2008/09.
Kutoka Zanzibar, Salma Said, anaripoti kuwa baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wamesema Zanzibar sio taasisi ya Tamisemi na wala haitakuwa hivyo kwa kuwa ni nchi yenye mamlaka yake kamili na ndio Kituo Cha Afrika Mashariki na Kati Cha Utafiti wa Simulizi za Asili na Lugha za Afrika (EACROTANAL) Zanzibar.
Wakichangia makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo ya mwaka wa fedha wa 2008/09 katika kikao cha Baraza la Wawakilishi wajumbe hao walisema suala la Zanzibar kuwa nchi haliwezi kuepukwa kwa hali yoyote ile hadi hapo tamko rasmi litakapotolewa.
Mwakilishi wa Jimbo la Koani (CCM) Haji Mkema Haji, alisema kutoka na kuwa Zanzibar kuwa nchi ndiyo maana jengo la EACROTANAL likajengewa Wazanzibari kwa kuwa wanafahamika kuwa wao ni watu wenye nchi kamili yenye mamlaka yake bila ya kuingiliwa na mtu yeyote.
?Mheshimiwa mwenyekiti Zanzibar ni nchi yenye mamlaka na sio Taasisi ya Tamisemi na wala haitakuwa na ndio maana tukatoa nyumba ile ya EACROTANAL haikujengwa Msumbuji wala Comoro imejengwa hapa kwa Wazanzibari,? alisema Haji. Tamisemi ni Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.
Haji alisema hakuna haja ya kutafutwa mambo ya kisheria kuhusu suala la Zanzibar kwani kila jambo linafahamika, hata suala la kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki linajulikana undani wake kwa kuwa wenyewe ndio walijitoa.
Akitilia mkazo kauli hiyo, Mwakilishi wa Jimbo la Gando (CUF), Said Ali Mbarouk, alisema katika suala la Zanzibar kuwa ni nchi au siyo, hilo halina mjadala linafahamika na Wazanzibari hawatataka kusikia lolote kwa kuwa wanajua Zanzibar ni nchi kamili.
''Katika suala la Zanzibar nchi au sio nchi hilo Mheshimiwa Mwenyekiti hatuna compromise (suluhu)'' alisema Mbarouk huku pande zote zikiwa zinapiga makofi na kuaza mazungumzo ya chini chini.
Kwa upande wake Kiongozi wa Kambi ya Upinzani, Abubakar Khamis Bakari, alisema tatizo la kudhalilishwa Wazanzibari linatokana na wenyewe kwa kushindwa kuheshimiana.
''Tunajidhalilisha wenyewe na hili nalizungumza kwa nia safi kabisa ndio haya yanatotokea?.tunaambiwa Zanzibar sio nchi jamani haya mambo tuyaangalie,'' alisema Abubakar ambaye ni Mwakilishi wa Jimbo la Magogoni (CUF).
''Sio mara moja nimeshawahi kumwambia Waziri Kiongozi kuwa yeye sio Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, lakini yeye ni Waziri Kiongozi wa Zanzibar ni wa Wazanzibari wote hili nalisema kwa nia safi kuanzia sasa aitwe Waziri Kiongozi wa Zanzibar,'' alisema Abubakar.