Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kero zake: Je, tuuvunje?
Ninataka kununua gari huko zanzibar kisha nilitumie bara, nitumie njia gani maana kule bei zao ndogo kuliko huku kwa Dp world

Ishu ipo TRA hapa dar mkuu, kwahiyo kabla ya kuniunua gari unayoitaka jaribu kuulizia watakulipisha kiasi gani ili upate kupiga hisabau zako vizuri
 
Tujadili kwa hoja sasa,

Hivi tuuseme ukweli kabisa ni nini faida mtanganyika anaipata kutokana na muungano na zanzibar?
Maana kwa mfano mzanzibar bodi ya mikopo zanzibar anapata mkopo na akifika tanganyika anapata tena mkopo.

Mzanzibar anapata ajira yoyote tanganyika lakini mtanganyika hapati kazi yoyote kule zanzibar.

Mtanganyika kununua na kumiliki ardhi zanzibar ni shughuli pevu sana lakini mzanzibar ananunua ardhi, mashamba na kadhalika tanganyika.

Mtanganyika huwezi kupata kitambulisho cha mzanzibar ili uwe na haki sawa na mzanzibar wakati huo mzanzibar analamba kitambulisho cha NIDA na kile cha uzanzibar yaani kiufupi mzanzibar ana uraia pacha kwa wakati mmoja, ana uraia wa zanzibar na anamiliki haki ya uraia wa tanganyika.

Mtanganyika kuingia zanzibar kama sio kuonesha passport basi uwe na kitambulisho ndio utaruhusiwa kuingia kwao lakini wao huingia tanganyika bila kitambulisho.

Halafu wao wakitamka neno zanzibar sio kosa wewe mtanganyika ukitamka mimi mtanganyika ni kosa ambalo halina kifungu cha sheria zaidi utaanza kuambiwa wewe mchochezi unavuruga amani na blah blah kibao
Mtanganyika hauwezi kuteuliwa nafasi za mkurugenzi, mkuu wa wilaya, kule zanzibar lakini wao wanateuliwa na wanalipwa na tanganyika, hadi mafao watalipwa.

Mtanganyika huwezi kugombea cheo kule zanzibar lakini wao ruksa kugombea tanganyika,
Muungano huu kiukweli hauna usawa na watanganyika wamechoshwa kunangwa kila leo na wanasiasa wa zanzibar kuonekana kwamba Watanganyika wanalazimisha muungano wakati ukweli hata uitishe kura ya maoni leo hutopata mtanganyika wa kuunga mkono muungano na kwanza kuna watanganyika wengi vijijini hawajui kama Zanzibar ni nchi wao wanajua zanzibar ni mkoa,
 
Tujadili kwa hoja sasa,
Hivi tuuseme ukweli kabisa ni nini faida mtanganyika anaipata kutokana na muungano na zanzibar?
Maana kwa mfano mzanzibar bodi ya mikopo zanzibar anapata mkopo na akifika tanganyika anapata tena mkopo,
Mzanzibar anapata ajira yoyote tanganyika lakini mtanganyika hapati kazi yoyote kule zanzibar.
Mtanganyika kununua na kumiliki ardhi zanzibar ni shughuli pevu sana lakini mzanzibar ananunua ardhi, mashamba na kadhalika tanganyika
Mtanganyika huwezi kupata kitambulisho cha mzanzibar ili uwe na haki sawa na mzanzibar wakati huo mzanzibar analamba kitambulisho cha NIDA na kile cha uzanzibar yaani kiufupi mzanzibar ana uraia pacha kwa wakati mmoja, ana uraia wa zanzibar na anamiliki haki ya uraia wa tanganyika,
Mtanganyika kuingia zanzibar kama sio kuonesha passport basi uwe na kitambulisho ndio utaruhusiwa kuingia kwao lakini wao huingia tanganyika bila kitambulisho,
Halafu wao wakitamka neno zanzibar sio kosa wewe mtanganyika ukitamka mimi mtanganyika ni kosa ambalo halina kifungu cha sheria zaidi utaanza kuambiwa wewe mchochezi unavuruga amani na blah blah kibao
Mtanganyika hauwezi kuteuliwa nafasi za mkurugenzi, mkuu wa wilaya, kule zanzibar lakini wao wanateuliwa na wanalipwa na tanganyika, hadi mafao watalipwa
Mtanganyika huwezi kugombea cheo kule zanzibar lakini wao ruksa kugombea tanganyika,
Muungano huu kiukweli hauna usawa na watanganyika wamechoshwa kunangwa kila leo na wanasiasa wa zanzibar kuonekana kwamba watanganyika wanalazimisha muungano wakati ukweli hata uitishe kura ya maoni leo hutopata mtanganyika wa kuunga mkono muungano na kwanza kuna watanganyika wengi vijijini hawajui kama Zanzibar ni nchi wao wanajua zanzibar ni mkoa,
Takataka nani anayejua ZNZ ni mkoa?

Hata darasa la 7 hajamaliza makaratasi ya kujibia mtihani?
 
Angalia in Big picture.

Viwanda vya Zanzibar haviruhusiwi kuuza Tanganyika, ila Vya Tanganyika vinauza Zanzibar, Zanzibar wana kiwanda cha Sukari ila kinaishia kule kule, hata wakiwa na surplus haiji kuuzwa huku, hii inasababisha Uwekezaji Zanzibar kutokua mzuri na kudhoofisha uchumi wao.

Walikua na umeme wao wenyewe umeuliwa Wanapewa na Tanesco, Kifupi Tanganyika wanatumia huu Mtego kuifanya Zanzibar iwe dependent na huku Bara na wasiwe na Maendeleo.
 

Sababu hii ni mfu kwa dunia ya sasa, ukumbuke muungano wakati wanaungana Nyerere na Karume hawakuitisha kura ya maoni kwa wananchi wa pande zote, yaani wazanzibar muungano hawautaki na watanganyika muungano hawautaki isipokua wenye nafasi za kisiasa ndio wanautaka muungano lakini tofauti na hapo hamna la zaidi
 
Angalia in Big picture.

Viwanda vya Zanzibar haviruhusiwi kuuza Tanganyika, ila Vya Tanganyika vinauza Zanzibar, Zanzibar wana kiwanda cha Sukari ila kinaishia kule kule, hata wakiwa na surplus haiji kuuzwa huku, hii inasababisha Uwekezaji Zanzibar kutokua mzuri na kudhoofisha uchumi wao.

Walikua na umeme wao wenyewe umeuliwa Wanapewa na Tanesco, Kifupi Tanganyika wanatumia huu Mtego kuifanya Zanzibar iwe dependent na huku Bara na wasiwe na Maendeleo.

Kile kiwanda hakizalishi sukari ya kutosha mahonda wanaimport sukari bei rahisi kutoka uarabuni halafu wanafanya packaging kwa label zao, hiyo ilifanya serikali ikawapiga bann kuingiza aina hiyo ya sukari huko bara,
 
Mleta uzi umeandika ushuzi mtupu. Sasa unataka wazanzibari wapoteze urithi wao wote kwa wabara kwa sababu ya Muungano? Wabara ina ardhi kubwa mno isiyotumika kwanini tusiitumie hadi kwenda kuchukua kakipande kadogo ka ardhi ya Zanzibar? Tuheshimu historia na utaifa wa Zanzibar. Hatukuungana ili kuipoteza Zanzibar.
 
Mleta uzi umeandika ushuzi mtupu. Sasa unataka wazanzibari wapoteze urithi wao wote kwa wabara kwa sababu ya Muungano? Wabara ina ardhi kubwa mno isiyotumika kwanini tusiitumie hadi kwenda kuchukua kakipande kadogo ka ardhi ya Zanzibar? Tuheshimu historia na utaifa wa Zanzibar. Hatukuungana ili kuipoteza Zanzibar.
Kwahiyo Zanzibar iwe na haki kwa kila kitu lakini bara haina haki yoyote? wapuuzi nyie hatuwataki huku rudini kwenu
 
Sababu hii ni mfu kwa dunia ya sasa, ukumbuke muungano wakati wanaungana Nyerere na Karume hawakuitisha kura ya maoni kwa wananchi wa pande zote, yaani wazanzibar muungano hawautaki na watanganyika muungano hawautaki isipokua wenye nafasi za kisiasa ndio wanautaka muungano lakini tofauti na hapo hamna la zaidi
Ukweli hatuutaki hata kidogo
 
Tunawaomba Watanzania wa dini zote,Waislamu, Wakristo,Wachungaji na Mashehe na WA jadi, tufunge tarehe 14,15,16 kuomba mapenzi ya Mungu yakafanyike kwa Tanganyika na Tanzania, ahsanteni sana.
Wakili Boniface Mwabukusi.
Mwisho wa kunukuu....
 
Back
Top Bottom