FRANCIS DA DON
JF-Expert Member
- Sep 4, 2013
- 38,920
- 44,970
safi......!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ulipofika kwa messi nimeacha kusoma unataka niamini kwamba Ronaldo ni zaidi ya messi ??
kwa kipi ??
Mada yako imeharibika Diamond mlinganishe na Ronaldo sawa ila kiba usimlinganishe na Messi
Messi ana tuzo nyingi kuliko Ronaldo na ana rekodi kubwa kuliko Ronaldo
Na rekodi zingine hazioti kwamba kuna siku atamkuta Messi
ni hayo tu.
Humu jamvini kuna vichwa bwana, angalau Mbumbu nao wa kubishana mambo yasikuwa na msingi wamejaa.
ha ha ha ha haaaaa daaaah unatu tusi mkubwa!!!!
Andiko zuri lakini kuna mambo ya kuangalia kwa wasanii wetu hapa Tanzania.
Ukiondoa Joseph Haule - Prof. J, wengine siwafahamu sana lakini huyu ndiye mtu ambaye kwa umri wake anafanya mambo yanayostahili kufanywa na mtu wa aina hiyo. Mfano Ana familia yenye heshima zote, hii inashabihiana na wasanii maarufu wa nchi kama Uganda maana wanaishi maisha yanayoelezeka.
Sasa huyu kijana wetu angeweka wazi lifestyle yake ingesaidia wengine, japo yeye anaita 'kazi na dawa' huenda huyu aliyempata sasa akamplekeka kusiko na sio muda atakuwa anasema 'inzi kufia kwenye kidonda...'
Ni kweli Mkuu. Heshima ya 20% iko pale pale. Haitobadilika kwamba alikuwa msanii wa kwanza kutengeneza historia ya kutwaa tuzo 5 nchini. Lakini hata hoja ya hapo pia si mbaya, ni kwamba kuna wasanii walikuwa na zama zao, lakini tungependa kuona mwisho wenye heshima zaidi. Ina Maana zile tuzo ndizo zilizokuwa tamati ya kipaji chake?
Zama za mwisho kwa kitabu cha nabii ni kifo tu! Ila hapa tuiweke hivi, 'Mwisho wa Zama za Msanii, ni aidha kifo ama kustaafu kwa heshima''. Tusije tukasapoti uzembe mkuu. Ni lazima wasanii wetu wapendwa wajue wanakosea wapi!
Wewe ni luqman mwenyewe au umecopy na kuileta hapa?Uko sahihi! Lakini hapa ililengwa zaidi kwenye tofauti zao za Kipaji & Jitihada. Messi ana kipaji, na Ronaldo ana jitihada. Ila Una hoja nzuri Mkuu!
Tuko pamojaUkweli hauna tabia ya kubembelezwa!
sijui why mleta mada kachagua hiyo picha,20% hapo alikuwa kwenye mazishi ya mzazi wake si unaona hata sura ya huzuni,hii thread ina ukweli ila mleta mada ana lengo lake kwanza anaonekana ni team wasafi mpaka anashuka na kamba kwenye helicopta yeye na diamond dar live,yeye anatumika akiombwa na diamond kukutanisha ashindanishwe na msanii mwingine,we unaombwa msanii umkutanishe na mimi hapo lazima mna lenu.Mimi hiyo picha tu ya 20% nimecheka sana
Mwanangu Kiba we endelea kufanya yako kama unavyotaka. Usiige akili ya mtu maana huku kuigaiga, nawe unaweza jikuta ukitumbuiza na boksa jukwaani.