Muziki kama Pesa: Iga Akili ya Diamond, Usiige ubongo wa 20%

Muziki kama Pesa: Iga Akili ya Diamond, Usiige ubongo wa 20%

Iga Akili ya Diamond,Usiige ubongo wa 20%?


  • Diamond ana Akili ila hana ubongo?
  • 20% ana ubongo ila hana Akili?

Mwandishi anapaswa pia kumpa heshima yake 20% hata kama lengo lake ni kumpongeza Diamond.

"Kila kitabu kina zama zake". Ni suala tu wa wakati...
 
Ulipofika kwa messi nimeacha kusoma unataka niamini kwamba Ronaldo ni zaidi ya messi ??
kwa kipi ??
Mada yako imeharibika Diamond mlinganishe na Ronaldo sawa ila kiba usimlinganishe na Messi
Messi ana tuzo nyingi kuliko Ronaldo na ana rekodi kubwa kuliko Ronaldo

Na rekodi zingine hazioti kwamba kuna siku atamkuta Messi

ni hayo tu.

Mkubwa MO11 ndugu hapo ameandika kadri ya ufahamu,muono na hatimae ushauri. Sina hakika sana lakini yawezekana ulinganifu alioufanya kati ya Mess na Ronaldo yuko sahihi.
 
Andiko zuri lakini kuna mambo ya kuangalia kwa wasanii wetu hapa Tanzania.
Ukiondoa Joseph Haule - Prof. J, wengine siwafahamu sana lakini huyu ndiye mtu ambaye kwa umri wake anafanya mambo yanayostahili kufanywa na mtu wa aina hiyo. Mfano Ana familia yenye heshima zote, hii inashabihiana na wasanii maarufu wa nchi kama Uganda maana wanaishi maisha yanayoelezeka.
Sasa huyu kijana wetu angeweka wazi lifestyle yake ingesaidia wengine, japo yeye anaita 'kazi na dawa' huenda huyu aliyempata sasa akamplekeka kusiko na sio muda atakuwa anasema 'inzi kufia kwenye kidonda...'

Inawezekana huyu kijana wetu umri tu nao unasumbua,si unajua tena kaumri bado bado ukichanganya na sente nazo zinamwagika basi daaaah full kuwavua ch**i. Hata wewe ikitokea sasa hivi ukapewa mgao wa ESCROW weeee utawapanga!!!
 
Ni kweli Mkuu. Heshima ya 20% iko pale pale. Haitobadilika kwamba alikuwa msanii wa kwanza kutengeneza historia ya kutwaa tuzo 5 nchini. Lakini hata hoja ya hapo pia si mbaya, ni kwamba kuna wasanii walikuwa na zama zao, lakini tungependa kuona mwisho wenye heshima zaidi. Ina Maana zile tuzo ndizo zilizokuwa tamati ya kipaji chake?

Zama za mwisho kwa kitabu cha nabii ni kifo tu! Ila hapa tuiweke hivi, 'Mwisho wa Zama za Msanii, ni aidha kifo ama kustaafu kwa heshima''. Tusije tukasapoti uzembe mkuu. Ni lazima wasanii wetu wapendwa wajue wanakosea wapi!

Nimekubaliana nawe.

Nafurahia mafanikio ya yeyote anayefanya bidii.

Nasikitika ninapoona au kusikia mwenye kipaji amefanya uzembe na kupotea wakati bado anahitajika.

Pengine ipo haja pia ya kufahamu kipi kilichomkuta 20% hadi kufikia hapo alipo "from hero to zero?".

Unaweza ukashangaa hata huyo mwandishi pia anamchango wake katika kumdidimiza the so called asiigwe "ubongo wa 20%"
 
Uko sahihi! Lakini hapa ililengwa zaidi kwenye tofauti zao za Kipaji & Jitihada. Messi ana kipaji, na Ronaldo ana jitihada. Ila Una hoja nzuri Mkuu!
Wewe ni luqman mwenyewe au umecopy na kuileta hapa?

Nataka nashukuru vya kutosha maana makala ya daraja la kwanza hii.
 
Well said.. Kwenye fani nyingi tu Watanzania tuna tabia ya kuangalia around us.. Tunapenda kuwa samaki wakubwa kwenye vibwawa vidogo.. Tunaridhika mapema sana.. Ushauri huu uende pia kwa wenye fani nyingine pia..
 
Daaaaa hizi kashfa mweee hiv 20% yuko wap
 
Mimi hiyo picha tu ya 20% nimecheka sana
 
Mwanangu Kiba we endelea kufanya yako kama unavyotaka. Usiige akili ya mtu maana huku kuigaiga, nawe unaweza jikuta ukitumbuiza na boksa jukwaani.
 
Mimi hiyo picha tu ya 20% nimecheka sana
sijui why mleta mada kachagua hiyo picha,20% hapo alikuwa kwenye mazishi ya mzazi wake si unaona hata sura ya huzuni,hii thread ina ukweli ila mleta mada ana lengo lake kwanza anaonekana ni team wasafi mpaka anashuka na kamba kwenye helicopta yeye na diamond dar live,yeye anatumika akiombwa na diamond kukutanisha ashindanishwe na msanii mwingine,we unaombwa msanii umkutanishe na mimi hapo lazima mna lenu.
Nakubali diamond anajitihada ila mleta mada kasahau kuelezea scandal chafu za diamond ambazo anazitumia ili avume:
1.kubaki na vyupi halafu kubong'oa ye na dancers wake,lazima watu wa udaku watasambaza.
2.wananyonyana mate na wema halafu wanavujisha picha
3.project na zari
4.mara peni
5.acha hivi vidagaa vya kufunua ambavyo havisikiki
6.skendo chafu video nayo inatolewa hapo hapo.


HAYO MAMBO YOTE KIBA HANA na hajashuka kimziki hata leo
 
Mwanangu Kiba we endelea kufanya yako kama unavyotaka. Usiige akili ya mtu maana huku kuigaiga, nawe unaweza jikuta ukitumbuiza na boksa jukwaani.

Uwiiiii,siku akifanya hivyo nitapotea JF wiki nzima!
 
Back
Top Bottom