Muziki wa leo umeshindwa kuwa bora kuliko wa zamani

Muziki wa leo umeshindwa kuwa bora kuliko wa zamani

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
MUZIKI WA LEO UMESHINDWA KUWA BORA KAMA ZAMANI

My fellow citizens natumaini mko poa.

Nawasalimu kwa jina la Chama Cha Mapinduzi. Kwa siku kadhaa nilikuwa kimya hadi wengi wenu mkawa mnaniuliza nini kimenipata. Niwatoe hofu kwamba niko salama kabisa ila kwa sasa nimeona niongeze elimu kwa kujiunga na shule ya uongozi ya Komredi Polepole ambayo haina ada. Jumamosi hii Mwalimu Polepole atatufundisha kuhusu ujamaa na kujitegemea. Hiyo shule kwakweli ni madini matupu yanatolewa. Komredi Polepole adumu.

Kama wiki mbili zilizopita boss wa label ya Koffi Central ambaye ni ndugu wa damu wa Koffi Olomide aitwaye Tutu Robert, aliulizwa na shabiki anadhani ni albamu gani ilikuwa bora zaidi kwa Koffi Olomide na kundi zima la Quartier Latin? Tutu Roba akajibu yeye anaona kiufundi kwa maana ya tungo na mambo ya kimuziki albamu ya V12 ya mwaka 1995 ilikuwa bora zaidi. Hii albamu ndo yenye wimbo Andrada. Ila albamu zilizompa Koffi tuzo nyingi ni Loi na Effrakata. Kwangu mimi komredi Tutu Roba alijibu kisomi sana. Na pia nakubaliana nae kwamba ile albamu ya V12 ilikuwa bora mno. Hadi leo Andrada au Etat Major ya Extra Musica ikipigwa bar huwa inaleta vibe la hatari hadi kwa vijana wa umri mdogo.

Baada ya kusoma majibu ya Tutu Roba nikajikuta naenda mbali na kutafakari zaidi kuhusu muziki. Nikajiuliza kwanini albamu ya V12 iwe bora kuliko zingine zilizotoka miaka zaidi ya 20 baadae? Nikaachana na Koffi na kuanza kurudi kwenye miziki mingine hasa USA. Nikaona kwamba wanamuziki wa leo bado hawajaweza kuvunja rekodi zilizowekwa na wababe wa enzi hizo kwenye utamu wa muziki. Wanamuziki wa leo labda rekodi waliyovunja ni kutengeneza pesa nyingi kuliko kipindi kingine ila kiufundi bado. Kwa mfano kwenye slow jams kuna wakali wa leo ambao wana nyimbo tamu kuwazidi Mariah Carey, Whitney Houston, Boyz II men, na wakali wengine wa zamani. Au kwenye pop kuna mtu aliyeweza kuvunja utamu wa nyimbo za MJ? Tukija kwenye hiphop kuna mambo ya ovyo sana. Tungo nyingi za kishenzi mno. Unaweza google lyrics za vijana wa leo ukaona ushuzi unaoimbwa. Hadi leo hii wimbo wa SEYA ni hitsong ya kwenye sherehe hasa harusi.

Na sio wanamuziki wapya tu hata wakongwe waliokuwepo zamani hadi leo wameshindwa kutoa vitu vikali kama walivyowahi kuvitoa mwanzoni. Je tatizo ni nini? PESA. Tatizo ni pesa. Hii kitu imetuvuruga. Yaani mtu anaimba chochote ili mradi ataingiza pesa. Raia nao hawajali tena maadili wanachotaka ni burudani tu kwa namna yoyote.

Na kwa tulipofikia hakuna kitu tunaweza fanya kubadilisha hii hali zaidi ya kuacha tu watu wajiimbie wanavyoweza cha msingi wanapata riziki. Ni tatizo la dunia nzima sio Tanzania tu.
 
Nasikiza Burning Up ya Chakachaka kisha nitasikiliza Nitakupiga Nyembe ya Domo halafu nitarudi
 
Hapa wata mtaja diamond simba wa tandale wakati mwenzao kasha sema anafanya mziki apate hela hayo ya ujumbe mi naona mwende kanisan. Na mskitin
 
Jana nimetoka kudownload..Nyimba kama hamsini za miaka 80 mpaka 90..
Nadhani wakati mwingine ni suala la memories(inakupa kumbukumbu fulani ya nyakati za nyuma)..
Kipindi hicho kupata wimbo/mziki unaoupenda ilikua ni adimu sana..

Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app
 
Hapa wata mtaja diamond simba wa tandale wakati mwenzao kasha sema anafanya mziki apate hela hayo ya ujumbe mi naona mwende kanisan. Na mskitin
Alisema hayo baada ya kuona ameshindwa kukonga nyoyo za watu wenye akili!!! Pesa kapata ila tuache utani hana music!!! Huo ndo ukweli
 
Mkuu sio ukweli. Mziki unasababisha kitu inaitwa Nostalgia. Nostalgia ndio inasababisha tunaona nyimbo za zamani ni nzuri. Omba umri mrefu. Kuna nyimbo za 2013 utajaziona ni nzuri. Kasikilize nyimbo za 1890 uje utuambie hapa kama ni nzuri
 
MUZIKI WA LEO UMESHINDWA KUWA BORA KAMA ZAMANI

My fellow citizens natumaini mko poa.

Nawasalimu kwa jina la Chama Cha Mapinduzi. Kwa siku kadhaa nilikuwa kimya hadi wengi wenu mkawa mnaniuliza nini kimenipata. Niwatoe hofu kwamba niko salama kabisa ila kwa sasa nimeona niongeze elimu kwa kujiunga na shule ya uongozi ya Komredi Polepole ambayo haina ada. Jumamosi hii Mwalimu Polepole atatufundisha kuhusu ujamaa na kujitegemea. Hiyo shule kwakweli ni madini matupu yanatolewa. Komredi Polepole adumu.

Kama wiki mbili zilizopita boss wa label ya Koffi Central ambaye ni ndugu wa damu wa Koffi Olomide aitwaye Tutu Robert, aliulizwa na shabiki anadhani ni albamu gani ilikuwa bora zaidi kwa Koffi Olomide na kundi zima la Quartier Latin? Tutu Roba akajibu yeye anaona kiufundi kwa maana ya tungo na mambo ya kimuziki albamu ya V12 ya mwaka 1995 ilikuwa bora zaidi. Hii albamu ndo yenye wimbo Andrada. Ila albamu zilizompa Koffi tuzo nyingi ni Loi na Effrakata. Kwangu mimi komredi Tutu Roba alijibu kisomi sana. Na pia nakubaliana nae kwamba ile albamu ya V12 ilikuwa bora mno. Hadi leo Andrada au Etat Major ya Extra Musica ikipigwa bar huwa inaleta vibe la hatari hadi kwa vijana wa umri mdogo.

Baada ya kusoma majibu ya Tutu Roba nikajikuta naenda mbali na kutafakari zaidi kuhusu muziki. Nikajiuliza kwanini albamu ya V12 iwe bora kuliko zingine zilizotoka miaka zaidi ya 20 baadae? Nikaachana na Koffi na kuanza kurudi kwenye miziki mingine hasa USA. Nikaona kwamba wanamuziki wa leo bado hawajaweza kuvunja rekodi zilizowekwa na wababe wa enzi hizo kwenye utamu wa muziki. Wanamuziki wa leo labda rekodi waliyovunja ni kutengeneza pesa nyingi kuliko kipindi kingine ila kiufundi bado. Kwa mfano kwenye slow jams kuna wakali wa leo ambao wana nyimbo tamu kuwazidi Mariah Carey, Whitney Houston, Boyz II men, na wakali wengine wa zamani. Au kwenye pop kuna mtu aliyeweza kuvunja utamu wa nyimbo za MJ? Tukija kwenye hiphop kuna mambo ya ovyo sana. Tungo nyingi za kishenzi mno. Unaweza google lyrics za vijana wa leo ukaona ushuzi unaoimbwa. Hadi leo hii wimbo wa SEYA ni hitsong ya kwenye sherehe hasa harusi.

Na sio wanamuziki wapya tu hata wakongwe waliokuwepo zamani hadi leo wameshindwa kutoa vitu vikali kama walivyowahi kuvitoa mwanzoni. Je tatizo ni nini? PESA. Tatizo ni pesa. Hii kitu imetuvuruga. Yaani mtu anaimba chochote ili mradi ataingiza pesa. Raia nao hawajali tena maadili wanachotaka ni burudani tu kwa namna yoyote.

Na kwa tulipofikia hakuna kitu tunaweza fanya kubadilisha hii hali zaidi ya kuacha tu watu wajiimbie wanavyoweza cha msingi wanapata riziki. Ni tatizo la dunia nzima sio Tanzania tu.
Tunavipenda vitu na mambo ya nyuma. Na hatuna budi lazima tuvikumbuke na tuvienzi, lakini lazima tusonge mbele no matter what! Ukimleta mtoto wangu ukamuulize muziki anaoukubali sana, atakwambia wa Diamond wa "Nyegezi..."! Babau yako hawezi kumzungumzia Koffi, bali atakwambia Led Wanyika au Moro Jazz. Akienda nje atakwambia Frank Sinatra!
 
Back
Top Bottom