Mvua Afrika Mashariki: Vimbunga pacha kupiga Alhamisi, Ijumaa

Mvua Afrika Mashariki: Vimbunga pacha kupiga Alhamisi, Ijumaa

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Vimbunga viwili vinatarajiwa kutua katika pwani ya Afrika Mashariki usiku wa leo Alhamisi na kesho Ijuamaa, mamlaka za hali ya hewa zinaripoti.

Eneo la Puntland nchini Somalia ndilo linalotarajiwa kuathirika zaidi na tufani hiyo.

Kwa mujibu wa wataalamu wa hali ya hewa, mgandamizo wa hali ya hewa ambao ulikuwa ukitengeneza vimbunga hivyo pacha umesababisha mvua kubwa katika nchi tisa za ukanda wa Afrika Mashariki.

Zaidi ya watu 130 wamepoteza maisha kutokana na mafuriko na maporomoko ya udongo nchini Kenya na Uganda.

Sehemu kubwa ya Somalia ni kame kwa muda mrefu, lakini toka mwezi Septemba, mvua kubwa ya zaidi ya mara mbili ya wastani wa kawaida zimekuwa zikinyesha sehemu kadhaa za nchi hiyo.

Mpaka kufikia mwezi Novemba, zaidi ya watu 270,00 walilazimika kuhama makazi yao nchini humo.

Kwa ujumla mvua zisizo za kawaida zinanyesha katika baadhi ya maeneo ya Kusini mwa Ethiopia, Tanzania, Djibouti, Rwanda, Burundi na Sudani Kusini.

1575538634720.png

Hata hivyo, mvua hizo zinatarajiwa kupungua kasi mara baada ya kutua kwa vimbunga hivyo.

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari juu ya vimbunga hivyo.

Kwa mujibu wa mamlaka hiyo, mgandamizo katika pwani ya Somalia unatarajiwa kuendelea kuwa mbali na pwani ya Tanzania na hautarajiwi kuwa na madhara kwa Tanzania.


"...mgandamizo mdogo wa hewa uliopo kusini magharibi mwa bahari ya Hindi (karibu na kisiwa cha Madagascar) unatarajiwa kuimarika na kuelekea kaskazini mwa kisiwa cha Madagascar, na hivyo unatarajiwa kusababisha ongezeko la mvua pamoja na vipindi vya mvua kubwa hususan katika baadhi ya maeneo ya Pwani ya Kaskazini ya nchi yetu kati ya terehe 5 na 6 Disemba 2019," inaeleza taarifa ya TMA.

"Mamlaka imeendelea kutoa tahadhari ya vipindi vifupi vya mvua kubwa kwa baadhi ya maeneo ya mikoa ya Dar es salaam na Pwani na angalizo la mvua kubwa kwa baadhi ya maeneo ya mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Mara, Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba, Rukwa, Mbeya, Songwe, Iringa, Njombe na Ruvuma."
 
79380329_186415152493651_2105512046656594688_n.jpeg

Mamlaka hiyo imetoa taarifa hiyo kupitia akaunti zake za kijamii”Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inatoa taarifa ya uwezekano wa kutokea kwa vimbunga pacha magharibi mwa Bahari ya Hindi upande wa kaskazini na kusini mwa Ikweta na hivyo kuwa na uwezekano wa kuathiri mifumo ya hali ya hewa nchini.” Imeandika TMA.

Mamlaka hiyo imeongeza kuwa ”Migandamizo hiyo midogo pacha inaelekea kuimarika na kuwa vimbunga katika Pwani ya Somalia (Upande wa Kaskazini mwa Ikweta ) na Kaskazini Mashariki mwa Kisiwa cha Madagascar (Kusini mwa Ikweta).”

”Aidha, mgandamizo mdogo wa hewa uliopo kusini magharibi mwa bahari ya Hindi (karibu na kisiwa cha Madagascar) unatarajiwa kuimarika na kuelekea kaskazini mwa kisiwa cha Madagascar, na hivyo unatarajiwa kusababisha ongezeko la mvua pamoja na vipindi vya mvua kubwa hususan katika baadhi ya maeneo ya Pwani ya Kaskazini ya nchi yetu kati ya terehe 5 na 6 Disemba 2019.”

”Mamlaka imeendelea kutoa tahadhari ya vipindi vifupi vya mvua kubwa kwa baadhi ya maeneo ya mikoa ya Dar es salaam na Pwani na angalizo la mvua kubwa kwa baadhi ya maeneo ya mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Mara, Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba, Rukwa, Mbeya, Songwe, Iringa, Njombe na Ruvuma.”

”Kwa upande mwingine, mgandamizo mdogo wa hewa katika pwani ya Somalia unatarajiwa kuendelea kuwa mbali na pwani ya Tanzania na hautarajiwi kuwa na madhara katika nchi yetu.”

”USHAURI: Wananchi wanashauriwa kuendelea kufuatilia taarifa za utabiri kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania na kuzingatia tahadhari zitakazotolewa na mirejeo yake pamoja na kupata na kuzingatia ushauri na miongozo ya wataalam katika sekta husika ili kupunguza athari zinazoweza kujitokeza.”

”Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania inaendelea kufuatilia hali hiyo katika bahari ya Hindi pamoja na mwenendo wa mifumo ya hali ya hewa kwa ujumla na itatoa taarifa za mrejeo kila itakapobidi.”
 
Back
Top Bottom