Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Hatua hiyo imechukuliwa kufuatia kunyesha kwa mvua kubwa Mkoani Morogoro kuanzia usiku wa kuamkia Januari 13, 2022 hasa katika maeneo ya Kihonda, Mafisa na Soko Kuu la Kingalu.
Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Albert Msando amesema hakuna taarifa ya kifo ila kuna uharibifu wa mali na kuwa shule ameagiza Walimu Wakuu wafunge shule zilizo maeneo hatarishi hadi hali ya usalama iwe nzuri.
Mvua hizo zimesababisha mafuriko, nyumba kubomoka, vitu kusombwa, Watoto kuokolewa baada ya kubebwa na maji, pia kujitokeza kwa foleni ya magari katika Barabara kuu ya Morogoro kwenda Dodoma.
Naye, Kaimu kamanda Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Morogoro, Emmanuel Ochieng amesema wameokoa watu 48 waliokuwa wamezingirwa na maji katika maeneo ya Kata ya Kihonda, kati yao Watoto ni 39 na Watu Wazima 9.
Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Albert Msando amesema hakuna taarifa ya kifo ila kuna uharibifu wa mali na kuwa shule ameagiza Walimu Wakuu wafunge shule zilizo maeneo hatarishi hadi hali ya usalama iwe nzuri.
Mvua hizo zimesababisha mafuriko, nyumba kubomoka, vitu kusombwa, Watoto kuokolewa baada ya kubebwa na maji, pia kujitokeza kwa foleni ya magari katika Barabara kuu ya Morogoro kwenda Dodoma.
Naye, Kaimu kamanda Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Morogoro, Emmanuel Ochieng amesema wameokoa watu 48 waliokuwa wamezingirwa na maji katika maeneo ya Kata ya Kihonda, kati yao Watoto ni 39 na Watu Wazima 9.