Pamoja sana wanajf.
Jana 21/10/2018 maeneo ya wilaya ya Ilemela - Mwanza, kuna mvulana au niseme dogo mmoja hivi alishangaza wengi, na hata wengine kuishia kucheka (nikiwemo Nahuja mie).
Tulikuta foleni kubwa ya magari eneo ambalo hata siku moja halina historia ya msongamano wa magari. Watu wakawa wanajiuliza kuna nini, wengine wakaenda mbali zaidi na kuhisi labda kuna ajali.
Baada ya kushuka kwenye magari tuone kuna nini huko mbele kinachosababisha foleni ndefu, oooooops! tukamshuhudia dogo anagalagala katikati ya barabara hali ambayo imefanya magari yashindwe kuendelea na safari.
Wengine wakasikika wakisema, "amekuwa kichaa". Lakini cha ajabu kukawa na vijana wengine pembeni mwa barabara ambao ni rika moja na yule aliyekuwa anagalagala barabarani walikuwa wanacheka sana,hadi machozi na makamasi yanawatoka.
Tukawauliza, vipi huyu wenzenu amekuwaje? wakatujibu kuwa, "ALIBET NA AMESHINDA KIASI CHA TSHS.1,850,000/=" Kijana mwingine akaongezea "JAMAA ALIBET MKEKA MKUBWA"...
Mfyuuuuuuu, watu tukafoka foka hapo, basi akanyanyuliwa wakamuweka pembeni mwa barabara magari yakaendelea na safari.
Jana 21/10/2018 maeneo ya wilaya ya Ilemela - Mwanza, kuna mvulana au niseme dogo mmoja hivi alishangaza wengi, na hata wengine kuishia kucheka (nikiwemo Nahuja mie).
Tulikuta foleni kubwa ya magari eneo ambalo hata siku moja halina historia ya msongamano wa magari. Watu wakawa wanajiuliza kuna nini, wengine wakaenda mbali zaidi na kuhisi labda kuna ajali.
Baada ya kushuka kwenye magari tuone kuna nini huko mbele kinachosababisha foleni ndefu, oooooops! tukamshuhudia dogo anagalagala katikati ya barabara hali ambayo imefanya magari yashindwe kuendelea na safari.
Wengine wakasikika wakisema, "amekuwa kichaa". Lakini cha ajabu kukawa na vijana wengine pembeni mwa barabara ambao ni rika moja na yule aliyekuwa anagalagala barabarani walikuwa wanacheka sana,hadi machozi na makamasi yanawatoka.
Tukawauliza, vipi huyu wenzenu amekuwaje? wakatujibu kuwa, "ALIBET NA AMESHINDA KIASI CHA TSHS.1,850,000/=" Kijana mwingine akaongezea "JAMAA ALIBET MKEKA MKUBWA"...
Mfyuuuuuuu, watu tukafoka foka hapo, basi akanyanyuliwa wakamuweka pembeni mwa barabara magari yakaendelea na safari.