Mvumo kama wa motor ya wiper kwenye engine

Mvumo kama wa motor ya wiper kwenye engine

Prince Nadheem

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2012
Posts
1,259
Reaction score
1,056
Habari za jumapili ya leo? Natumai wengi mmetulia mkijitathmini namna ya kuanza mikiki mikiki ya wiki mpya mbele yetu.
Nimekuja hapa nikiwa nina shida moja, gari yangu siielewi.
Gari ilianza kupunguza oil, nikaona hapo overhaul yanihusu. Kutokana na sababu za kifedha nikaona niwe naangalia tu oil isiishe kwa kujazia pindi inapotokea imepungua hadi nipate pesa ya overhaul.nilipoipeleka service ya mwisho juzi baada ya km 3000 kutimia niliweka Oil yangu ya Siku zote (BP Premium.).
Siku ya pili kuwasha gari nikaona inatoa moshi mwingi sana wa blue. Ila gari ikitembea kidogo moshi unakata na siku nzima haitoi moshi zaidi ya asubuhi.
Sasa imekuja na ugonjwa mpya tena. Nikiiwasha inawaka vizuri tu halafu baada ya kama dakika mbili unaanza mvumo kama nimewasha mota ya kuoshea kioo cha mbele na wiper (hapo gari inakuwa na milio miwili)ila haiathiri mlio wa gari.
Nimechunguza ila sijapata hata sehemu ya kuihisi kuhusika.
Naombeni mawazo yenu kama hii shida inahusiana na oil pump au chujio limejaa uchafu au ni kitu gani.
Gari kwa sasa nimeipaki hadi ijumaa ijayo ndio nafikiria kuipeleka garage maana nataka pia nisimamie kila hatua, najua nikianza nayo ijumaa basi j2 ijayo narudi na gari.

Please usichangie mzaha wala utani. Kama huna mchango pita kimya kimya tu.

NB: gari ni Toyota Corolla 5A ya 1998, imetembea km 127,000 hadi sasa
 
Mkuu hiyo gari angekua mtu angekua ashabalehe na amekua mtu mzima. One good advice shun it!
 
Mkuu hapo ujitaarishe na overhaul kweli. Oil inaingia kwenye combustion chamber ambapo haitakiwi kufika uko. Piston rings na oil seal zitahisika kwenye hio fitina ya moshi.

Kuhusu huo mlio wa kama wiper motor, hio ni gari gani? Kama ina throttle body ya fly by wire (electronic controlled) inaweza ikawa hio. Huwa inatokea ikiwa kuna vacuum leak.
 
Mkuu hapo ujitaarishe na overhaul kweli. Oil inaingia kwenye combustion chamber ambapo haitakiwi kufika uko. Piston rings na oil seal zitahisika kwenye hio fitina ya moshi.

Kuhusu huo mlio wa kama wiper motor, hio ni gari gani? Kama ina throttle body ya fly by wire (electronic controlled) inaweza ikawa hio. Huwa inatokea ikiwa kuna vacuum leak.
Ni Toyota Corolla 110, engine ya 5A. Ndio najipanga kwa hilo mkuu. Shida yangu ni hako kamlio tu. Nimeona hicho kikombe cha overhaul hakikwepeki kwangu.
Je kama kuna hiyo vaccum leak, tiba yake ni nini sasa??
 
Unahitaji kufanya
Ni Toyota Corolla 110, engine ya 5A. Ndio najipanga kwa hilo mkuu. Shida yangu ni hako kamlio tu. Nimeona hicho kikombe cha overhaul hakikwepeki kwangu.
Je kama kuna hiyo vaccum leak, tiba yake ni nini sasa??
Itakubidi ufanye uchunguzi sehemu zenye gasket na pia utizame pipes za kwenye engine. Tizama intake manifold yako, tafuta Caburator cleaner, pulizia kwenye njia iliowekwa gasket, ukinotice mabadiliko katika silence ya gari basi hapo panatatizo, pia kwenye throttle body gasket pulizia hio dawa, pakitokea mabadiliko na hapo ndio ivo ivo. Tizama pipes zile ndogo ndogo nazo pengine ipo ilotoboka au kukatika kabisa.

Another tip, hakikisha hydraulic fluid imo ya kutosha
 
Back
Top Bottom