Mwabukusi: Vijana wa kitanzania wanajua vifungu vyote vya FIFA ila hawana mpango wa kuijua wala kujua mapungufu ya katiba ya nchi yao

Akina Mwabukusi, Lissu, Mbowe &Co
Wangepata vijana kama wa Kenya, wangekuwa mbali sana .
 
Watu wasilaumiwe wamekata tamaa..fuatilia rafu ccm wanazofanya utaona
Wewe bwana,2008 lowasa fisadi,2015 mabadiliko lowasa lowasa mabadiliko,2017-21 wabunge upinzani wananunuliwa kama malaya, halafu mnataka tuhangaike na siasa!!.. hangaikeni nazo nyinyi mnaokula kupitiazo
 
Mwabukusi ni mkweli tu. Vijana wa bongo Wana uwezo wa kutaja vikosi vizima vya Simba na Yanga lakini ni weupe kwenye vifungu vya katiba.
 
Hahaha Mwabukusu sasa anaanza kupagawa, KATIBA hata tukiijua tutafanya nini ikiwa CCM na majeshi yao bado wanaishi?
 
Huyu nae mbona anaanza kuwa roporopo...
Anafikiri Hilo Ni kosa la Nani!?
 
Ushamba tu , hiyo ni inakuhusu wewe ...Serikali za kitanzania hata ujue hamna cha maana .
 
Katiba ifundishwe mashuleni tangu darasa la nne Hadi form six...
Watawala ndio hawataki watu wajue haki zao ndio maana katiba haifundishwi.
Wanaogopa watawafungua watu macho....
Sote tunajua mtu mweusi kiasili ni mvivu kusoma hivyo njia nzuri ni kuifundisha mashuleni na ikiwezekana kwenye mafundisho ya kipaimara na kwenye madrasa na hata kwenye mafunzo ya Mgambo au hata ya ndoa.
 
Na ndiko huko CCM inaelekeza nguvu zote kwa sasa
 
CCM wanautumia huo udhaifu kutapeli nchi kijinga na wizi mwingine
 
Mnawasingizia tu vijana wa Tanzania, huku msingi wa hoja mkiukwepa. Na napenda kukufahamisha kuwa sio vijana tu na hata, watanzania wengi hawapendi kujihusisha na siasa kwa kuwa siasa zimevamiwa, na waroho wa madaraka.

Mfano vyama vingi vya siasa ni vya kifamilia tu na viongoz wa vyama ni wa, miaka yote.cdm Mbowe ni mwenyekiti wa kudumu, CUF Lipumba ni wa kudumu, ACT pia kipo kimchongo.

Aidha, Mbowe,ukiwa mbunge anakukata one million kwenye salary,wizi mkubwa. Mbowe,na genge lake walituhaminisha kuwa Lowassa ni fisadi,halafu akawa, mgombea, wao wa urais. Watu wengi wenye akili na busara kipindi hicho waliondoka cdm na hawataki kusikia huo ujinga wa siasa tena. Wabunge kama Sugu wapo kunufaisha matumbo kwa kugombea madaraka. Sugu anatuonyesha hotel yake badala atuonyeshe maendeleo ya wananchi aliyofanya. Kwa ujumla wabongo wanameamua kutafuta sehemu ya kupunguza stress kuliko huo ujinga wa siasa.
Kwa hiyo ndugu kawambie hao waliokutuma kuwa wabongo sio wajinga na hawapendi stress.
 
tatizo mfumo wetu ni kandamizi sana haswa linapokuja swala la kuhoji haki za msingi kwa raia au kumkosoa kiongozi kwa hoja unapotezwa. vijana tusilaumiwe kwa hili, wengi wetu tushajikatia tamaa na mambo ya uongozi wa kimabavu wa hii nchi tunaona bora tudili na mpira kubet huenda labda milango ya mafanikio ikafungukia huko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…