Mwadui 0-1 Simba | Uwanja wa Kambarage | Vodacom Premier League

Mwadui 0-1 Simba | Uwanja wa Kambarage | Vodacom Premier League

Kuna viwanja huwa vinamsumbua Mnyama kupata goli nyingi.
Ila yote kwa yote points tatu ndo kitu muhimu sana.
 
Ntashangaa Morrison asipochukuliwa hatua kwa kitendo cha uzalilishaji kwa mshika kibendera
Linesman amejichanganya mwenyewe Tu, kimichezo wachezaji waga wanapigana makalio mara kibao Tu kama pongezi au pale mchezaji anapofanyiwa sub

Me naamini Morrison alikuwa anamwambia linesman asogee Kwa kumpiga tako ili apige kona, bahati mbaya jamaa akatafsiri tofauti
 
Hongera Simba kwa ushindi lakini kuna mambo benchi la ufundi wasipoyafanyia kazi kwa umakini yatailetea shida Simba hapo baadaye.
1. Simba leo wamewadharau sana Mwadui tokea mwanzoni mwa mchezo wakajisahau kuwa mpira unadunda. Walikuwa "slow" sana katika kipindi cha kwanza kiasi walikuwa wanawapa muda Mwadui wachezaji tisa kujipanga nyuma ya mpira hivyo ikawa kazi ngumu kuipenya ngome yao. Viungo wa Simba Nyoni na Mkude walitakiwa kuwa wanapeleka mipira mbele kwa haraka kabla Mwadui hawajipanga vizuri.

2. Chikwende bado hajaingia vizuri kwenye mfumo wa Simba sioni sababu ya kila wakati benchi la ufundi kumtumia wakati una Dilunga, Miraji na Morison ambao wamezoea viwanja vibovu vya mikoani. Chikwende ni wa kupewa dakika kumi za mwisho tena wakati Simba imeshashinda goli zaidi ya tatu mpaka atakapoingia vizuri kwenye mfumo wa Simba. Na hili sio ajabu na yeye sio wa kwanza kwani hata Morison, Bwalya na Mugalu iliwachukua muda kidogo kuendana na mfumo wa Simba.

3. Uwanja ulikuwa mbovu kwa sababu nyasi zake hazijapunguzwa vizuri kwa hiyo mpira ulikuwa hautembei vizuri lakini maajabu Simba walitaka bado wacheze kama wapo kwa Mkapa. Kuna mpira Onyago alirudisha kwa Manula haukufika vizuri na mshambuliaji wa Mwadui alizubaa kidogo. Hiyo ilipaswa iwe kengele ya hatari kwa Simba kuacha pasi fupi fupi kule nyuma badala yake wahakikishe wanacheza mipira mirefu muda wote kuelekea kwenye lango la Mwadui.

4. Benchi la ufundi la Simba lilijilipua kwa kumuingiza Boko acheze na Kagere nilitegemea Simba wangetumia mipira mirefu kwani Boko ni mzuri sana kwenye mipira ya juu lakini ajabu Boko na Kagere wakawa watazamaji hasa baada ya goli kupatikana. Baada ya Simba kupata goli moja ndio mizaha ikazidi utafikiri Simba walikuwa wanaongoza goli tano wanasahau kuwa goli moja linaweza kurudi hata ikibaki sekunde moja. Nahisi Simba wamesahu walivyokoswa koswa dakika za mwisho kama sikosei na Dodoma Jiji.

5. Uongozi ulikumbushe benchi la ufundi kuwa kwenye mechi za mikoani kinachohitajika ni ushindi tu wala sio mbwembwe za mpira biriani hilo lisubiri kwa Mkapa. Kwa sasa kinachohitajika sana ni pointi tisa za kanda ya ziwa wala sio mbwembwe za mpira biriani. Na kwa hili Chama, Bwalya, Erasto na Mkude wajulishwe mapema waache mizaha yao ya vipasi vifupi fupi na kupoozesha mashambulizi. Hivi walikuwa hawaoni namna wenzao Wawa na Morison walivyokuwa äggresive" wanalazimisha kwenda kwenye goli la Mwadui?
 
Pamoja na ushindi wa leo sijafurahia jinsi Simba wanavyocheza Chama na Shabalala wanakaa sana na mpira, Wawa apunguze kupiga pasi ndefu kwani nyingi zinapotea. Goli moja sio la kuliamino inaweza kutokea ndondokela.likarudi tukashindwa kuongeza hivyo Wimba wasiridhike na goli moja
 
Pamoja na ushindi wa leo sijafurahia jinsi Simba wanavyocheza Chama na Shabalala wanakaa sana na mpira, Wawa apunguze kupiga pasi ndefu kwani nyingi zinapotea. Goli moja sio la kuliamino inaweza kutokea ndondokela.likarudi tukashindwa kuongeza hivyo Wimba wasiridhike na goli moja
Chama [emoji106]
Shabalala [emoji106]
Sultan Wawa [emoji106]
 
Pamoja na ushindi wa leo sijafurahia jinsi Simba wanavyocheza Chama na Shabalala wanakaa sana na mpira, Wawa apunguze kupiga pasi ndefu kwani nyingi zinapotea. Goli moja sio la kuliamino inaweza kutokea ndondokela.likarudi tukashindwa kuongeza hivyo Wimba wasiridhike na goli moja
Asante Mkuu,
Shabalala tena aambiwe mapema aache hiyo tabia
Bocco na Kagere wameshatengeneza space wananyoosha mikono waletewe mpira yeye anapiga back pass
Hata nyoni
 
Hongera Simba kwa ushindi lakini kuna mambo benchi la ufundi wasipoyafanyia kazi kwa umakini yatailetea shida Simba hapo baadaye.
1. Simba leo wamewadharau sana Mwadui tokea mwanzoni mwa mchezo wakajisahau kuwa mpira unadunda. Walikuwa "slow" sana katika kipindi cha kwanza kiasi walikuwa wanawapa muda Mwadui wachezaji tisa kujipanga nyuma ya mpira hivyo ikawa kazi ngumu kuipenya ngome yao. Viungo wa Simba Nyoni na Mkude walitakiwa kuwa wanapeleka mipira mbele kwa haraka kabla Mwadui hawajipanga vizuri.
2. Chikwende bado hajaingia vizuri kwenye mfumo wa Simba sioni sababu ya kila wakati benchi la ufundi kumtumia wakati una Dilunga, Miraji na Morison ambao wamezoea viwanja vibovu vya mikoani. Chikwende ni wa kupewa dakika kumi za mwisho tena wakati Simba imeshashinda goli zaidi ya tatu mpaka atakapoingia vizuri kwenye mfumo wa Simba. Na hili sio ajabu na yeye sio wa kwanza kwani hata Morison, Bwalya na Mugalu iliwachukua muda kidogo kuendana na mfumo wa Simba.
3. Uwanja ulikuwa mbovu kwa sababu nyasi zake hazijapunguzwa vizuri kwa hiyo mpira ulikuwa hautembei vizuri lakini maajabu Simba walitaka bado wacheze kama wapo kwa Mkapa. Kuna mpira Onyago alirudisha kwa Manula haukufika vizuri na mshambuliaji wa Mwadui alizubaa kidogo. Hiyo ilipaswa iwe kengele ya hatari kwa Simba kuacha pasi fupi fupi kule nyuma badala yake wahakikishe wanacheza mipira mirefu muda wote kuelekea kwenye lango la Mwadui.
4. Benchi la ufundi la Simba lilijilipua kwa kumuingiza Boko acheze na Kagere nilitegemea Simba wangetumia mipira mirefu kwani Boko ni mzuri sana kwenye mipira ya juu lakini ajabu Boko na Kagere wakawa watazamaji hasa baada ya goli kupatikana. Baada ya Simba kupata goli moja ndio mizaha ikazidi utafikiri Simba walikuwa wanaongoza goli tano wanasahau kuwa goli moja linaweza kurudi hata ikibaki sekunde moja. Nahisi Simba wamesahu walivyokoswa koswa dakika za mwisho kama sikosei na Dodoma Jiji.
5. Uongozi ulikumbushe benchi la ufundi kuwa kwenye mechi za mikoani kinachohitajika ni ushindi tu wala sio mbwembwe za mpira biriani hilo lisubiri kwa Mkapa. Kwa sasa kinachohitajika sana ni pointi tisa za kanda ya ziwa wala sio mbwembwe za mpira biriani. Na kwa hili Chama, Bwalya, Erasto na Mkude wajulishwe mapema waache mizaha yao ya vipasi vifupi fupi na kupoozesha mashambulizi. Hivi walikuwa hawaoni namna wenzao Wawa na Morison walivyokuwa äggresive" wanalazimisha kwenda kwenye goli la Mwadui?
Upo sahihi kabisa...
Na leo dharau zingewacost
 
Back
Top Bottom