Duuh, jamaa ana uchungu,katema cheche hatari. Ana hasira na yuko tayari kwa lolote....
Katibu mwenezi BAVICHA Taifa Twaha Mwaipaya amesema hakuna Jeshi la Polisi litaloweza kutuzuia vijana tukiamua kutafuta haki yetu barabarani. Ameyasema haya alipokuwa akichangia hoja katika kongamano la TCD, DSM leo Alhamisi tarehe 19/9/2024.
"Vijana tunatekwa tunatembea kwenye nchi yetu ya Tanzania nchi ambayo tumerithishwa na babu zetu. Hatuna amani kwa sababu tunapingana maoni na watu wengine. Hivi kuna thamani ya kuishi kujifungia ndani ety kusema tuna amani kuliko kulinda uhai wetu tulio nao"Mwaipaya
Tuache watu watazame na wasikilize kwa makini ktk video clip hii kisha tujadili.