Mwaka 2025 Tuazimie Kufanya Mazoezi

Mwaka 2025 Tuazimie Kufanya Mazoezi

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Screenshot_20241231_184839_Google.jpg



Rafiki yetu 2024 ndio anatuaga leo anakwenda zake,tulikuwa nae pamoja na changamoto za hapa pale lkn baadhi yetu hawakupata bahati ya kuwa hai mpaka leo na wengine masaa haya machache yaliyobakia huenda tukatoboa au tusitoboe hakika uhai ni miliki ya Allah

Mwishoni mwa 2023 nilihitimisha na uzi wa TUAZIMIE KUACHA KUACHA KUANGALIA FILAMU ZA NGONO



Hope baadhi yetu tulikula kiapo hicho na tukakomaa nacho hatuna budi kujipigia makofi hakika kongole kwetu sote tumeushinda huo uraibu na kuuponya ubongo wetu na kuwa mbali na tabia ya kupanda mnazi kwa mkono mmoja,maana porn mwenzake ni masterbation

Mwaka huu ambao tutaingia hivi punde inshallah tuazimie kufanya mazoezi kwa ajili ya afya zetu,hakika tutaepuka magonjwa yasiyo ambukiza kama presha,kisukari na mengineyo ambayo yanapatikana kutokana na mtindo wetu wa maisha

Screenshot_20241231_185000_Google.jpg


Lakini tukijikita zaidi kwa kufanya mazoezi ya kutembea kama hatua 10,000 kama anavyosema Doktori Janabi naamini kabisa tutajenga afya zetu,kuna jogging na mazoezi mengine ya viungo mbali mbali

Kwasisi wazee ambao tupo kwenye miaka 40 hasa sisi wanaume itatusaidia pia kuepukana na matatizo ya tezi dume,wataalamu wanasema kufanya mazoezi kunasaidia sana kuepukana na matatizo haya

Pasina kusahau afya yetu ya uzazi,wanaume mazoezi kwetu ni muhimu kuimarisha mzungumko wa damu na matokeo yake tunapokuwa kwenye mambo yetu ya sita kwa sita tusizingue,amini nakwambia hakuna mwanaume mwenye matatizo ya nguvu za kiume ni kubadilisha mtindo wa maisha,acha pombe,kula vizur na piga tizi sana utakuwa vizur sana,mazoezi ya kegel usikose yanasaidia chuma kusimama imara na kwenda mbio ndefu

Screenshot_20241231_185152_Google.jpg


Kwa ujumla tujenge utamaduni wa kufanya mazoezi ni bora sana kwa afya zetu,usifikirie utaanza lini bali anza sasa,anza hata kwa hatua 3000 za kutembea au anza kwa kukimbia mita mia tu,hiyo itakupa hamasa ya kufanya zaidi na zaidi

Tambua mazoezi ni kwa ubora wa afya yako mwenyewe

Happy New Year

Ni hayo tu!
 
Ebu tupe ratiba na utaratibu wako wa tz mkuu.
Mimi huwa nakimbia walau mara nne kwa wiki, na ni mara moja tu kwa maana sio asubuhi na jioni,kama asubuhi ni asubuhi na kama jioni ni jioni

Baada ya jogging huwa napiga push up,sukwati na mazoezi mengine ya viungo,kila kitu kina uraibu wake,ukifanya kwa kipindi kirefu hakika hautataka kumiss mazoezi,ingawa kuna baadhi ya siku unaweza kosa kufanya lkn utapambana wakati mwingine ufanye

Kikubwa ni kujitahidi kufall in love na mazoezi baada ya hapo ni kama kumsukuma mlevi
 
Muhimu sana. Acheni kutembelea tako jamani. 40 min walking kwa siku tusha sana. Unasikia mwili upo vizuri.
Baadae utaongeza mpaka unafika 2hrs walking
 
tuwakumbushe wadada wa "vitako mchomoko" mnatutia majaribuni sana na vitaiti vyenu va mazoezi
 
Back
Top Bottom