Mwaka wa kumi huu au zaidi umeajiriwa (unatumwa tumwa tu); je, ni kitu gani kinakufanya usijiajiri?

Mwaka wa kumi huu au zaidi umeajiriwa (unatumwa tumwa tu); je, ni kitu gani kinakufanya usijiajiri?

Tatizo vijana ukweli hatutaki kuusikia.
Wewe ni mzee wa miaka 60 tena kada wa CCM , Tabia yenu kubwa mnaendeleza mitazamo yenu ya miaka sabini katika Dunia ambayo imechukua uelekeo.mwingine , huwa hamtaki kukubali ukwelii mnasimamia msimamo wa miaka ile.
 
Nani kakwambia nimeajiriwa Mkuu? Au umejiamulia kuja na conclusion yako?.

Unakosea sana unaposema waliojiajiri ndio wagunduzi, huu ni ujinga wa hali ya juu Mkuu.

Mtu yoyote anayefanyakazi kwa bidii anayetaka maendeleo haijalishi ameajiriwa au kajiajiri anaweza kuwa mgunduzi.

Hivi unajua utofauti wa kuajiriwa sekta binafsi na serikalini ni ndogo sana na ambayo haiathiri ugunduzi wa mtu.

Tatizo sisi vijana wa kitanzania ni wavivu sana na walalamishi mno.
Aliyeajiriwa anafanya kazi(anafungwa) kwa misingi na kanuni zilizoainishwa na mamlaka husika; hawezi kufanya ubunifu wake nje ya miongozo iliyowekwa.
 
Wengine wanafikiri kufanya biashara unahitaji akili ya shule kama degrees au uwe na mtaji mkubwa sana wa kuanzia biashara

Babu yangu hakusoma kabisa ila kwenye kurudisha chenji na kuendeleza mtaji alikuwa makini sana mpaka kumfundisha na mwanae (baba)
Leo biashara zinaendelezwa na wajukuu
Kuna mzee alikuwa anahojiwa biashara zao zilianza 1930s na 40s na sasa warithi wanakuja ila waendeleze View attachment 2877360
Inawezekana sisi wengine tunashindwa kutokana na mazingira tuliozaliwa au uwezo wetu wa kufikiri ni mdogo, au labda tupo bado kwenye uendelevu wa 'evolution stage'
 
Shida ya mbongo inakuwa hapa akisikia neno kujiajiri anafikiria ujasiriamali.

Wewe ni mwanasheria umefanya kazi ya kuajiriwa umekusanya pesa ya kutosha kwanini usiache ajira na kuanzisha Law firm yako, wewe Ni daktari ushajijengea jina watu wakakuamini kwanini usifungua kliniki yako na mdogo mdogo ikawa hospitali ukaajiri watu wengi , Wewe ni mhasibu na CPA yako kuliko kuendelea kuajiriwa kwanini usitoke kwenye comfrot zone na kuanzisha Auditing firm yako.
Kama raia tukiwa na mawazo haya nchi itapiga hatua, maana faida zake ni nyingi kwanza utaacha nafasi ya watu wengine kuajiriwa na wewe pia utaajiri , kuliko kusubiria kufa au kustaafu ili wengine wapate ajira.

Nchi ya Marekani yenye idadi ya watu zaidi ya milioni 150 ni asilimia 18 tu ya idadi yote ya watu wameajiriwa serikalini na asilimia zote zilizobaki ni sekta binafsi na wengine kujiajiri.
Maana yake ni nini? , hata taifa kibwa kama Marekani halina uwezo wa kuajiri raia wake wote sasa Sembuse Tanzania ambayo ndio kwanza hata uchumi wa kati hatujafikia.

Ukishajiajiri na ukatoboa maana yake unaingiza biashara yako au Kampuni yako katika orodha ya sekta binafsi.

Wenzetu wamepiga hatua kwasasabu mitazamo yao ishabadilika muda mrefu lakini sisi ndio kwanza tunalumbana hapa kitu ambacho kipo wazi.
Wenye akili kubwa watakuwa wamekuelewa
 
Inawezekana sisi wengine tunashindwa kutokana na mazingira tuliozaliwa au uwezo wetu wa kufikiri ni mdogo, au labda tupo bado kwenye uendelevu wa 'evolution stage'
Yaani kuna wakati huwa nawaza na kujisemesha mwenyewe
Hivi kwanini kusiwe na shule ya nidhamu tu ya kuwafundisha watoto na watu wazima namna ya kuishi kama binadamu?
Shule badala ya kutafuta the finest eti wamechujwa na kwenda private au international naona wanahitaji kuwa na shule za kuwafundisha kutokuwa waongo, waizi, matapeli, wala rushwa na uchafu mwingine wote

Yaani kweli leo wanafunzi wanaofikiriwa kuwa wafanyakazi au viongozi au kuwa na taasisi leo hawajui hata namna ya kutumia Vyooo UDOM?
Sasa hao na wanyama wana tofauti gani?

Hao ndio wanaokuja kuwa wala rushwa na matusi kibao ukimwendea ofisini maana anatoka chuo hajui maana ya nidhamu kabisa bali kakariri tu vitabu

Bungeni kuna mbunge aliibiwa laptop au simu sikumbuki na hao ndio viongozi
Yaani sio kibaka aliingia bungeni laa bali wao ndio vibaka
Unategemea nini hapo mkuu
Ntakuja fungua shule ya nidhamu tu na maadili
Kwani lazima tuige wazungu wakati hatuwafikii
Wao wamepigana na Uongo, Rushwa na hata kupiga watoto
Sisi tuanze tu ya kwetu ila tuna safari ndefu sana
 
Unahisi ni nini kichowafanya watu wasijiajiri?
Well..kwa sasa (nyakati hizi)

-Kujiajiri kuna alot of risk ambazo zinahitaji utayari na uthubutu, kwa vijana wengi wanaotoka masomoni inahitaji courage..(kuajiajiri yaweza kua ujasiriamali., kufungua ofisi za consultancy etc).

-Upatikanaji wa mitaji si rafiki sana ..maana banks ili ukopesheke lazima uwe na securities na kama unavyojua uchumi wetu una fluctuate....

- Uwepo wa longolongo nyingi kwenye kupata vibali husika..ina discourage esp kwa kujiajiri sector binafsi..sina maana kua hatuna taratibu na mifumo ila ipo mizuri lakini baadhi ya watu wanasimamia ndivyo sivyo.

- Mindset/mtazamo ni kama inaonekana ukiajiriwa umeula hivyo kwa kiasi flani inasababisha hasa kwa vijana kuchukulia kuajiriwa ni salama zaidi..ofcourse risk ni ndogo.

- mifumo yetu ya elimu na mitaala haichochei ubunifu na mtu kujituma...kama unafuatilia ni kama tunaishi kwa kuangalia "motivation speakers"

Tufanye nini:
-Elimu iboreshwe [ya ufundi...vyuo..etc
- Mazingira ya kujiajiri
-uthubutu
- Tupunguze ukiritimba na tartibu nyingi kwenye secta binafsi

-Sio kila kitu tuingize siasa
 
[emoji23][emoji2] Vijana mmekosa ajira mnaishia kujifariji kujiita wafanya biashara...
Nyie ni machinga tu mnao bangaiza maisha mpate pesa ya kula na kulipa kodi vyumba vya uani...
Watu wameajiriwa wanakula mishahara take home sio chini ya Million 1 na ana uhakika wa kupata Allowances kila wiki...
Wakati wew uliyekaa hapo umefungua kibanda cha kuuza juice urembo chupi na biscuits faida kwa mwezi haifiki Laki 1 [emoji23][emoji23]
VIJANA MSIDANGANYIKE HII TZ MTU ANAYEFAIDI MAISHA BILA STRESS NI MUAJIRIWA TENA WA SERIKALINI...
Anaenda kazin siku 5 kwa wiki, ana uhakika wa mshahara umeme uwake ukatike, jua au mvua inyeshe, hana hofu ya kufukuzwa kazi, anaenda likizo kila mwaka, akiumwa anapewa ruhusa bila kipingamizi, akifiwa hata na jirani haendi kazin...
Hivi hamjiulizi kwanini viongoz wengi wana ng'ang'ania madarakani..?[emoji23][emoji2]
Nasikia chadema wameandaa maandamano [emoji23][emoji2] watakao enda ni nyie vijana mnajiita wafanya biashara kwasabab hamna uhakika wa kula na kuishi kesho...
UKWELI MCHUNGU [emoji23][emoji2][emoji120]
Japo ni UKWELI MCHUNGU juu ya kula kwenu maisha wafanyakazi wa serikali ukilinganisha na kundi kubwa la vijana waliojiajiri.

Hili la ninyi kula maisha ndo linaloleta changamoto mbalimbali ktk jamii, mfano kwa sababu mna uhakika wa mshahara kila mwezi, basi wengi wenu ni wavivu, wachache sana miongoni mwenu ambao ni wachapakazi na wabunifu, wengi wenu ni bora siku zinakwenda.

Wale wachache wabunifu na wachapakazi utakuta wameajiriwa vilevile wamejiajiri hao ndo sasa huumiza vichwa vyao ili kututatulia changamoto ktk jamii zetu.

Kupitia uchapakazi wao na ubunifu wao wanatengeneza fursa za kazi kwa vijana walioko mtaani, huko makazini wanatoa huduma nzuri kwa raia nk.

Ila wale ambao wanasema serikalini ndo sehemu ya kula maisha wengi ni mzigo katika jamii kwa sababu tija ya ni ndogo sana ktk ustawi wa jamii.

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom