Shadida Salum
Journalist at JamiiForums
- Sep 11, 2020
- 69
- 105
Klabu ya Yanga imesema kuwa haitendewi haki na vyombo vinavyosimamia mpira wa miguu kwa maana ya Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF),Bodi ya ligi, kamati ya ya masaa 72 na kamati ya waamuzi.
Hayo yamesemwa na Makamu Mwenyekiti wa Yanga Fredrick Mwakalebela alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari hii leo.
Katika mazungumzo yake Mwakalebela, ametaja mechi yao dhidi ya Mbeya City jinsi ambavyo waamuzi walikuwa wakikinzana katika kufanya maamuzi huku akiataja penati ambayo ilikataliwa na mwamuzi .
Pia akaongeza katika mchezo wao dhidi ya Kagera sugar penati nyingine ilikataliwa baada ya mchezaji wao kuangushwa ndani ya box huku mchezaji wa Kagera sugar akiokoa kwa mkono.
Aidha wamehoji kuwa je waendelee kuwepo kuwepo kwenye ligi au wajitotoe na kama kuna bingwa tayari ameandaliwa basi apewe ubingwa huo.
Vilevile ameviomba vyombo vinavyohusika kuingilia kati swala hilo.