Mwakinyo ashikiliwa na Polisi Tanga, akituhumiwa kum-shambulia mtu

Mwakinyo ashikiliwa na Polisi Tanga, akituhumiwa kum-shambulia mtu

Bondia wa ngumi za kulipwa nchini Tanzania, Hassan Mwakinyo anashikiliwa na jeshi la Polisi mkoa wa Tanga, akituhumiwa kumshambulia mtu anayedaiwa kuingia katika eneo lake bila ridhaa yake.

Mwakinyo anashikiliwa na jeshi hilo tangu jana alhamisi katika kituo cha polisi Chumbageni kutokana na sakata hilo huku mtu aliyemshambulia akiendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa ya Bombo iliyopo Tanga.

Chanzo cha kuaminika kimelieleza gazeti la Mwananchi kuwa sababu kubwa ya bondia huyo kushikiliwa na jeshi hilo ni kutokana madai ya kumshambulia mtu huyo na kumsababishia majeraha makubwa mwilini.

Mwananchi limemtafuta kaimu kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga, ACP Maket Msangi amekiri pia wanamshikilia bondia huyo.

"Sisi tunamshikilia Hassan Mwakinyo hatumshikilii bondia.
Hakuna shia ila ana tuhuma za kumshambulia mtu ambaye inasemekana alipita katika maeneo ya nyumbani kwake na kujaribu kuingia kwa namna ya mazingira ambayo inadaiwa ni kwa nia ya kutenda kosa kwa hiyo akamkamata," amesema Msangi.

"Wakati tunapewa taarifa alikua amemkamata Polisi tulienda kwaajili ya kumchukua mtuhumiwa lakini alikua kidogo ana majeraha tukampeleka akapate huduma ya kwanza Bombo kwa hivyo tunamshikilia kutokana na kumkuta mtuhumiwa kidogo ana majeraha, Tunaendelea kumhoji Mwakinyo kwanini mpaka akajeruhiwa hivyo.

"Hivyo elewa kwamba tunamshikilia kwasababu hiyo tutafikisha suala hilo ofisi ya mashitaka kwaajili ya kutafsiri sheria na kama kuna tatizo ushahidi unathibitisha kosa basi hatua nyingine stahiki zitachukuliwa," alisema Msangi.
Sasa waizi wakija majumbani kwetu tusiwafanye chochote mpaka Polisi waje?
 
Uwezo wako wa kufikiri ni Mdogo sana.

Kwa maelezo ya Kamanda, kwa lugha nyepesi huyo aliepigwa ni intruder, ambaye Intruder siku zote Nia yake hua ovu. Kwa sababu katika akili yako ya kawaida unawezaje kupita ama kuingia kwenye makazi ya mtu bila ridhaa yake, na zaidi hakujui.
Kama alikuwa na matatizo ya akili je?
 
Kama aliingia kwa lengo la kwenda kuiba mwacheni Mwakinyo bila masharti yeyote...Wezi wanarudisha nyuma maendeleo...Na alimuonea huruma ilibidi mje kumchukua huyo mwizi hajitambui.
 
Yule jamaa alivyo pigwa kukatwa na kisu Hadi kufunguliwa mbwa mwakinyo ni mnyama sizani kama ata ana mke
 
Mtu ameingia nyumbani kwako bila ruhusa (Trespass) kwa lengo usilolijua aidha kukudhuru, kukuibia, kukubambikizia madawa, n.k.

Sioni shida ya kumshushia kichapo, labda kama ni mtoto mdogo au mwanamke
Kwamba mwanamke hawezi kua adui?

Sent from my Infinix X669 using JamiiForums mobile app
 
Hakuna mtu mwenye ruhusa ya kutoa hukumu ya kosa lolote isipokuwa mahakama.
Kwahiyo mwakinyo nae amejichukulia Sheria mkononi Hivyo nae ni mtuhumiwa wa uharifu Tu kama wahalifu wengine.
Hio hai-apply kwenye issue ya tresspassing.. mbaya zaidi usiku kwenye eneo lenye fence..
Mtu anaruhusiwa kulinda mali na mwili wake kivyovyote vile maana hajui ulikuja kuiba nazi tu au kuna mengine..
Sema hata hivyo jamaa inaonekana ana nature ukatili tu, kulikuwa hamna haja ya kumuumiza sana baada ya kumdhibiti na kujiridhisha hana silaha..
Ila kisheria naona kama hana kesi.
 
Uwezo wako wa kufikiri ni Mdogo sana.

Kwa maelezo ya Kamanda, kwa lugha nyepesi huyo aliepigwa ni intruder, ambaye Intruder siku zote Nia yake hua ovu. Kwa sababu katika akili yako ya kawaida unawezaje kupita ama kuingia kwenye makazi ya mtu bila ridhaa yake, na zaidi hakujui.
Don't kill the comedy, huyu mwamba hayupo serious, ameamua kuchekesha kidogo...ngumi kidogo, comedy kidogo...life is too short..
 
Alishindwa kuruka ukuta vizuri akaanguka

Hivi kweli mwamba alikosa sehemu za kuvamia mpaka akaenda kwa mwakinyo
Yan leo uende kuruka ukuta wa yule Myukrein Oleksandr Usyk wakati unajua wazi kabisa hata Tyson furry angekuwa mwizi asingeenda kuruka ukute wa bwana Usyk....watu bwana Yan on his Prime Mike Iron Tyson unaenda kufanya ukibaka nyumbani kwake wakati unaona mijitu futi 7 inadondoka kama milingoti mafinga hapo, daaah. Leo ituchanganye nyumbani kwa Francis Nganou sijui hata kuandika jina lake la pili huwez kutoka salama
 
Yan leo uende kuruka ukuta wa yule Myukrein Oleksandr Usyk wakati unajua wazi kabisa hata Tyson furry angekuwa mwizi asingeenda kuruka ukute wa bwana Usyk....watu bwana Yan on his Prime Mike Iron Tyson unaenda kufanya ukibaka nyumbani kwake wakati unaona mijitu futi 7 inadondoka kama milingoti mafinga hapo, daaah. Leo ituchanganye nyumbani kwa Francis Nganou sijui hata kuandika jina lake la pili huwez kutoka salama
SI unajiona punching bag
 
Nimewasikiliza majirani wa Mwakinyo wakisema kuwa anazingua muda mrefu tu.Mwakinyo kalewa sifa,anajiona yeye ndiyo yeye,hana heshima na adabu kwa majirani zake,inasemekana kawashika viongozi wengi wa mtaa na polisi.Mwakinyo inabidi apewe fundisho pimbi yule ili asirudie upumbavu wake.Ikishindikana aje mtu na vinyama vya mshikaki avitie sumu aanze na mbwa wake,mpuuzi sana yule na roho yake mbaya na yawezekana si mtu wa tanga,watu wa tanga hawana roho kama yake,inawezekana ana asili ya rwanda pimbi yule.
 
Nimewasikiliza majirani wa Mwakinyo wakisema kuwa anazingua muda mrefu tu.Mwakinyo kalewa sifa,anajiona yeye ndiyo yeye,hana heshima na adabu kwa majirani zake,inasemekana kawashika viongozi wengi wa mtaa na polisi.Mwakinyo inabidi apewe fundisho pimbi yule ili asirudie upumbavu wake.Ikishindikana aje mtu na vinyama vya mshikaki avitie sumu aanze na mbwa wake,mpuuzi sana yule na roho yake mbaya na yawezekana si mtu wa tanga,watu wa tanga hawana roho kama yake,inawezekana ana asili ya rwanda pimbi yule.
Vijana wa Tanga kazi hamtaki kufanya mnachotaka ni kuiba au kupigwa pipe mpate hela ya kustarehe. Mwanknyo kapiga mwizi sisi huku tulipo tunaua kabisa. Yani nikukute ndani kwangu saa 10 usiku alafu utoke unapumua ushukuru Mungu
 
Vijana wa Tanga kazi hamtaki kufanya mnachotaka ni kuiba au kupigwa pipe mpate hela ya kustarehe. Mwanknyo kapiga mwizi sisi huku tulipo tunaua kabisa. Yani nikukute ndani kwangu saa 10 usiku alafu utoke unapumua ushukuru Mungu
Acha matusi we kipapa unafikiri kila mtu yuko bongo
 
Mtu ameingia nyumbani kwako bila ruhusa (Trespass) kwa lengo usilolijua aidha kukudhuru, kukuibia, kukubambikizia madawa, n.k.

Sioni shida ya kumshushia kichapo, labda kama ni mtoto mdogo au mwanamke
Nyie ndio hata hamjui sheria za nchi kiasi kwamba inawagharimu
 
Back
Top Bottom