Mwakyembe awatega wabunge CHADEMA, awaambia wakitaka ukweli warudishe hoja ya Richmond Bungeni

Mwakyembe awatega wabunge CHADEMA, awaambia wakitaka ukweli warudishe hoja ya Richmond Bungeni

Katika suala lolote lililo na utata LAZIMA LAZIMA mtu ahojiwe. Hata kesi Mahakamani bila ushahidi ni upungufu mkubwa sana. Suala la Richmond kulikuwa na upungufu mkubwa sana kwa kutomhoji Mhe. Lowassa. Yeye anaweza kuamini kuwa ALIONEWA.
 
Yaani Mwakyembe ana Hasira Na Lowasa sijui walikosana nini! Si umpeleke tu Mahakama uliyosaidia kuasisi ya Mafisadi?
 
Yaani Mwakyembe ana Hasira Na Lowasa sijui walikosana nini! Si umpeleke tu Mahakama uliyosaidia kuasisi ya Mafisadi?
HATHUBUTU ,
Mahakamani sio pa mchezo. Isitoshe hana kesi ya kumshtaki nayo Lowassa, angekua nayo asingeweweseka hivyo. Kama utakumbuka wakati wa uchaguzi Lowasa alisema wapeleke kesi mahakamani , hapo Mwakyembe alikuwa hajafufuka!?
 
Mwakyembe amefeli sana. Nilitegemea mwanasheria kama yeye lile swala alipeleke kwenye ile mahakama yao iliyokosa watuhimwa maarufu kama MAHAKAMA YA MAFISADI.

Hizi porojo za kunyoana kwa chupa sijui zimetoka wapi!

Mwakyembe is a hopeless fellow..! Ndio maana mwajiri wake akamdharau na kumpa wizara isiyohitaji msomi.
 
Hadi sasa ni miezi kadhaa imepita tangu mahakama ya mafisadi iundwe. Waziri/mbunge/aliyekuwa Waziri wa Sheria anakurupuka leo na kuropoka kuwa yupo tayari kumshughulikia MTU aliyejiuzulu kuruhusu HAKI ITENDEKE miaka 8 iliyopita.
Huyu ni Profesa msomi kweli!?
Ni nzima wa akili!?

Sent from my Vodafone 875 using JamiiForums mobile app
Rudisheni hoja ili tujue mbivu na mbichi
 
You are an imbecile. Mnaolalamika kuwa alionewa ni CDM. CCM tulimkata kwa sababu tulikuwa na ushahidi wa yeye kutokuwa Mwadilifu. Ninyi mnaolalamika leteni hoja

Kwanza acha hoja za kitoto. Kutokuwa mwadilifu au fisadi??
You are an imbecile. Mnaolalamika kuwa alionewa ni CDM. CCM tulimkata kwa sababu tulikuwa na ushahidi wa yeye kutokuwa Mwadilifu. Ninyi mnaolalamika leteni hoja

What you are saying don't make sense. Mlimkata kwa sababu "hakuwa mwadilifu" je kukosa uadilifu ilikuwa ni pamoja na kuwa fisadi? au alianza kuwa fisadi lini? Maana kama alikuwa fisadi (kabla hamkamkata), unafikiri adhabu ya fisadi ni kukatwa na si kufikishwa mahakamani?? Now you know who is an imbecile??
 
Una maana gani mkuu kwa hili neno lair!????? Nijuavyo mimi maana ya hili neno ni mahali ambapo wanyama wa porini wanaishi sasa sijui unaunganishaje na Mwakyembe na mnyama wa porini????? Ungeamua kutumia lugha moja tu ambayo unayoielewa kamili iwe kidhungu ama kimang'ati usingejichanganya namna hii. Usiwe kama ma surrogate wa Donald Fred Trump wakibanwa wanarudisha habari za Obama. Hapa kaulizwa juu ya Richmond wewe unataka ajibu kuhusu ESCROW halafu unataka kudharau IQ za wenzako wakati wewe IQ ya kwako ni questionable.

Mkuu, the world is "Liar" and you know it is typo from the way i used it. Wewe hukujifunza kingereza shuleni? don't be silly....kisha unapoteza muda wangu na maneno mengi yasiyo na msingi... ESCROW na Richmond hazifanani kwa namna yoyote kwako? halafu tukisema low IQ mnakasirika..
 
Ni Tanzania pekee ambapo waziri anayelipwa na kodi za wananchi anawadhihaki wananchi kuwa anajua ufisadi ila hataki kusema. Amebaki kutishia pale anapolemewa na kitu fulani.
 
Mkuu, the world is "Liar" and you know it is typo from the way i used it. Wewe hukujifunza kingereza shuleni? don't be silly....kisha unapoteza muda wangu na maneno mengi yasiyo na msingi... ESCROW na Richmond hazifanani kwa namna yoyote kwako? halafu tukisema low IQ mnakasirika..
Kwani ukisema ulikosea anadhani utachekwa???? wewe ulikwenda shuleni kujifunza kuongea na kuandika kiingereza tu kama ungekwenda shuleni kwa maana ya kwenda shule basi ungejua kwanini nilikukosa. Unapotaka kutukana watu jaribu kuwa mkamilifu mwenyewe. Wewe uliuliza IQ za watu wakati wewe mwenyewe huko mkamilifu. Me say
 
Waziri wa habari Harrison Mwakyembe amewambia wabunge wa chadema kama wanataka ukweli wa ufisadi wa Richmond warudishe hoja hiyo bungeni.

Haya sasa karibuni kukanyagana maana hii hoja ni mwiba ambao watu wengine hawatakaki hata kuuona!

Dk Mwakyembe, Nassari wapimana

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe (kushoto) na Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nasari, Wawili hao walihamisha mjadala wa hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Rais Tamisemi na kurudisha suala la Richmond lililotokea mwaka 2008, huku Nasari akimtuhumu Dk Mwakyembe kuwa hakutenda haki katika ripoti yake na kumuondoa bila kumpa nafasi ya kujitetea aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa.

Dodoma. Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nasari na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe jana walichafua hali ya hewa bungeni na kusababisha mzozo mkubwa katika mjadala uliokuwa ukiendelea.

Wawili hao walihamisha mjadala wa hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Rais Tamisemi na kurudisha suala la Richmond lililotokea mwaka 2008, huku Nasari akimtuhumu Dk Mwakyembe kuwa hakutenda haki katika ripoti yake na kumuondoa bila kumpa nafasi ya kujitetea aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa.

“Huyu Mwakyembe ndiye aliyeongoza ripoti ya Richmond na hakumpa nafasi mheshimiwa Lowasa ajitetee, leo tena kapewa dhamana ya kuongoza Wizara ya Habari, Nape (Nnauye) ameondolewa lakini hakuna nafasi ya kumhoji Mkuu wa Mkoa... hakuna haki hapo,” alisema.

Kauli za Nasari zilimfanya Dk Mwakyembe kuomba mwongozo na aliposimama alisema: “Nilikuwa naongoza kamati na utaratibu mzuri wa kisheria ni kuwa, kama utaona kuna ushahidi wa kutosha hakuna sababu ya kumuita mtu, unaleta taarifa bungeni halafu Bunge linakuja kuamua.”

Dk Mwakyembe alisema katika taarifa yao, waliona hakuna sababu ya kumuita Lowassa kuhojiwa kwani ushahidi ulikuwa wazi na ndiyo maana hakutakiwa kuitwa mbele ya kamati badala yake walikuja kumshtaki bungeni.

“Huyu mtu wanayekuwa na mahaba naye kwa sasa, nasema wamlete hata leo waone kama hatutamnyoa kwa chupa, kanuni za kibunge zinaruhusu anaweza kuirudisha tena taarifa ya Richmond na ikaanza upya,” alisema Dk Mwakyembe.

Chanzo: Mwananchi

Data anazo. Alikuwa waziri wa sheria karibia miaka miwili na ameshindwa kumfikisha mahakama ya mafisadi. Kwani bunge ni mahakama? Wasichezee hela za walipa kodi.
 
Pelekeni hoja ya richmond uone kama lijinga
Na hizi zingine utalepeka lini?
Kagoda, rada, epa, escrow, lugumi, kiwira, Richmond, serikali, mikataba mibovu ya madini,......Nyumbu nyie mnaharibu nchi. Mahakama ya mafisadi inafanya nn kwa ufisadi wote huo......Kazi ya mahakama zenu nyima akina lema dhamana na kufunga wapinzani jela bila sababu za msingi na baadae kuachiwa huku watafuna raslimali za nchi wakitembea kifua mbele mtaani....
Na unyumbu wenu wa Lumumba ndo umetufikisha hapa.......WOTE MABASHITE
 
Kwani ukisema ulikosea anadhani utachekwa???? wewe ulikwenda shuleni kujifunza kuongea na kuandika kiingereza tu kama ungekwenda shuleni kwa maana ya kwenda shule basi ungejua kwanini nilikukosa. Unapotaka kutukana watu jaribu kuwa mkamilifu mwenyewe. Wewe uliuliza IQ za watu wakati wewe mwenyewe huko mkamilifu. Me say
Nitachekwa na nani, na wewe? ha ha, don't be ridiculous....., the rest you are talking shit. Ndiyo nimekuweka kwenye group ya low IQ. Hampendagi tu kuambiwa ukweli. Mbona wewe umeniambia kuhusu typo? when you talk nonsense, we should say so.
 
Mwakyembe ataleta ukweli gani tena mwingine wakati amekiri yeye mwenyewe bungeni tena waziwazi kuwa hakumpa Lowasa natural justice ya kusikilizwa?
Tatizo kubwa ni kuwa tunakariri sana pasipo hata kuelewa kwa nini jambo fulani linafanyika, mazingira yepi yanapelekea natural justice kufanyika. Kila kitu natural justice natural justice. Mfano itokee waziri amelewa, anatoa hotuba huku anapepesuka, anaongea dirty huku TV zikiwa live bado mtataka natural justice. Memo aliyoandika ipo wazi, kinyume cha utaratibu wa manunuzi, official letter ipo akielekeza mchakato wa manunuzi usifuatwe eti kuokoa taifa na giza bado tu unataka natural justice. Ninyi ndio wale mnakaa kimya wakati mkichojolewa nguo mnaongoja mpaka mkongomekwe dude kwa ajili ya kupata ushahidi wa kushtaki mahakamani
 
Maa
Kwanza acha hoja za kitoto. Kutokuwa mwadilifu au fisadi??


What you are saying don't make sense. Mlimkata kwa sababu "hakuwa mwadilifu" je kukosa uadilifu ilikuwa ni pamoja na kuwa fisadi? au alianza kuwa fisadi lini? Maana kama alikuwa fisadi (kabla hamkamkata), unafikiri adhabu ya fisadi ni kukatwa na si kufikishwa mahakamani?? Now you know who is an imbecile??

Maadili ni pamoja na kutokuwa fisadi. Dhambi yoyote iwe uzinzi, wizi, kusema uwongo etc ni ukosefu wa Maadili. So you now prove that you are are a professional IDIOT!
 
Maa


Maadili ni pamoja na kutokuwa fisadi. Dhambi yoyote iwe uzinzi, wizi, kusema uwongo etc ni ukosefu wa Maadili. So you now prove that you are are a professional IDIOT!

Tatizo la kwanza, you don't read between the lines. Hapo juu nilisema, kwa nini unasema nilimwacha kwa "Kukosa maadili" (Ufisadi) wakati mlitakiwa kuwa mmemfikisha mahakamani??? Yaani fisadi badala ya kufikishwa mahakamani wewe unasema unamwacha kwa kukosa maadili! I told you before, you write BS but try to be defiant and defensive. Be just a little smart dude..
 
Back
Top Bottom