KALOKAGATHOS
Member
- Jul 9, 2013
- 38
- 6
Imezoeleka kuwa waalimu wa kiume ndiyo huwapachika wanafunzi wa kike mimba,lakini hali imekuwa tofauti kwa mwalimu huyu (jina limehifadhiwa)wa shule ya secondary Mwakibete hapa jijini Mbeya.huyu mwalimu kahamia shuleni hapa siku si nyingi kutokea shule flani hapahapa Mbeya.kuna walimu wengi wa kike wana tabia ya kuhamia katika shule za mjini wakitokea shule za vijijini,lengo kubwa ni kuwafuata mabwana zao,lakini wengine huja mjini kwa lengo la kuponda raha na kuonja bata za Town,Shule ya sekondari Mwakibete imekuwa Moto wa kuotea mbali kati ya shule kadhaa za kata hapa mjini,mwalimu huyu mwanadada hajamaliza hata mhula tangu ahamie hapa Mwakibete.baada ya kumkosa bwana wake hapa mjini akaamua kujichanganya na wanafunzi.kama ilivyo ada vijana wengi wamekomaa japo bado wapo shule.huyu mwalimu kachanganyikiwa maana inasemekana alikuwa anatoka na wanafunzi kadhaa wa Form III na IV,yaani hajui mwenye mimba ni nani,balaa tupu,kwanza aliifanya siri lakini kwa sasa mambo fwaaaa!!!,sasa sijui nani atachukuliwa hatua kati ya mwalimu na wanafunzi hao.cha ajabu ni kwamba uongozi wa shule umetulia tuli.Wizara ya elimu vipi? kamati ya shule hebu fuatilieni hili,CWT mpoooo?