Mwalimu Kihere apewa mtaa Sahare Tanga

Mwalimu Kihere apewa mtaa Sahare Tanga

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
MWALIMU KIHERE APEWA MTAA SAHARE TANGA

Tanga imemtunuku Mwalimu Kihere Mtaa kwa kutambua mchango wake katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Siku moja katika miaka ya mwanzo sana baada ya uhuru ikatokea Mwalimu Kihere, Dossa Aziz, Abdul Sykes na Julius Nyerere walikuwa wako pamoja wakawa wanazungumza.

Mwalimu Kihere akawaambia wenzake hawa kuwa itapendeza kama historia ya TANU itaandikwa wao wakiwa hai.

Julius Nyerere akadakia akasema hiyo ni fikra nzuri sana.

Basi wakakubaliana historia ya TANU iandikwe na Nyerere akasema kuwa mtu ambae angefaa sana kuifanya kazi hiyo ni Abdul Sykes.

Nyerere alisema vile kwa kuwa Abdul hakuwa mbali na African Association na TANU na akiijua historia yote.

Bahati mbaya historia hii ilianza kuandikwa pale ofisi ya TANU, Lumumba lakini kazi hii haikufika mbali ikakumbwa na matatizo.

Abdul Sykes akajitoa katika uandishi wa historia ile.
Kisa hiki nimeshakieleza mara nyingi wengi wanakifahamu.

Mwaka wa 1984 Chuo Cha CCM Kivukoni kilipokuja kuchapa kitabu chake, ''Historia ya TANU 1954 - 1977,'' si Mwalimu Kihere wala Abdul Sykes walitajwa ndani ya kitabu hicho.

Hii ndiyo ikawa sababu ya Mwalimu Kiherere na wazalendo wengi kutofahamika katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Mwalimu Kihere ana mengi katika historia ya uhuru lakini mimi napenda kisa cha jinsi alivyokusanya fedha za safari ya Nyerere UNO mwaka wa 1955.

Mweka Hazina wa TANU na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika, Iddi Faiz Mafungo akafunga safari kwenda Tanga kwenda kuzichukua fedha hizo.

Wakati Iddi Faiz anarudi Dar es Salaam na fedha hizo basi lake kufika Turiani Iikasimamishwa na Special Branch Iddi Faiz akakamatwa.

Kisa cha kusisimua.

Lakini zaidi napenda sana kumkumbuka Mwalimu Kihere kwa mchango wake katika kuinusuru TANU na mgogoro mkubwa uliotishia kukigawa chama katika makundi mawili hasimu katika mjadala wa Kura Tatu, Parish Hall, Tabora mwaka wa 1958.

Mwalimu Nyerere alitambua kuwa TANU ilikuwa hatarini kwa sababu ya masharti ya kibaguzi ya kupiga kura na kupigiwa kura.

Kwa ajili hii basi siku chache kabla ya mkutano wa Kura Tatu Tabora, Nyerere na Amos Kisenge wakaenda Tanga kukutana na Mwalimu Kihere, Hamisi Heri na Sheikh Abdallah Rashid Sembe kufanya mashauriano ya siri.

Kikao hiki cha mashauriano na kupanga mkakati vipi watakailiana na wapinzani wa Kura Tatu ndani ya chama na dua iliyofanyika Mnyanjani kijiji kidogo nje ya Tanga ndicho kilichompatia Mwalimu Nyerere ushindi na kuwashinda wapinzani wote Kura Tatu wakiongozwa na Sheikh Suleiman Takadir, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU, Makao Makuu, New Street.

Kwa ujanja mkubwa sana Mwenyekiti wa mkutano wa Kura Tatu Mwalimu Nyerere alimpasia Mwalimu Kihere kwa muda kiti chake cha uenyekiti akidai kuwa yeye anataka achangie mjadala kama mjumbe.

Ndoana ikanasa kwenye koo la samaki.

Mwalimu hakujadili bali alitoa hotuba ambayo ilibadili mle ukumbini fikra za wapinzani wengi wa Kura Tatu.

Kwa nusu karne mkakati huu wa Tanga na kisomo cha Mnyanjani kupambana na "wabishi'' ndani ya TANU ilibakia siri kubwa sana na siri hii kubwa ikazidi kuwa siri kubwa kadri miaka ilivyokuwa ikiyoyoma na wazalendo hawa; mmoja baada ya mwingine wakiaga dunia hadi wakabaki wawili, Sheikh Abdallah Rashid Sembe na Nyerere.

Nyerere akiamini kabisa kuwa siri ya Tanga na Mnyanjani itabaki siri hadi karibu mwaka mmoja anafariki 1999 ndipo alipomdhihirikia kuwa siri imefichuka.

Siri ilifichuka mwaka wa 1998 kitabu cha Abdul Sykes kilipochapwa Uingereza.

Bila shaka Mwalimu Nyerere labda alijiuma kidole aliposoma katika kitabu ule mkutano wao wa siri waliofanya Tanga mjini kisha wakahamisha kikao kwenda Mnjanjani walipofanya, ''tawasul,'' usiku kumuomba Allah asahilishe mpango wao waliopanga kuutekeleza Tabora katika Mkutano Mkuu wa TANU kujadili Kura Tatu.

Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akishiriki katika dua hii.

Wazalendo hawa wanastahili na wana haki ya kukumbukwa kwani wamefanya mengi.

Kwa kweli ni muhimu sana historia zao zikakumbukwa na kuhifadhiwa.

1660665962425.png
1660666006015.png

Mwalimu Kihere​
 
Hakika Wana Tanga wamefanya maamuzi ya Busara ktk kuwakumbuka watu muhimu Sana katika historia ya inchi hii,nawapa kongole Sana!
 
Mzee said si useme walienda kuloga tuuu...!
Maisha...
Ungejaaliwa kuuliza maswali kwa adabu na ustaarabu kwangu nimekupa mengi niliyokutananayo katika utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes.

Haya sikuyaweka katika kitabu kwa kuwa yalinishtua na kunishangaza sana.
Waafrika hatuwezi kuwekwa mbali na imani zetu za asili.

Hayo uliyosoma ni dua kwa Mwenyezi Mungu:

''Nyerere and Kissenge were taken to Mnyanjani and the tawaswil was performed there under great secrecy. Attending the occasion were Abdallah Rashid Sembe, Sheikh Dhikr bin Said, Mzee Zonga, Hemed Anzwan, Salehe Kibwana, who was a prolific poet, Akida Boramimi bin Dai and Mmaka Omari.

Chosen to recite the Holy Qur’an was Mwalimu Kihere’s uncle, Sheikh Ali Kombora.''
(Kutoka kitabu cha Abdul Sykes)
Ndugu yangu unadhani hii historia ni ya kufanyiwa kejeli kwa lugha kama hiyo yako?
Au ni hasad ikuangaishayo kwa nini Waislam wako mstari wa mbele na katika kupigania uhuru wa Tanganyika?

The untold story...
 
Waislam wameifanyia mengi Tanganyika. Nitafurahi endapo Katiba mpya itaandikwa kiarabu kuuenzi uislam....na sheik Mohamed Said ndiye awe mwenyekiti wa Tume

Kiroho safi
 
Bora hii dini haikushika madaraka sijui kama taifa tungekua wapi
Tajiri...
Allah kakataza dhulma.
Asingebaguliwa mtu kwa sababu ya dini yake.

Soma kipande hicho hapo chini ujifunze:

#25

Edward A Chapa said:

Wewe ni mdini Una udini. Hapo ndio natofautiana na wewe! Na mtu kama wewe ndio kila sehemu mnaweka udini na Kupanda mbegu mbaya ya Udini katika nchi yetu. Kila kitu wewe unaleta Udini tuu. Ninyi mnarudisha nyuma maendeleo kwa ajili ya Udini.

Bwana Edward huijui historia ya uhuru na sababu walioshika serikali wanaiogopa.

Laiti wazee wetu wangekuwa wabaguzi wa dini Nyerere asingekuwa kiongozi wa TAA, TANU na Tanganyika.

Je, unawajua waliompokea Nyerere Dar es Salaam ya miaka ya 1950 na kuishi na yeye kama ndugu yao?

Unajua nyumba aliyoishi Nyerere Dar es Salaam baada ya kuacha kazi ya ualimu Pugu?

Unaijua historia ya Abdul Sykes na mkewe Mama Daisy na Nyerere na Mama Maria?

Je na ya Ali Msham na Nyerere na Mama Maria?…

Edward A Chapa said:

Wewe ni mdini Una udini. Hapo ndio natofautiana na wewe! Na mtu kama wewe ndio kila sehemu mnaweka udini na Kupanda mbegu mbaya ya Udini katika nchi yetu. Kila kitu wewe unaleta Udini tuu. Ninyi mnarudisha nyuma maendeleo kwa ajili ya Udini.

JIBU

Bwana Edward huijui historia ya uhuru na sababu walioshika serikali wanaiogopa.

Laiti wazee wetu wangekuwa wabaguzi wa dini Nyerere asingekuwa kiongozi wa TAA, TANU na Tanganyika.

Je, unawajua waliompokea Nyerere Dar es Salaam ya miaka ya 1950 na kuishi na yeye kama ndugu yao?

Unajua nyumba aliyoishi Nyerere Dar es Salaam baada ya kuacha kazi ya ualimu Pugu?

Unaijua historia ya Abdul Sykes na mkewe Mama Daisy na Nyerere na Mama Maria?
Je na ya Ali Msham na Nyerere na Mama Maria?

Je ya Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir na Nyerere?
Je historia ya Mshume Kiyate, Mwinjuma Mwinyikambi na Max Mbwana na Nyerere?

Bi. Shariffa bint Mzee na Suleiman Masoud Mnonji na Sheikh Yusuf Badi Lindi, Mtwara na Mikindani Waislam wengi wasio na hesabu Tanganyika nzima.

Wapi umesikia wametajwa?
Hawa walimbagua Nyerere kwa kuwa alikuwa Mkatoliki?

Hivi kuandika historia za mashujaa hawa waliofutwa katika historia ya uhuru wetu ndiyo imekuwa ubaguzi wa dini?

Au hujui kama historia hii ilifutwa?
Unawajua waliotishwa na historia hii na bado inawatia hofu hadi leo?

Nini sababu ya uoga huu?

Je uliridhika kuona kuwa historia hii haikuwa inafahamika na leo unachukia kuona mimi nimeiandika na watu wameanza kujua ukweli.

Unajua kuwa wenye madaraka ya kuongoza nchi si Waislam na mgao ni 20:80?

Rais Mkapa alielezwa hali tuliyonayo na akaomba ushahidi na ushahidi akapewa na Prof. Hamza Njozi kupitia kitabu cha mauaji ya Mwembechai.

Kitabu kilipigwa marufuku.
Huu ndiyo udini wenyewe.

Hili ni tatizo na linafahamika.
Wewe ungeridhika kuona Waislam wamehodhi serikali kwa 80%.

Sidhani.

Hii ndiyo mbegu mbaya uliyoitaja ati inapandwa na Waislamu.
Ukipenda naweza nikakusomesha somo hili.

Udini ulianza tu baada ya uhuru mwaka 1961 kwa kuwekwa mikakati ya kufuta historia ya Waislam katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Hii ni mada ya inayojitegemea yenyewe.

Soma historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika si hii iliyoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni mwaka wa 1981.

Soma kitabu cha Abdul Sykes na mwandishi ni mie.
Kitabu kinakwenda toleo la tano toka kuchapwa mwaka wa 1998.

Kitabu kimependwa kwa kuwa kina historia ya kweli inayowavutia wasomaji wengi wao ni vijana wa kizazi ambacho hakikuwepo wakati wa kudai uhuru.

Ukweli wote umo humo ndani.

Kitabu hiki ndiyo sababu ya kuandikwa Biography of Julius Nyerere ikidhaniwa kuwa kinaweza kujibu masuala ndani ya kitabu cha Abdul Sykes.

Yapo mengi.
Ikiwa hujui kitu uliza wenye kujua ufahamishwe.

Mimi siandiki kufanya maskhara.
Naandika kuitafutia amani ya kweli nchi yangu.

Naandika ili viongozi wetu wachukue hatua kurekebisha hali hii.
Angalia picha hizo hapo juu.

Ulipatapo kuziona popote.
Ziko nyingi sana na zinajieleza wenyewe.

Je unaona ni sawa kuwa historia hii isifahamike?
Bado unaamini kuwa Waislam ni wabaguzi hata baada ya ushahidi huu?
 
Back
Top Bottom