Mwalimu Maganga, Katibu Mkuu CWT aliyekataa uteuzi wa Ukuu wa Wilaya arudishwa kwenye Ualimu

Mwalimu Maganga, Katibu Mkuu CWT aliyekataa uteuzi wa Ukuu wa Wilaya arudishwa kwenye Ualimu

Pantomath

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2019
Posts
842
Reaction score
3,449
Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke, Elihuruma Mabelya amemtaka Mwalimu Japhet Maganga kurejea kazini kufuatia Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- Utumishi, Juma Mkomi kutoidhinisha maombi ya mwalimu huyo kupata kibali cha kuazimwa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mabelya, Maganga ni muajiriwa wa Manispaa ya Temeke katika nafasi ya ualimu na aliomba kibali cha kuazimwa kwa vipindi tofauti vya miaka mitatu, kuanzia mwaka 2017- 2020, kisha 2020 hadi Septemba 30, 2023.

“Mwalimu Maganga aliomba tena kibali cha kuazimwa kwa mara ya tatu ambapo Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Utumishi hajaridhia maombi hayo,

“hivyo, Mwalimu Maganga M. Japhet anapaswa kurejea kwenye kituo chake cha kazi mara moja, mnamo tarehe 01, Oktoba 2023,” kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi Manispaa ya Temeke.

Itakumbukwa mnamo Januari 25, 2023, Maganga aliteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa, ingali ni Katibu Mkuu wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) lakini hakuafikiana na uteuzi huo.

====

TANGAZO KWA UMMA KUREJESHWA KWENYE KITUO CHA KAZI CHA AWALI MKURUGENZI WA MANISPAA YA TEMEKE ANAPENDA KUTOA TAARIFA KUWA MWALIMU MAGANGA M. JAPHET MWENYE CHECK NO.9607099 MWAJIRIWA WA MANISPAA YA TEMEKE MWENYE CHEO CHA MWALIMU MWANDAMIZI DARAJA A, ALIOMBA KIBALI CHA KUAZIMWA CHA TAREHE 21 AGOSTI, 2017 NA KUPEWA KIBALI CHA KUAZIMWA NA CHAMA CHA WALIMU TANZANIA (CWT) KWA BARUA KUMB NA. CA.87/164/01/'Β'/160 YA KATIBU MKUU OFISI YA RAIS -UTUMISHI.

KIBALI HIKI KILIKUWA CHA MIAKA MITATU KUANZIA DESEMBA 2017 HADI SEPТЕМВА 30, 2020. AIDHA MWALIMU MAGANGA ALIOMBA NYONGEZA YA KIBALI KWA BARUA YA TAREHE 01 JUNI, 2020 NA KATIBU MKUU OFISI YA RAIS -UTUMISHI ALIMPA KIBALI CHA NYONGEZA KUMB NA CA.164/228/01/'V'/68 CHA TAREHE 10 AGOSTI, 2020 KINACHOISHIA TAREHE 30 SEPTEMBA, 2023.

MWALIMU MAGANGA ALIOMBA TENA KIBALI CHA KUAZIMWA KWA MARA YA TATU AMBAPO KATIBU MKUU OFISI YA RAIS - UTUMISHI HAJARIDHIA MAOMBI HAYO HIVYO BASI MWALIMU MAGANGA M. JAPHET ANAPASWA KUREJEA KWENYE KITUO CHAKE CHA KAZI MARA MOJA MNAMO TAREHE 01 ОКТОВА, 2023.

IMETOLEWA NA:

MKURUGENZI MANISPAA YA TEMEKE
23.09.2023


1741166291239.png

Pia soma: Katibu mkuu CWT agoma kurudi Temeke kufundisha
 
Kwhy anaenda kuwa mwalimu wa darasa form two C au sijaelewa
 
Hii inanikumbusha kauli moja iliwahi kusemwa na wahenga kuwa ukibebwa bebeka na ukilishwa kamwe using'ate kidole kikulishacho!

Hatimaye rasmi sasa bwana huyo kukiona cha moto kwa kurudishwa kituo chake cha kazi kama Mwalimu Mwandamizi Daraja A katika Manispaa ya Temeke.

Ikumbukwe kwamba Ndg. Japhet Maganga na Viongozi wenzake wa CWT walikataa uteuzi huo January mwaka huu na wakasahau kwamba wanafanya kazi katika serikali hiyo hiyo yenye mamlaka ya kuwasubiri (hii imedhihirisha usemi wa aliye juu mgonje chini)

Leo nilishtuka baada ya kuona barua hii Kutoka Tamisemi ikiwa imeandikwa na manispaa ya Temeke. Maelezo yote yapo kwenye barua hii;

Screenshot_20230923-181508.png
 
Bwana Maganga ana akili sana tena kuzidi wewe mtoa mada alijua fika kuwa cheo cha ukuu wa wilaya ni cheo cha kwenda kudhalilishwa na alikuwa ametegwa ali atenguliwe na kupigwa bench kwa mgongo wa kupangiwa kazi nyingine …kwa hiyo alikuwa mbele ya muda na alifikiri zaidi yako….

Hivi kwa akili yako kabisa alikataa tuu bila kujua kitakachotokea? Alijua fika…
Bora afundishe kwa uhuru kabisa kuliko kwenda kudhalilishwa kwenye ukuu wa wilaya…
Yuko wapi jerry muro? Leo tuu mkuu wa wilaya ya Mtwara katenguliwa…

Alifanya jambo sahihi kabisa
 
Bwana Maganga ana akili sana tena kuzidi wewe mtoa mada alijua fika kuwa cheo cha ukuu wa wilaya ni cheo cha kwenda kudhalilishwa na alikuwa ametegwa ali atenguliwe na kupigwa bench kwa mgongo wa kupangiwa kazi nyingine …kwa hiyo alikuwa mbele ya muda na alifikiri zaidi yako…
Sasa unajua pesa aliyokuwa anapata kama Katibu Mkuu CWT ni kubwa na Ingeweza kulingana na Pesa ya Mkuu wa wilaya.

Ila kwa sasa anapelekwa kurudi kama Mwalimu mwandamizi Daraja A unajua anapata kiasi gani na atafundisha Shule ya msingi unajua udhalilishaji na majuto atakayopata maana hata diwani atakuwa boss wake sasa....KIPI NI BORA?
 
Nzi wanasemaga we ukijua hivi wenzio wanajua vile
Huu hapa 🤣🤣 nahisi alidanganywa na wtu akasahau nyadhifa aliyo nayo ni nyadhifa ya Kuhitaji Kibali kwa mteuzi wa mtu aliyeteuliwa na yule ambaye yeye amemgomea uteuzi wake (Yaani kifupi aliyemuonyesha dharau)
 
Mantiki ya taarifa za mwajiriwa kuwekwa hadharani ni zipi?

Alipaswa apewe barua yake kisha aripoti kazini. Kubandikwa kwenye mbao za matangazo ni upuuzi usio na maana.

Mbona kabla ya hapo, vibali vyake havikuwa wazi?

Pathetic!.
 
Sasa unajua pesa aliyokuwa anapata kama Katibu Mkuu CWT ni kubwa na Ingeweza kulingana na Pesa ya Mkuu wa wilaya...

Ila kwa sasa anapelekwa kurudi kama Mwalimu mwandamizi Daraja A unajua anapata kiasi gani na atafundisha Shule ya msingi unajua udhalilishaji na majuto atakayopata maana hata diwani atakuwa boss wake sasa....KIPI NI BORA?
Aliyekuzidi kakuzidi wala usilalame
 

21 September 2023
Uvinza, Kigoma
Tanzania

Uvinza kwa waka moto, mheshimiwa waziri mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa awa mbogo


View: https://m.youtube.com/watch?v=osWgD5N1OuU

Waziri mkuu Mh. Kassim Majaliwa akiongea akiwa ameongozana na mkuu wa mkoa wa Kigoma Kamishna wa Polisi CP Thobias Andengenye, mkuu wa wilaya ya Uvinza DC Dina Dina Mathamani, mkurugenzi wa mtendaji wa halmashauri ya Uvinza Bi. Zainab Mbunda na vigogo wengine wa mkoa wa Kigoma, waziri mkuu ahoji uongozi kushidwa kuhakikisha majengo mapya ya hospitali na vifaa tiba kuanza kufanya kazi ya kutoa huduma kwa wananchi.


TOKA MAKTABA:
31 January 2023

RC ANDENGENYE AMUAPISHA MKUU WA WILAYA UVINZA​


Posted On: January 31st, 2023

1695483335570.png

HABARI PICHA: HAFLA YA KUMUAPISHA MKUU WA WILAYA YA UVINZA DINAH MATHAMANI ILIYOFANYIKA JANURI 31, 2023 KATIKA UKUMBI WA KATIBU TAWALA OFISI YA MKUU WA MKOA KIGOMA
Source : https://kigoma.go.tz/new/rc-andengenye-amuapisha-mkuu-wa-wilaya-uvinza-5
 
Back
Top Bottom