Mwalimu Maganga, Katibu Mkuu CWT aliyekataa uteuzi wa Ukuu wa Wilaya arudishwa kwenye Ualimu

Mwalimu Maganga, Katibu Mkuu CWT aliyekataa uteuzi wa Ukuu wa Wilaya arudishwa kwenye Ualimu

Hii inanikumbusha kauli moja iliwahi kusemwa na wahenga kuwa ukibebwa bebeka na ukilishwa kamwe using'ate kidole kikulishacho!

Hatimaye rasmi sasa bwana huyo kukiona cha moto kwa kurudishwa kituo chake cha kazi kama Mwalimu Mwandamizi Daraja A katika Manispaa ya Temeke.

Ikumbukwe kwamba Ndg. Japhet Maganga na Viongozi wenzake wa CWT walikataa uteuzi huo January mwaka huu na wakasahau kwamba wanafanya kazi katika serikali hiyo hiyo yenye mamlaka ya kuwasubiri (hii imedhihirisha usemi wa aliye juu mgonje chini)

Leo nilishtuka baada ya kuona barua hii Kutoka Tamisemi ikiwa imeandikwa na manispaa ya Temeke. Maelezo yote yapo kwenye barua hii;

aandike barua ingine ya kukubali
 
Huyoticha itakuwa alishawalia waticha sana atakuwa namabiznezi hapatown hananjaa ndomana akagomeaga kupeleka chocho na tucheo twa kupelekeshwa!! Hiyo kazi aliyoteuliwa hatamimi sitaki ni yamadhambi...ukaibie watu makura,ukanyanyase wapinzani no. asa kisa nini?
Ticha zuga hapojob hku unapigwa biznez zako hapatown,wanaomuonea huruma wajihurumie wao.
 
Kwa unamaanisha vetting ya mweshimiwa Rais haikuwa sAwa kumchagua
Kwani hiyo vetting inafanywa na malaika? Inafanywa na binadamu tuu, rais ni binadamu na hao wanaomsaidia ni binadamu na wana mapungufu yao mengi tena sana tu. Ni mara ngapi teuzi zimefanyika tena kwenye uongozi huu huu wa rais samia na kutenguliwa kabla hata ya mtu kuapishwa kushika nafasi hiyo??
 
Watanzania asilimia kubwa sisi ni wajinga sana, Kwan ukipata uteuzi lazima ukubali? Kwann tusiheshimu maamuzi yake? Serikali ya CCM imejaa viongozi wa wapumbavu kabisa, kulikuwa na umuhimu gan wa ku publish hiyo barua? mbona hizo zingine zilizopita hazikuwahi kuwekwa public kama hivyo? Tunajua mmefanya hivyo kumkomoa kwa kukataa uteuzi wa ukuu wa wilaya yaan mmekaa kukomoana tu laiti ningekuwa mm ndio Maganga naachana na hiyo kazi yenu ya kipumbavu
 
Watanzania asilimia kubwa sisi ni wajinga sana, Kwan ukipata uteuzi lazima ukubali? Kwann tusiheshimu maamuzi yake? Serikali ya kijinga kabisa, kulikuwa na umuhimu gan wa ku publish hiyo barua? mbona hizo zingine zilizopita hazikuwahi kuwekwa public kama hivyo? Tunajua mmefanya hivyo kumkomoa kwa kukataa uteuzi wa ukuu wa wilaya yaan mmekaa kukomoana tu laiti ningekuwa mm ndio Maganga naachana na hiyo kazi yenu ya kipumbavu
Kuwa na akili na wewe..unamgomeaje Rais!!?
 
Kwahy mnasema hii nyaraka sio sahihi!?he was public figure lzm ijulikane hvyo asije tapel watu kwa cheo mfu.
 
Mwenzako alienda kuripoti alafu baadae ndio akachokoa
20230924_120215.jpg
 
Ukishakuwa mtumishi wa umma unaridhia miiko ya kiutumishi (codes of ethics) na unapaswa kuiishi, huwezi kuishi utakavyo na huwezi kuivimbia serikali ambayo hiyo hiyo ndiyo inakupa mkate.

Hivi kwa busara ya kawaida tu, unamtuma mwanao kazi ya nyumbani afanye anakukatalia halafu na majirani zako wanashuhudia hivi utajisikiaje; lazima apewe "panadol" ajifunze adabu
 
Nilidhani kwakuwa rais ni mama basi hakutakuwa na visasi kwenye utawala wake!
Kwani kukataa uteuzi ni uvunjifu wa katiba au sheria? na kama ndivyo basi si ashitakiwe kwa mujibu wa sheria hizo na sio kumuathiri kisaikolojia?
Mungu ibariki Tanzania kwakweli!
 
Back
Top Bottom