Mwalimu Nyerere: Hii Katiba ya Tanzania, tukimpata Rais asiye na busara anageuka kuwa Mungu

Mwalimu Nyerere: Hii Katiba ya Tanzania, tukimpata Rais asiye na busara anageuka kuwa Mungu

Nakubaliana na wewe, Mzee


Nakubaliana na wewe, Mzee Mandela aliona mbali na akaiacha nchi yake katiba ambayo haiwezi kuchezewa na kufinyangwa finyangwa kwa matakwa ya kiongozi aliyepo madarakani ndiyo maana Zuma anaona kiti cha moto. Kinachomtia kiwewe ni katiba ambayo inalinda maslahi ya taifa na siyo matakwa na utashi wa aliyekalia kiti cha urais.

Hiyo ndo tofauti ya Mandela na Nyerere huwezi kumwelewa Mandela kama una akiri ndogo
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa hii katiba yetu, inampa mno madaraka makubwa sana, mwalimu alisema kuwa kama tukimpata Rais asiyekuwa na busara, kwa katiba hii Rais anageuka kuwa mungu, unakubaliana na kauli ya mwalimu Nyerere?
Mkuu Mwalimu JKN ni mmoja wa wanasiasa wa kiwango cha juu ambao hatokuja kusahaulika upesi.

Lakini kumbuka kuna watu walifungiwa vizuizini, huku wakuu wa wilaya wakipewa kazi ngumu ya kuhakikisha hao waliopigwa karantini ya kisiasa wasitoke nje ya eneo la wilaya.

Kwa maneno mengine tendo la kumzuia mtu asitoke kwenye eneo moja tayari ni uvunjaji wa haki za kibinadamu.

Yapo mengi kama yale ya JKN alipomchukia mtu kushindwa kabisa kumsamehe, ambayo huwa nayapata kwa Baba yangu mzazi ambaye Mungu kamjalia jana kafikisha miaka 83, alifanya kazi katika sehemu kubwa ya awamu ya kwanza.

Tumwache Ngosha achape kazi, historia itakuja kumhukumu kama inavyomhukumu Baba wa Taifa letu kwa sasa.
 
Call a spade a spade plz.
sio kila kilichotamkwa na nyerere ni cha kishujaa/busara.
Hili la katiba mwl. yupo sahihi kabisa.
Ila kama aliona udhaifu uliopo kwenye katiba kwanini hakulifanyia kazi ili katiba iwe kwa maslahi ya watanzania wote?
 
Yani viongozi wa zamani walikuwa na maono sana
 
Katiba ya USA iliandikwa mwaka 1787 na inatumika mpaka leo. Mwl Nyerere na uwanafalsafa wake wote alichokishindwa ni kutuachia katiba itakayokidhi matakwa ya wananchi kwa miaka mingi. Ila kutuambia eti akija mtu mwenye nia tofauti katiba haifai ni udhaifu mkubwa. But kila kitu alichofanya nyerere kinaonekani ni chakishujaa
Yake kaiandika mwaka 77 na haikufaa tangu ameiandaa mpaka amekufa na haitakaa ifae.... je mwandishi wa katiba ya usa mwaka 1787 alikiwa anamzidi fikra za kidemokrasia Nyerere? Jibu ni ndiyo.... sasa je baada ya Nyerere kugundua kuwa haifai kwa nn hakuibadili? Labda tukamuulize mzee Butiku atatusaidia.....
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa hii katiba yetu, inampa mno madaraka makubwa sana, mwalimu alisema kuwa kama tukimpata Rais asiyekuwa na busara, kwa katiba hii Rais anageuka kuwa mungu, unakubaliana na kauli ya mwalimu Nyerere?

Kwani ilitungwa lini na ni nani alikuwa Rais?
 
  • Thanks
Reactions: ydn
Katiba hii 1977 ilitungwa na jopo lililopewa jukumu la kutunga katiba ya CCM.Baada ya kamaliza ya CCM wiki moja wakaanza hii mlionayo na wakati huo Nyerere akiwa mkuu wa nchi ...sasa kama kweli alikua na nia nzuri kwanini aliipitisha kwa kutia mkono wa ndio...Wanasiasa wa hivi waogopwe sana
 
  • Thanks
Reactions: ydn
Katiba ya USA iliandikwa mwaka 1787 na inatumika mpaka leo. Mwl Nyerere na uwanafalsafa wake wote alichokishindwa ni kutuachia katiba itakayokidhi matakwa ya wananchi kwa miaka mingi. Ila kutuambia eti akija mtu mwenye nia tofauti katiba haifai ni udhaifu mkubwa. But kila kitu alichofanya nyerere kinaonekani ni chakishujaa
YA Jaji Warioba na Kikwete iliishia wapi?? Ukipata jibu hili ndio urudi nyuma kutafakari hiyo ".... mbaya" ya mwalimu
 
  • Thanks
Reactions: ydn
J

Namlaumu sana na hata simwombei, alijua shida itatupata na akakaa kimya.
Pale unapojua tatizo halafu usifanye chochote unakuwa wewe ndio mwenye kubeba lawama wala sio huyo aliokosa Busara
Tehehehe, kizazi chako kimeamini vivyo, hata kesho kitukuu chako kikimlaumu Kikwete yote heri.
Ila ashukuriwe mwalimu, japo aliowaamini sicho walichomuaminisha.
Mwalimu alipata kukili (kiutu uzima ni kama aliomba samahani) kwamba kuna mabaya aliyafanya, na kuna mazuri aliyafanya,
Hivyo hatuna budi kujifunza katika yale mazuri.
Amini amini, nakwambia kama leo Pogba angelikuwa Mwalimu enzi zile, katu hasingeng'atuka kuanzia Tanu mpaka leo kiti kingekuwa bado kimekaliwa na yeye tu.
 
Ila Nyerere akaja kuziua na Kuanzisha Viota na Vitalu vya kukuzuia Mafisadi na ndio Leo hii wanatesa Taifa wote walisoma Enzi za Mwalimu.
Walisoma enzi za mwalimu, ila wakapata kazi enzi za Mwinyi, kipindi cha dirisha na milango ikiwa wazi.
Wakasahau kwamba kuna misingi wameiacha ambayo ndio imewalea na kuwafikisha walipo.
Kilichotokea sikitofaitoshi na simulizi la Adam na Eva/Hawa. Walipata kuyajua mazuri yote, na Mungu kwa upendo wake kwao hakutaka wayajue MABAYA, maana mabaya ndio yamebeba MAUTI. Kwa ukengeukaji wao Nyoka/Shetani akamtumia Hawa/Eva kumrubuni na akarubunika kweli kweli, na kwa tamaa zao, wisho wa siku wakajikuta wamekula tunda la mti wa katikati, walilokatazwa na Mungu, kilichotokea sipendi kumalizia, bali ni matokeo ya wewe ku comment ulicho comment sahivi.
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa hii katiba yetu, inampa mno madaraka makubwa sana, mwalimu alisema kuwa kama tukimpata Rais asiyekuwa na busara, kwa katiba hii Rais anageuka kuwa mungu, unakubaliana na kauli ya mwalimu Nyerere?

Mkuu, kwa vile Watanzania kwa ujumla wetu tumeamua kumuenzi Nyerere kama Nyerere kwa uadilifu wake, ni vyema tuepuke kuanzisha mada/mijadala ya aina hii ili wengi wasikwazwe. Hili swali jibu lake li wazi kabisa. Katiba iliandikwa na Nyerere mwenyewe kwa misingi ya kidikteta kwa vile hakutaka kuletewa "bugdha" na mtu yeyote katika uendeshaji wake wa nchi. Na katika hilo alikuwa na nia njema kabisa ya kuendeleza Taifa na si kujineemesha kibinafsi.

Lakini hakuzingatia ukweli kwamba serikali haiendeshwi kwa utashi wa mtu mmoja na kwamba inabidi iandaliwe katiba itakayoweka na kusimamia mfumo mpana zaidi unaodhibiti yeyote atakayekuwa sehemu ya uongozi wa nchi bila kujali wadhfa wake. Na alianza kupata taabu mara baada ya kuachia urais. Sikiliza hotuba zake (wosia wa baba) zinazotolewa ITV utagundua nyingi ni za kumhukumu aliyemrithi kwa kushindwa kuongoza nchi vizuri. (sikiliza kile kipande: ... rais anayeweza kumwambia mkewe, he, hatukuja ikulu kufanya biashara!) Ukweli ni kwamba aliacha katiba inayomwezesha rais kufanya anachotaka bila kuwajibika kwa yeyote kama alivyojigamba rais wa Ufaransa baada ya vita kuu ya pili, Charles de Gaule: "L'etat, c'est moi".

Sasa kukumbuka alichosema kuhusu katiba haitusaidii chochote zaidi ya kutuonyesha chimbuko la tatizo la msingi la taifa letu: katiba mbovu na utawala wa kiimla kupitia CCM. Huo ndio urithi mtata aliotuachia tunaotakiwa kuachana nao. Yeye alikuwa muadilifu, mzalendo na mwenye nia ya kuendeleza wote bila ubaguzi; tumuenzi kwa hilo. Lakini, kwa kukosa mikakati sahihi, alituachia zigo la misumari; tulitue basi. Tusichanganye mambo.
 
Back
Top Bottom