Mwalimu Nyerere: Hii Katiba ya Tanzania, tukimpata Rais asiye na busara anageuka kuwa Mungu

Mwalimu Nyerere: Hii Katiba ya Tanzania, tukimpata Rais asiye na busara anageuka kuwa Mungu

Akimalizana na sisi atakukuja kwenu baadae kwa wale na wale wengine..Ccm wanavurugana hata miaka miwili JPM Mpiana hajafikisha
 
Tatizo ni sie Watanzania wenyewe. Subiri muone, uzi huu huu watakuja watu watasifia yanayotokea kuwa ni sawa. Sasa mnadhani hata mwenda wazimu akivua nguo hadharani na kucheza sindimba kama kuna watu wanamshangilia unadhani ataacha?
 
Kwa bahati mbaya Yeye na Sisi hatukuchukua hatua yo yote. Leo hii Yeye hayupo, sisi tupo, hatuna la kufanya kwani tulitakiwa tupate ufumbuzi wakati ule ule alipotumbia. Yetu macho tu!

Lakini hiyo katiba haikujiandika yenyewe.
 
Jamaa alikuwa kama Nabii. Aliyasema haya miaka 35 iliyopita sasa yamekuwa kweli. RIP Baba wa Taifa.
Mimi sijaelewa kama yeye alijua kwanini asiibadilishe yeye mwenyewe.wakati yeye ndio alioitunga
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Ishara za mtu huyu kwamba hana roho ya binadamu zilianza pale alipoanza kuuza nyumba za serikali wakati wafanyakazi wa serikali wamo ndani. Aliuza nyumba na watu waliomo ndani. Ishara nyingine ni wakati akiwa waziri wa barabara. aliwabomolea watu nyumba bila huruma. alitaka kubomoa hata jengo la TANESCO hapa Ubungo. Aliwaambia vikongwe na wagonjwa wa Kigamboni kama hawawezi kulipa nauli ya kivuko basi wapige mbizi. Zile zilikuwa ni dalili za mawingu.

Huyu mtu ni hatari. Kuna mke wake wa kwanza pale Changanyikeni alimtelekeza hadi leo. Huyu mama ana binti mkubwa ambaye kwa sasa huyo binti kaolewa. Anasali Roman Catholic pale Chapel ya UDSM.
 
"Katiba hii imenipa Madaraka makubwa sana, siku atakuja mtu ataitumia atakavyo na kuwa kama Mungu" - Mwl. Nyerere 1982!

Sasa watanzania wataona umuimu wa mabadiliko ya katiba hasa hasa wanachama wa CCM
 
Ameonyesha ni jinsi gani mtu mmoja anaweza kulisababishia taifa hasara katika nyanja za kiuchumi, kijamii, kiusalama, kisiasa, na hamna cha kumfanya.

Kinadharia katiba inasema mamlaka yanatoka kwa wananchi lakini kiuhalisia wananchi wamepokwa nguvu, wako powerless, hawawezi kufanya chochote kuiwajibisha serikali, sio kwenye sanduku la kura, sio bungeni ambako ni sawa na mkutano wa halmashauri kuu ya CCM, au hata kutoa maoni tu, na ukinung'unika jiandae kutekwa na kupotezwa.

Magufuli kathibitisha pasipo na shaka kuwa katiba inayotegemea utashi wa mtu mmoja ni moja ya mfumo mbovu kabisa wa kiutawala.

Kaonyesha matundu kwenye katiba yetu ambayo zamani yalikuwa yanasemwa kwa kinadharia, lakini sasahivi tunayashuhudia madhara yake live kutokana na matendo ya mtu mmoja kutodhibitiwa kikatiba na yeye kufanya atakavyo bila kujali wengine.

Magufuli ni kilele cha uthibitisho wa ubovu wa katiba tuliyonayo. Katukwamisha na kuturudisha nyuma. Nchi haina mwelekeo.

Kwa kadhia tuliyopitia hii miaka michache, inaonyesha ni jinsi gani pamoja na kuwa katiba ya warioba ina afadhali kuliko tuliyonayo sasa, bado na yenyewe ina mapungufu.

Tunahitaji katiba mpya, bahati mbaya kwa vile nchi inategemea maamuzi ya mtu mmoja. Hilo tusahau kwa sasa.
 
Back
Top Bottom