Mwalimu Nyerere na Tatizo la Udini na Ukabila

Mwalimu Nyerere na Tatizo la Udini na Ukabila

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Hotuba nzuri sana iko hapo chini Mwalimu akionya kuhusu tatizo la udini na ukabila.

Msomaji wangu mmoja kaniletea na kuniomba nimpe fikra zangu kuhusu hii kansa.

Nami nimejitahidi kuliangalia tatizo hili nikipitia historia yake mwenyewe Mwalimu.

Mwalimu Nyerere alipigiwa kura kuwa Rais wa TAA ndani ya ukumbi wa Arnautoglo mwaka wa 1953 na wengi wa waliompigia kura kumchagua walikuwa Waislam.

Kuna video imetengenezwa na TBC1 kuhusu tukio hili la kihistoria nikihojiwa ndani ya ukumbi ule wa Arnautoglo.

Nyerere mwaka wa 1953 hakuwa aliyekuwa anamfahamu.

Alikuwa hajulikani na nafasi hiyo alikuwa anagombea na kijana maarufu wa Dar es Salaam Abdulwahid Sykes aliyekuwa Act. President na Secretary wa TAA.

Halikadhalika alikuwa mmoja wa wafadhili wa TAA pamoja na mdogo wake Ally, Dossa Aziz na John Rupia.

Nyerere alishinda uchaguzi ule.

Uchaguzi huu ndiyo uliobadili historia ya Nyerere.

Nini kimesababisha leo kuwa wananchi wanapiga kura kuchagua viongozi kwa kigezo cha dini na kabila?

Hili swali linahitaji jibu.

Tazama historia ya African Association ilikotoka 1929 hadi kufikia 1954 ilipoundwa TANU.

Tuanze 1954 na turudi nyuma:

Waasisi wa TANU 1954:

1. Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
2. Germano Pacha – Jimbo la Magharibi
3. Joseph Kimalando – Jimbo la Kaskazini
4. Japhet Kirilo – Jimbo la Kaskazini
5. C.O. Milinga – Jimbo la Mashariki
6. Abubakari Ilanga – Jimbo la Ziwa
7. L.B. Makaranga – Jimbo la Ziwa
8. Saadani A. Kandoro – Jimbo la Ziwa
9. Suleman M. Kitwana – Jimbo la Ziwa
10. Kisung’uta Gabara – Jimbo la Ziwa
11. Tewa Said Tewa – Jimbo la Mashariki
12. Dossa A. Aziz – Jimbo la Mashariki
13. Abdulwahid Sykes – Jimbo la Mashariki
14. Patrick Kunambi – Jimbo la Mashariki
15. Joseph K. Bantu – Jimbo la Mashariki
16. Ally Sykes – Jimbo la Mashariki
17. John Rupia – Jimbo la Mashariki

Waasisi wa African Association 1929:

1. Cecil Matola (President)
2. Kleist Sykes (Secretary)
3. Mzee bin Sudi
4. Ibrahim Hamisi
5. Zibe Kidasi
6. Suleiman Majisu
7. Ali Said Mpima
8. Rawson Watts
9. Raikes Kusi

TAA Political Subcommittee 1950:

1. Dr. Vedasto Kyaruzi (President)
2. Abdul Sykes (Secretary)
3. Mufti Sheikh Hassan bin Ameir
4. Sheikh Said Chaurembo
5. Hamza Mwapachu
6. Steven Mhando
7. John Rupia

TAA Executive Committee 1953:

1. J.K. Nyerere (President)
2. Abdulwahid Sykes (Vice-President)
3. J.P. Kasella Bantu (General Secretary)
4. Alexander M. Tobias na Waziri Dossa Aziz (Joint Minuting Secretary)
5. John Rupia (Treasurer)
6. Ally K. Sykes (Assistant Treasurer)
7. Committee Members: Dr Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo na Patrick Aoko.

(Tanganyika Standard 19 June, 1953)

Denis Phombeah alikuwa Mnyasa kutoka Nyasaland, Dome Budohi Mluya kutoka Kenya, C. Ongalo na Patrick Aoko Wajaluo kutoka Kenya.

Hawa Wakristo na wala hawakuwa Watanganyika.

Hawa wamechaguliwa kuwa viongozi katika TAA na waliowapigia kura ni Waislam.

Kitu gani kilitokea kubadili hali hii na kuingiza uhasama na uadui baina ya wananchi kiasi Mwalimu Nyerere anaonya kutokea vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa sababu ya udini na ukabila?

Lakini kwa Tanzania ukabila si tatizo.

Tatizo la Tanzania ni udini.
Hali hii imekujaje?

Nani aliyeleta udini katika siasa Tanzania?


View: https://youtu.be/XgQQoWKh6H0?si=Lw-Jy9ACJHcotbwe
 
sijawahi kuelewa neno “udini“ maana yake nini, binafsi kwa maoni yangu kama wewe ni Mkristo ungependelea kuishi kufwata mafundisho ya kibliblia hauwezi kuishi na waislamu na kinyume chake kama wewe ni muislamu na unataka kuishi kiislamu hauwezi kuishi na wakristo au wahindu ni rahisi kihivyo.

suluhisho ni kuigawa nchi kama kweli lengo ni kuishi kidini kama hilo ni gumu basi hata majimbo ya wanaotaka kuishi kufwata maandiko ya Biblia takatifu majimbo yao na waislamu vivyo hivyo, partition kama india na pakistan, kinyume na hapo tuondoe mambo ya dini na tuseme sisi Godles secular state, binafsi napendelea kuishi kidini na kuseparate …
 
Hotuba nzuri sana iko hapo chini Mwalimu akionya kuhusu tatizo la udini na ukabila.

Msomaji wangu mmoja kaniletea na kuniomba nimpe fikra zangu kuhusu hii kansa.

Nami nimejitahidi kuliangalia tatizo hili nikipitia historia yake mwenyewe Mwalimu.

Mwalimu Nyerere alipigiwa kura kuwa Rais wa TAA ndani ya ukumbi wa Arnautoglo mwaka wa 1953 na wengi wa waliompigia kura kumchagua walikuwa Waislam.

Kuna video imetengenezwa na TBC1 kuhusu tukio hili la kihistoria nikihojiwa ndani ya ukumbi ule wa Arnautoglo.

Nyerere mwaka wa 1953 hakuwa aliyekuwa anamfahamu.

Alikuwa hajulikani na nafasi hiyo alikuwa anagombea na kijana maarufu wa Dar es Salaam Abdulwahid Sykes aliyekuwa Act. President na Secretary wa TAA.

Halikadhalika alikuwa mmoja wa wafadhili wa TAA pamoja na mdogo wake Ally, Dossa Aziz na John Rupia.

Nyerere alishinda uchaguzi ule.

Uchaguzi huu ndiyo uliobadili historia ya Nyerere.

Nini kimesababisha leo kuwa wananchi wanapiga kura kuchagua viongozi kwa kigezo cha dini na kabila?

Hili swali linahitaji jibu.

Tazama historia ya African Association ilikotoka 1929 hadi kufikia 1954 ilipoundwa TANU.

Tuanze 1954 na turudi nyuma:

Waasisi wa TANU 1954:

1. Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
2. Germano Pacha – Jimbo la Magharibi
3. Joseph Kimalando – Jimbo la Kaskazini
4. Japhet Kirilo – Jimbo la Kaskazini
5. C.O. Milinga – Jimbo la Mashariki
6. Abubakari Ilanga – Jimbo la Ziwa
7. L.B. Makaranga – Jimbo la Ziwa
8. Saadani A. Kandoro – Jimbo la Ziwa
9. Suleman M. Kitwana – Jimbo la Ziwa
10. Kisung’uta Gabara – Jimbo la Ziwa
11. Tewa Said Tewa – Jimbo la Mashariki
12. Dossa A. Aziz – Jimbo la Mashariki
13. Abdulwahid Sykes – Jimbo la Mashariki
14. Patrick Kunambi – Jimbo la Mashariki
15. Joseph K. Bantu – Jimbo la Mashariki
16. Ally Sykes – Jimbo la Mashariki
17. John Rupia – Jimbo la Mashariki

Waasisi wa African Association 1929:

1. Cecil Matola (President)
2. Kleist Sykes (Secretary)
3. Mzee bin Sudi
4. Ibrahim Hamisi
5. Zibe Kidasi
6. Suleiman Majisu
7. Ali Said Mpima
8. Rawson Watts
9. Raikes Kusi

TAA Political Subcommittee 1950:

1. Dr. Vedasto Kyaruzi (President)
2. Abdul Sykes (Secretary)
3. Mufti Sheikh Hassan bin Ameir
4. Sheikh Said Chaurembo
5. Hamza Mwapachu
6. Steven Mhando
7. John Rupia

TAA Executive Committee 1953:

1. J.K. Nyerere (President)
2. Abdulwahid Sykes (Vice-President)
3. J.P. Kasella Bantu (General Secretary)
4. Alexander M. Tobias na Waziri Dossa Aziz (Joint Minuting Secretary)
5. John Rupia (Treasurer)
6. Ally K. Sykes (Assistant Treasurer)
7. Committee Members: Dr Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo na Patrick Aoko.

(Tanganyika Standard 19 June, 1953)

Denis Phombeah alikuwa Mnyasa kutoka Nyasaland, Dome Budohi Mluya kutoka Kenya, C. Ongalo na Patrick Aoko Wajaluo kutoka Kenya.

Hawa Wakristo na wala hawakuwa Watanganyika.

Hawa wamechaguliwa kuwa viongozi katika TAA na waliowapigia kura ni Waislam.

Kitu gani kilitokea kubadili hali hii na kuingiza uhasama na uadui baina ya wananchi kiasi Mwalimu Nyerere anaonya kutokea vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa sababu ya udini na ukabila?

Lakini kwa Tanzania ukabila si tatizo.

Tatizo la Tanzania ni udini.
Hali hii imekujaje?

Nani aliyeleta udini katika siasa Tanzania?


View: https://youtu.be/XgQQoWKh6H0?si=Lw-Jy9ACJHcotbwe

Mkuu kwani kuna tatizo umeliona sehemu? Mbona tunaishi kwa amani kabisa? Tuelezee kidogo labda kuna sehemu umetuacha njiani
 
Mkuu kwani kuna tatizo umeliona sehemu? Mbona tunaishi kwa amani kabisa? Tuelezee kidogo labda kuna sehemu umetuacha njiani
Paddy,
Hakuna tatizo.

Nimekumbuka mengi katika historia ya vipi Mwalimu alivyopokelewa Dar es Salaam 1952 na hakutazama nyuma.

Mwalimu akawa kiongozi mkubwa Afrika.

Nikajiuliza ingekuwaje wale waliompokea wangekuwa wana udini na ukabila kama watu hawa anaowaeleza katika hotuba yake?
 
Aisee haya mambo haya, ni nani basi alikua nyuma ya mwalimu.??

Je waliompa nafasi hawakuweza kumpoka pale walipoona ndivyo sivyo??
 
sijawahi kuelewa neno “udini“ maana yake nini, binafsi kwa maoni yangu kama wewe ni Mkristo ungependelea kuishi kufwata mafundisho ya kibliblia hauwezi kuishi na waislamu na kinyume chake kama wewe ni muislamu na unataka kuishi kiislamu hauwezi kuishi na wakristo au wahindu ni rahisi kihivyo.

suluhisho ni kuigawa nchi kama kweli lengo ni kuishi kidini kama hilo ni gumu basi hata majimbo ya wanaotaka kuishi kufwata maandiko ya Biblia takatifu majimbo yao na waislamu vivyo hivyo, partition kama india na pakistan, kinyume na hapo tuondoe mambo ya dini na tuseme sisi Godles secular state, binafsi napendelea kuishi kidini na kuseparate …
Kuna option ya kuhamia nchi inayofata mlengo wa dini moja. Nayo option nzuri pia.
 
Msiwe wanafiki wengi wenu mna Udini uliopitiliza, nakumbuka kuna mtu alikuja na uzi unaongelea kuhusu maelezo ya dkt. Kijaji kuna mwamba akatililika na "hili ni tatizo la elimu ya madrasa" na wengine wakaunga mkono hoja, na nimeona kwenye nyuzi nyingi sana watu wakitoa povu with no reason kama ile ya mufti wa Oman kupongeza serikali kupinga ushoga wengi waliikana serikali kuwa haijachukua hatua yoyote ile ila huyo mufti eti ana kihelehele walijisahaulisha kuwa ni mawiki kadhaa nyuma bunge lilipitisha sheria ya kifungo cha miaka 30 jela kwa yeyote atakayejihusisha na vitendo hivyo, nisimalize maneno.....
 
Back
Top Bottom