Mwalimu Nyerere vs Thabita Siwale

Mwalimu Nyerere vs Thabita Siwale

Hii habari sijaisikia. Maoni yangu ni kwamba walimu wanaowabughudhi watoto wa viongozi,I hate them with perfect hatred. Hao watoto wa Wabunge,watoto wa Katibu Kata,mimi kaka yao. Tabia ya kuwaita vibaka,walevi,teja,na kuwafanyia fujo,ikomeshwe mara moja. I ask that they should be left in peace.

sijawahi muona huyu andrew, lakini mara nyingi posts zake zinakuwa na walakini. I think smth is missing upstairs.
 
Wapi Andrew Nyerere atupe version yake?

Wanyakyusa sio watu wakubembeleza bembeleza, Ambangile Mwambungu nae kama Thabitha Mwambenja Siwale alimfukuza shule Andrew Nyerere toka Mkwawa!! Nyerere kama alivyomteua Kamuzora kuwa RDD nae Mwambungu akateuliwa kuwa RDD!! Chezea wanyakyusa wewe hata baba MwanaAsha anajua jeuri yao!!
 
Hii habari sijaisikia. Hili jambo naona ni distraction.Huyu Thabita Siwale sikuifuatilia sana career yake. I was too youmg at that time to be preoccupied with politics. Halafu hakuna mtoto wa Mwalimu ambaye amesoma Tabora.
Maoni yangu ni kwamba walimu wanaowabughudhi watoto wa viongozi,I hate them with perfect hatred. Hao watoto wa Wabunge,watoto wa Katibu Kata,mimi kaka yao. Tabia ya kuwaita vibaka,walevi,teja,na kuwafanyia fujo,ikomeshwe mara moja. I ask that they should be left in peace.

Makongoro Nyerere alisoma Tabora Boys mpaka anaenda jeshini.
 
Wanyakyusa sio watu wakubembeleza bembeleza, Ambangile Mwambungu nae kama Thabitha Mwambenja Siwale alimfukuza shule Andrew Nyerere toka Mkwawa!! Nyerere kama alivyomteua Kamuzora kuwa RDD nae Mwambungu akateuliwa kuwa RDD!! Chezea wanyakyusa wewe hata baba MwanaAsha anajua jeuri yao!!

Andrew nyerere amejibu hapo juu ila hakusema kama yeye ndie aliyefukuzwa labda atakuja kueleza hapa kama yeye ndie aliyefuzwa.
 
Last edited by a moderator:
Wadau wa historia habari zenu? naombeni msaada kuna habari nimewahi kuisikia zamani kidogo inamhusu Mwalimu Nyerere kipindi hicho akiwa Rais wa Tz na mwanasiasa mkongwe Bi Thabita Siwale waziri wa zamani wa elimu na utamaduni!

Hbr yenyewe ipo hivi huyu bi Thabita Siwale chanzo cha yeye kuteuliwa na Mwalimu Nyerere kuwa Waziri wa Elimu miaka hiyo ni ujasiri wa kipekee aliounyesha akiwa mkuu wa shule sekondari maarufu mkoani Tabora(jina nimelisahau) kwa kuumpa adhabu ya kurudi nyumbani kwa muda(sunspension)mtoto Mwalimu Nyerere aliyekuwa akisoma katika shule hiyo na kumuamuru siku ya kurudi shule aje na mzazi wake ili hali akijua kabisa mzazi wake ni rais wa nchi mwalimu Nyerere!

Aidha inasemekana baada ya kumpa adhabu hiyo watu wengi walianza kumtisha Bi Thabita kuwa atafukuzwa kazi kwa kumrudisha nyumbani mtoto wa Rais.

Baada ya adhabu kwisha yule mtoto alirudi shuleni akiwa na mzazi wake kama alivyoamriwa katika barua aliyopewa wakati wakurudishwa nyumbani Walimu na hata Bi Tabitha walistaajabu walipomwona yule mtoto kaja na Mwalimu Nyerere,wenyewe walimu na Bi Tabitha walitegemea mwalimu Nyerere angemtuma mwakilishi kutokana majukumu na hadhi yake ya urais wa nchi.

Baada ya kumwona Nyerere inasemekana mama Tabitha na staff nzima walichanganyikiwa wakajua sasa mwisho wao ndiyo umefika wa kufukuzwa kazi,lkn mwalimu Nyerere aliwatoa wasiwasi na kuwambia wasiwe na hofu yoyote yeye pale hajaja kama Rais wa nchi bali amekuja kama mzazi wa mtoto,baada ya hapo kengele ya paredi ikangongwa wanafunzi wakakusanyika wote yakaelezwa yale makosa ya mtoto wa Nyerere akaamriwa kuchapwa viboko na mwisho wa siku akaruhusiwa kuendelea na masomo,mwalimu Nyerere akarudi zake Dar es Salam.

Nasikia baada ya muda BiThabita badala ya kufukuzwa kazi akateuliwa kuwa waziri elimu kwa ushujaa aliounyesha!Maswali ya kujiuliza je kwa sasa hivi ni mkuu gani wa shule anaweza kumfukuza mtoto wa rais Shule achilia mbali watoto wa wabunge,mkuu wa wilaya au mkoa,waziri au hata wakurugenzi tu?

Kwa hakika Bi thabita alionyesha ushujaa wa hali ya juu sana!Kwa kizazi cha sasa tuna hitaji aina ya viongozi km Bi Tabitha Siwale ambao wanaweza kufanya maamuzi magumu bila kujali hadhi ya mtu!

Siyo kweli; mama Tabitha alipandishwa kutokana na ujasiri wa kumshitaki Chediel Mgonja aliyekuwa Waziri wa Elimu wakati huo ila akawa anafanya umalaya na wanafunzi wa kike, mmoja wa wanafunzi waliokuwa wakifanya ufuska na Mgonja alikuwa mwanafunzi wa Korogwe Girls ambako Tabitha alikuwa Headmistress. Hivyo Tabitha akamfuata Mwalimu pale Magogoni akiwa na makbarasha ya ushahidi dhidi ya Mgonja ka kumpa makavu makavu Nyerere kuhusu waziri wake huyo; huku akimtaka akome kuvurugia wanafunzi wake. Ndipo Mwalimu alifurahia ujasiri wa mama yule, akamfuta Mgonja Uwaziri wa Elimu mara moja na kumpa nafasi hiyo mama Tabitha.
 
Roho mbaya ya huyu mama ni ya asili. Aliwahi kuropoka amri mwaka 1982 wakati akiwa waziri. Alisema eti seminary si secondary za kawaida hivyo alizuia wote waliomaliza f 4 seminary wasiendelee f5 kwenye shule za serikari na watu wakaumizwa kirahisi . Wkt huo shule zilikuwa chache ajabu hasa high school. Mama huyu nikimwona nitamani nimwadhibu. Nyambaf
 
Roho mbaya ya huyu mama ni ya asili. Aliwahi kuropoka amri mwaka 1982 wakati akiwa waziri. Alisema eti seminary si secondary za kawaida hivyo alizuia wote waliomaliza f 4 seminary wasiendelee f5 kwenye shule za serikari na watu wakaumizwa kirahisi . Wkt huo shule zilikuwa chache ajabu hasa high school. Mama huyu nikimwona nitamani nimwadhibu. Nyambaf
Hao wa kutoka seminarini walienda wapi baada ya kumaliza kidato cha nne.
 
Alikuwa headmistress Korogwe Girls na sio Tabora. Her political stardom started with the then infamous Chediel Mgonja flinging with school girls.........I will end here for now!

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/23748-waziri-wa-zamani-chadiel-mgonja-afariki-print.html
 
Mmmghhh Heri yangu mimi ambaye sijasikia chochote.... Better shut up
 
Mkuu hao waliomaliza f4 walilazimika kwenda kubanana kwenye high school chache za seminary hata km hawakutaka, wengine walijiunga na shule za binafsi ila kuna wengi walilazimika kutafuta vyuo mbalimbali.
Ila yote hayo sbb ya wakubwa km huyu mama wameropoka. Too sad.
 
Siyo kweli; mama Tabitha alipandishwa kutokana na ujasiri wa kumshitaki Chediel Mgonja aliyekuwa Waziri wa Elimu wakati huo ila akawa anafanya umalaya na wanafunzi wa kike, mmoja wa wanafunzi waliokuwa wakifanya ufuska na Mgonja alikuwa mwanafunzi wa Korogwe Girls ambako Tabitha alikuwa Headmistress. Hivyo Tabitha akamfuata Mwalimu pale Magogoni akiwa na makbarasha ya ushahidi dhidi ya Mgonja ka kumpa makavu makavu Nyerere kuhusu waziri wake huyo; huku akimtaka akome kuvurugia wanafunzi wake. Ndipo Mwalimu alifurahia ujasiri wa mama yule, akamfuta Mgonja Uwaziri wa Elimu mara moja na kumpa nafasi hiyo mama Tabitha.

lakini Chedieli Mgonja alikuwa waziri wa elimu 1971/1974, na aliyempokea wizara hiyo ni Simon Chiwanga. kwa hiyo inaelekea Mgonja aliondoka wizara ya elimu kwa sababu nyingine na siyo "kuchongewa" na Siwale kama unavyosema.

marehemu Chediel Mgonja "kaghembe" ni mhanga wa siasa za maji taka. wanasiasa wenye chuki toka north pare ndiyo waliokuwa wakimfanyia vituko na kumzushia kila aina ya uongo. mgogoro wa kisiasa dhidi ya Mgonja ulidhoofisha maendeleo ya wilaya ya Pare na kusababisha utengano baina ya jamii moja, kabila moja.

Mgogoro huo ulioanzishwa na wanasiasa wa north pare ambao walikuwa hawawezi kupambana na Mgonja katika medani ya siasa ndiyo umeendelea mpaka ukahamia kwenye Dayosisi ya Pare ya KKKT.

hivi inaingia akilini Mgonja awe anazini na wanafunzi halafu Mwalimu Nyerere aendelee kumteua katika baraza la mawaziri. Tena amwamini kiasi cha kumteua mkuu wa mkoa wa Mtwara wakati vita vya ukombozi wa Msumbiji vimepamba moto?

The Fixer, Dingswayo, [MENTION=215045]Queen Esther, Naghenjwa, tenanzinyo, MASHANJARA
 
Last edited by a moderator:
lakini Chedieli Mgonja alikuwa waziri wa elimu 1971/1974, na aliyempokea wizara hiyo ni Simon Chiwanga. kwa hiyo inaelekea Mgonja aliondoka wizara ya elimu kwa sababu nyingine na siyo "kuchongewa" na Siwale kama unavyosema.

marehemu Chediel Mgonja "kaghembe" ni mhanga wa siasa za maji taka. wanasiasa wenye chuki toka north pare ndiyo waliokuwa wakimfanyia vituko na kumzushia kila aina ya uongo. mgogoro wa kisiasa dhidi ya Mgonja ulidhoofisha maendeleo ya wilaya ya Pare na kusababisha utengano baina ya jamii moja, kabila moja.

Mgogoro huo ulioanzishwa na wanasiasa wa north pare ambao walikuwa hawawezi kupambana na Mgonja katika medani ya siasa ndiyo umeendelea mpaka ukahamia kwenye Dayosisi ya Pare ya KKKT.

hivi inaingia akilini Mgonja awe anazini na wanafunzi halafu Mwalimu Nyerere aendelee kumteua katika baraza la mawaziri. Tena amwamini kiasi cha kumteua mkuu wa mkoa wa Mtwara wakati vita vya ukombozi wa Msumbiji vimepamba moto?

The Fixer, Dingswayo, Queen Esther, Naghenjwa, tenanzinyo, MASHANJARA

Ni kweli, nami niliandika kwa lugha ya mkato tu. Nyerere alikuwa na tabia fulani ambayo labda itasaidia kujua kwa nini Mgonja aliendelea kwenye siasa. Alikuwa mgumu sana wa kufukuza watu wake kwa hiyo alikuwa akiwahamisha kutoka sehemu moja kwenda nyingie; Mgonja alikuwa ni mmoja wa watu wa Nyerere; alikuwa mchapakazi mzuri sana inapokuwa utendaji, ila personal behavior yake tumekuwa tunaiskia kwa watu tu. Mashitaka ya Siwale dhidi ya Mgonja ndiyo yaliyopelekea Mgonja kutolewa Wizara ya Elimu na kufanwa kuwa mkuu wa Mkoa wa Mtwara ingawa yule mama hakufanywa kuwa Waziri wa Elimu mara moja bali alifanywa waziri wa Nyumba ambayo nadhani pia ilikuwa pia na jukumu la kusimamia mambo ya wanaweke na watoto. Politics za upareni za wakati huo sizifahamu. Friction hiyo baina ya Mgonja na Siwale haikuwa publicized kwenye media bali ilipatikana kutoka kwa watu waliokuwa wakiijua kwa kina, hasa waalimu wa Korogwe Girls; kama unamjua mwalimu mmoja wapo wa Korogwe ghirls wakati huo jaribu kufuatilia.
 
Mkuu suala hapa siyo tu ujasiri was with pia unaangalia na viongozi wenyewe kwan sidhan kamakunakiongozi ambaye ataweza kustahimili aliyostahimili Mwalimu Nyerere.
 
je kwa sasa hivi ni mkuu gani wa shule anaweza kumfukuza mtoto wa rais.?

Jibu ni kwamba hakuna rais au waziri atakae wasomesha watoto wake tanzania..
 
Sawa kabisa ebaeban! Tabitha alipewa uwaziri kwa sababu ya ujasuri wake. Si unajua yule ni Mnyakyusa?

Ila alikija kukosana na Nyerere baada Tabitha kuanza kumdharau mumewe. Kwa vile tu alikuwa waziri!

Safi sana Mwalimu. Siyo hawa kina Pindi Chana ambao ndoa zimewashinda kisa madaraka.
 
Back
Top Bottom