The Red Pen
JF-Expert Member
- Sep 26, 2014
- 517
- 206
Mi nasema; Hakuna tatizo kwa mwalim wa Book-keeping kwend sahihisha Geography. Kule kuna tayari mfumo unaofanana wa kusahihishia. Haendi kufundisha Geography bali kusahihisha. Kwanza maswali yenyewe ni hayo ya kujaza abc?? Kwani anaenda kusahihisha ya kujieleza? Acheni za kuleta, mwache mwalim mkuu naye ajiinue nyiye mmheshimu. Atapata wapi heshima yake kwenu waalim anao waongoza?? Ukimnyenyekea kama boss wako wengine wanasema anatunyanyasa yaani Tz kila kitu siasa
Sielewi mtindo wa TZ, sana. Ikiwa ni mambo ya ABCD, basi hapo hamna shida. Lakini ikiwa ni mengine, basi hapo kuna shida. Tatizo hilo usilaumu mwalimu, bali laumu NECTA yenyewe. Waje huku Kenya wajifunze jambo kutoka kwa KNEC.
Nilipokuwa mwanafunzi kidato cha nne, yule anayesahihisha Geography Paper 1 (Physical Geography,) hakuwa anasahihisha Geography paper 2 (Human Geography.) Hii ni kwasababu paper 1 na paper 2 yalitofautiana sana. Kiingereza na Kiswahili, Paper 1 (Insha na Lugha) na Paper 2 (Fasihi) zilikuwa na sheria tufauti sana, na yule aliyekuwa amezoa kumark Paper 1, angeona tatizo kumark paper 2.
Ninashangazwa na yule anayesema kuwa eti mwalimu wa fizikia anaweza kusahihisha mtihani wa Jiographia. Labda iwe ni ule mchezo tunaoita "cha baba na mama." Kabla walimu kuanza kusahihisha, ilibidi waufanye mtihani huo huo, na apate zaidi ya 60%. Baada ya hapo, waufanye mtihani huo kama mara mbili hivi, mkijadiliana njia zote zile mwanafunzi anaweza kuwa amelielewa lile swali, an ni wapi mtihani huo unaweza kuwa hujaeleweka vizuri. Baada ya hapo, mnaiunda marking scheme vizuri zaidi na kutunga sheria mpya kwa huo mtihani pekee, kulingana na yale matatizo ambayo hao examiners wameona. Kwa mfano, mtihani wa Paper hisabati mwaka wa 1999, ulikuwa mgumu hadi examiners wakaambiwa wa mark hadi cancelled work. Kama umefanya, kisha ukachora msitari, na ukaandika vibaya, examiners wanakubaliwa kusahihisha ile kazi mbovu. Walimu hawa walikuwa wanasajiliwa na KNEC wenyewe, bali sio mwalimu mkuu wa shule.
Baada ya hapo, wanapelekwa mafunzo, jinsi ya kudetect irregularity na mambo mengine. Mtu huendelea hapo akizidi kupandishwa madaraka. Ukishakuwa examiner kwa mda mrefu, basi unapandishwa cheo na kuwa "team leader." Baada ya hapo unakuwa Senior examiner (Kama ni History paper 1, basi ni senior examiner, History paper 1,) Baada ya hapo ukifanikiwa, basi unazidi kupanda madaraka hadi unakuwa Chief Examiner. Hakuna vile basi unaweza kuja kupewe kazi ambayo hujasomea, na hata hujafundisha. Utaelewaje matatizo yanayowakumba wanafunzi ikiwa hujawahi kuwafundisha na kusahihisha vitabu vyao?
Ni kweli kabisa mkuu.Kuna rafiki yangu mmoja anafundisha shule "X" ya Private jijini Dar alinidokeza kuwa yaani ile shule ni Vituko vya Mkuu wa shule na makamu wake. Barua ilikuja ikiwa inamtaka ateue walimu wasiopungua Watano kwenda kusimamia mtihani wa kidato cha NNE.Lakini cha kushangaza MKUU WA SHULE AKAMTEUA MAKAM WAKE TU akaenda kusimamia. Makamu ametoka huko akaunganisha kusimamia NECTA F2.Makam huyo huyo ametoka kusimamia NECTA F2 akaunganisha kwenda kusahihisha NECTA F2 kwa Ticketi ya Somo la kiingereza huku yeye akiwa siyo mwalimu wa hilo somo na wala hafundishi somo lolote kidato cha Pili.Huku mwalimu wa hilo somo akiachwa solemba.Baraza wanatumia marker walewale miaka nenda rudi, sio utaratibu mzuri sana. Nashauri baraza wawaumie tu wakuu wa shule na data base yao kujua nani anafaa lkn sio kila mwaka mtu huyohuyo, kusimamia huyohuyo, necta form 4 huyohuyo necta form 2 huyohuyo necta form 6 huyo, ni upuuzi mkubwa kabisa. kibaya zaidi necta haijui utegaji wa mtu katika kazi za kishule, wanawapa viburi marker wa aina hii.
markers wanaochagliwa haohao kila mwaka wanasababisha kusimama kazi nyingi sana. Hivi hawo marker hawafunsihi masimo yanayohitaji kusahihishwa mwisho wa mwaka? hivi wanajua huyo mtu wanaemuita anatulia kazini? Tabia za wanaojiita maacordinato kupigia simu ndio wanaharibu kabisa.
kule kule marking unashangaa mtu ameitwa.
Kule kule marking anafundishana stail za ajabu kabisa namna ya ushaihishaji, yaani ni upuuzi mtupu.
Wewe mleta mada ni muongo Necta wenyewe ndo wanachagua, anachofanya mkuu wa Shule ni kujaza form kila mwaka ya Walimu walioko kituoni... Mwaka wa kuanza kwzi, TSD no na masomo yanayofundishwa kazi ya Baraza ni kuchagua ingawa pia comment za mkuu zibaanfaliwa
Labda ungesema mitihani inayosimamiwa na TAHOSSA labda ila Necta Mkuu wa shule hahusiki
Na uyo wa somo la geography akasahahishe Book keeping si ndio? Tatizo lipo hapo.Mi nasema; Hakuna tatizo kwa mwalim wa Book-keeping kwend sahihisha Geography. Kule kuna tayari mfumo unaofanana wa kusahihishia. Haendi kufundisha Geography bali kusahihisha. Kwanza maswali yenyewe ni hayo ya kujaza abc?? Kwani anaenda kusahihisha ya kujieleza? Acheni za kuleta, mwache mwalim mkuu naye ajiinue nyiye mmheshimu. Atapata wapi heshima yake kwenu waalim anao waongoza?? Ukimnyenyekea kama boss wako wengine wanasema anatunyanyasa yaani Tz kila kitu siasa