Mwalimu wa St. Doroth (Tabora) ashtakiwa kwa kumnajisi Mwanafunzi wa Darasa la Pili

Mwalimu wa St. Doroth (Tabora) ashtakiwa kwa kumnajisi Mwanafunzi wa Darasa la Pili

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
TABORA - MWALIMU Dotto Elias (29) wa Shule ya mchepuo wa Kiingeza ya Mtakatifu Doroth iliyopo maeneo ya kidatu Manispaa ya Tabora anayedaiwa kumnajisi mwanafunzi wa darasa la pili chooni amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Tabora.

Akisoma mashtaka hayo jana Agosti 15, 2024, Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mwanasheria wa Serikali, Charles Magonza aliiambia mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, John Mdoe kuwa mtuhumiwa alikuwa akimnajisi mtoto huyo (jina limehifadhiwa) chooni kipindi cha kunywa uji.

Soma Pia: Mwalimu Mkuu adaiwa kumlawiti mwanafunzi Bunda

Alidai Julai 26, 2024 kati ya saa 1 na saa 2 usiku bibi wa mtoto huyo alibaini mtoto huyo kufanyiwa vitendo vya unajisi baada ya kumkagua na kuona alivyoharibiwa.

Alisema kwa mujibu wa Sheria ya Makosa ya Adhabu Sura ya 16 marejeo ya Mwaka 2022 Kifungu cha 154 Sura Ndogo ya 15 ya Makosa ya Utu, mtu atakayemwingilia mwenzake kinyume cha maumbile kwa lazima ama kwa kutaka mwenyewe adhabu yake/zao wote ni kifungo cha maisha gerezani au kifungo cha miaka 30 jela.

Mshtakiwa Elias baada ya kusomewa mashitaka yake alikana kutenda kosa hilo kwa mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka saba.

Chanzo: Habari Leo
 
Mkuu wa Mkoa kamwambia mzazi mwenye majonzi "haya yatakwisha." Mtoto ambae kaachiwa kovu la maisha physically na psychologically. Yatakwisha kivipi, kwa kumshona sphincters ?

Halafu kaamuru mwananchi anaewashawishi familia wakae chini wayamalize akamatwe na polisi! Sijui kwa kesi gani

Na sielewi kwa nini wilayani na mkoani huwa hakuna mwendesha mashtaka aliyesomea sheria, na mwenye mamlaka ya kufungua kesi ya jinai, kuwatua mzigo hawa kina "Mwenyeviti wa Ulinzi na Usalama" ambao kwenye sheria ni ma dunderhead
 
Back
Top Bottom