Mwamakula: Naweka mkakati upya ulioboreshwa zaidi kisha nitautangaza kwa Watanzania

Mwamakula: Naweka mkakati upya ulioboreshwa zaidi kisha nitautangaza kwa Watanzania

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Askofu wa Kanisa la Uamsho la Moravian, Emmaus Mwamakula amesema anatafakari na kuweka mkakati upya ulioboreshwa zaidi kisha atautangaza kwa Watanzania.

Februari 15, 2021. Mwamakula alikamatwa na polisi kwa madai ya kuhamasisha maandamano ya kudai tume huru na Katiba Mpya kwa njia ya mtandao lakini alikamatwa na kuwekwa rumande kwa siku moja.

Akizungumza na waandishi wa habari Jumatano Februari 17, 2021 nyumbani kwake Kimara jijini Dar es Salaam amesema mwishoni mwaka 2020 aliutangazia umma kusudio lake la kuongoza matembezi ya hiari nchi nzima lengo likiwa kuhamasisha upatikanaji wa Katiba Mpya na tume huru ya uchaguzi.

Amebainisha kuwa azma ya kuongoza matembezi hayo ilichangiwa na sababu kadhaa ikiwemo uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 baada ya kuzunguka nchi nzima na aliyekuwa mgombea urais wa Chadema, Tundu Lissu.

“Nilizunguka bara na visiwani pamoja na mambo mengine nilijionea na kushuhudia jinsi mchakato mzima wa uchaguzi ulivyoathiriwa na vitendo vya ukiukwaji na upendeleo wa wazi.”

“Vitendo hivyo ni pamoja na kuwaengua kwa kiasi kikubwa wagombea wa vyama vya upinzani katika nafasi za udiwani, uwakilishi na ubunge,” amedai.

Amesema mwanzoni mwa Februari, 2021 alitangaza kuzindua matembezi ya hiari jijini Dar es Salaam kuanzia Februari 16, 2021.

“Nilielekeza wazi kuwa watu watatembea katika makundi ya watu 10 hadi 20 na kwamba kutakuwa na umbali usiopungua mita 100 kati ya kundi na kundi na kwamba matembezi hayo yataelekezwa katika ofisi yoyote ya umma,” alieleza akibainisha kuwa nia yake hiyo ilizimwa baada ya kukamatwa na kupelekwa kituo cha polisi Oysterbay.

Amesema licha ya kutofanikiwa kuandaa matembezi hayo lakini kuzuiwa kwake kumesaidia uzinduzi wa kampeni zenyewe.

Chanzo: Mwananchi
 
Tungekuwa na Maaskofu walau 10 tu kama huyu Mwamakula, hakika Taifa letu lisingetawaliwa na duhuluma, ubabe, ukatili, ubinafsi, uonevu, ukabila na kila aina ya madudu.

Hongera sana Askofu Mwamakula. Mamilioni ya Watanzania wapenda Mabadiliko ya kweli, tuko nyuma yako.
 
Nakuunga mkono askofu sema shida ya watanzania sio watu wa kuwapa dhamana hawakawii kuku snitch watz sio watu wa kuaminika unless kama umeamua kusimama wew kama wew watz sio watu wa kutegemewa katika mapambano
 
Askofu nimekusikikiza jana, hakika Roho wa Mungu yu ndani yako. Uliukizwa maswali mengine, mengine ilikuwa vigumu kutabiri utajibu namna gani, lakini kila jibu ulilotoa lilijaa hekima kubwa ndani yake.

Yawezekana hatuna ujasiri kama wa Askofu, lakini tuna wajibu wa kuunga mkono jitihada za Askofu, siyo kwa faida ya Askofu bali kwaajili yetu, vizazi vijavyo, na kwaajili ya utukufu wa Mungu aliyetupatia nchi hii ili pawe mahali pema na furaha kwa watu wote.
 
Hivi kweli hayo matembezi yana ulazima kweli katika kipindi hiki ambapo watu wanakufa na hizi pneumonia? kwanini wakati huu tusitumia kuitaka serikali itueleze ukweli ni nini kinaendelea kwenye hivi vifo vinavyoendelea kutokea?
 
Hivi kweli hayo matembezi yana ulazima kweli katika kipindi hiki ambapo watu wanakufa na hizi pneumonia? kwanini wakati tusitumia kuitaka serikali itueleze ukweli ni nini kinaendelea kwenye hivi vifo vinavyoendelea kutokea?
Askofu kachagua katiba. Wewe chagua tatizo lililopo. Huoni tutakuwa tumepiga ndege wawili kwa jiwe moja?

Labda useme unataka kumtuma askofu halafu wewe ujifiche nyuma ya keyboard
 
Askofu kachagua katiba. Wewe chagua tatizo lililopo. Huoni tutakuwa tumepiga ndege wawili kwa jiwe moja?

Labda useme unataka kumtuma askofu halafu wewe ujifiche nyuma ya keyboard
Ndio nimeuliza kuna ulazima wa hilo la kufanya matembezi kudai katiba katika hali tuliyopo ambapo watu wanakufa na matatizo ya kushindwa kupumua na tunazika watu kila siku?
 
Back
Top Bottom