Mwamba wa Hiphop halisi, Saigon 'Treach' wa iliyokuwa D.P.T ana masahibu gani hivi?

Mwamba wa Hiphop halisi, Saigon 'Treach' wa iliyokuwa D.P.T ana masahibu gani hivi?

Wsimjui KBS

Naona malegend mnashuka tu Maelezo yake

Huyo ni nguli wa kitambo na hakuwahi kuchuja. walikuwa crew yao ikiitwa Diplomatz likitamkwa Tha De-Plow-Matz (DPT) lilikuwa kundi la muziki wa hip hop lililotamba sana katika miaka ya tisini. Kundi linaundwa na Saigon (Saleeh Mzee), balozi Dolasoul (Ahmed Dola), Trip Dogg (Philip Mwinmanji) na Storm (Amour Shamte) na meneja wao Nkwessa. Awali nyimbo zao walikuwa wanaimba Kiingereza tu. Baadaye wakawa wanaimba Kiswahili huku wakitia maneno ya Kiingereza katika mistari yao.
 
Nimekaa na Saigon mwaka jana kati kati, nilichogundua jamaa hana Kichwa kizuri cha kunywa kilevi (Double Kick) analewa sana hadi anaanza kugombana na watu, ni basi tu tunamuheshimu na tunajua sio akili yake ndo tunamkimbia kuepesha Shari.

Ila kwa jicho la tatu ni mtu mwenye majuto na stress za hatari sana, na pia kuna kiashiria kwa mbali kwamba pombe haimtaki, haiwezi (Kichwa Panzi) kwani akiacha pombe tu anakua mtu Poa sana.

Pia miaka ile ya nyuma kipindi cha EATV 2007-09 aliachishwa Kazi kwa sababu tu ya pombe akinywa akili zinaruka anaanza kuzingua ile isiyovumilika kabisa.

Namuombea Mwenyezi Mungu ampe tena nafasi nyingine ya kujirudi na kuachana na vyote vinavyomshinda na kumptezea nguvu, maarifa na Heshima yake.

Bado tunamdai vingi kwenye game letu la hip hop...
 
Nimekaa na Saigon mwaka jana kati kati, nilichogundua jamaa hana Kichwa kizuri cha kunywa kilevi (Double Kick) analewa sana hadi anaanza kugombana na watu, ni basi tu tunamuheshimu na tunajua sio akili yake ndo tunamkimbia kuepesha Shari.

Ila kwa jicho la tatu ni mtu mwenye majuto na stress za hatari sana, na pia kuna kiashiria kwa mbali kwamba pombe haimtaki, haiwezi (Kichwa Panzi) kwani akiacha pombe tu anakua mtu Poa sana.

Pia miaka ile ya nyuma kipindi cha EATV 2007-09 aliachishwa Kazi kwa sababu tu ya pombe akinywa akili zinaruka anaanza kuzingua ile isiyovumilika kabisa.

Namuombea Mwenyezi Mungu ampe tena nafasi nyingine ya kujirudi na kuachana na vyote vinavyomshinda na kumptezea nguvu, maarifa na Heshima yake.

Bado tunamdai vingi kwenye game letu la hip hop...
Sana aisee mi sio mhenga ila hawa jama walinifanya niipende sana hiphop na makundi kama kwanza na zavara wao.
 
Huyo ni nguli wa kitambo na hakuwahi kuchuja. walikuwa crew yao ikiitwa Diplomatz likitamkwa Tha De-Plow-Matz (DPT) lilikuwa kundi la muziki wa hip hop lililotamba sana katika miaka ya tisini. Kundi linaundwa na Saigon (Saleeh Mzee), balozi Dolasoul (Ahmed Dola), Trip Dogg (Philip Mwinmanji) na Storm (Amour Shamte) na meneja wao Nkwessa. Awali nyimbo zao walikuwa wanaimba Kiingereza tu. Baadaye wakawa wanaimba Kiswahili huku wakitia maneno ya Kiingereza katika mistari yao.
Asante kwa Maelezo mazuri
 
Huyu ni Saleh, almaarufu 'Saigon'.
Mwanachama wa-miongoni mwa makundi ya awali kabisa kuwahi kutamba katika tasnia ya muziki wa Hiphop.
Hapa tunazungumzia mwanzoni kabisa mwa miaka ya 90.

Jamaa alikuwa Mkali kwa kwa maana halisi ya ukali kuanzia katika Tungo na Style yake.
Si hivyo tu Mchizi kunako 'tambo huru', moja ya nguzo muhimu na za lazima za Hiphop, yupo vizuri.

Sanjari na sifa hizo huyu bwana amejaaliwa 'Yai' ambalo ukiwaondoa pengine aliokuwa akifukuzana nao kwa karibu enzi hiz,
watu kama akina Eazy-B au D-Rob wa KU crew, Saigon hakuna wa kufanana nae hadi sasa na pengine hatatokea.

Nilifurahi wakati fulani pale alipoweza kuonyesha kipaji na uwezo wake mwingine katika maswala ya utangazaji hasa kwenye Runinga. Nani hakumbuki kionjo chake kilichotamba cha 'Ebwana Dah!' wakati ule akiwa na EATV?

Nikaja kumuona mara kadhaa akionekana mpenzi wa Kanzu, Bargashia wakati mwingine full-Hagal,
Tofauti na mazoea yake ya uvaaji wa ki-hiphop haswaa, pensi, T-shirt, Boots, Sneaker nk.
Kuuliza naambiwa jamaa sasahivi swala haimpiti. -Nikasema safi.

Mara kapotea, hainekani wala hasikiki tena.

Hoja ya uzi wangu;
Huyu bwana nimemuona wiki ya jana maeneo ya Sinza,
Siha na muonekano kwa kumuangalia tu, -Kuna shida,-Hayuko sawa.

Ndugu, jamaa na marafiki mnaomtakia mema huyu mwamba mtafutena angalieni mnamsaidiaje.

Na kama yupo anaejua anasumbuliwa na nini si mbaya kutumegea.
Dah,
E bwana dah,
E bwana dah,
E bwana oi oi,
Kalinye kalinye episode,
Again,Yaan tena,
 
Sifa za "we mkali mwanangu noma" na [emoji1477] zinawaponza sana vijana, wanajiona wanajua sana halafu hakuna wanachopata.

Kisha huamua kususa na kujifanya maustadhi, huku akili haikubali uhalisia.

Mwingine ni Maalim Nash MC.

Uchebe chaka a.k.a Zuzu. Maalim Nash wa Mitihani.

-Kaveli-
 
Sifa za "we mkali mwanangu noma" na [emoji1477] zinawaponza sana vijana, wanajiona wanajua sana halafu hakuna wanachopata.

Kisha huamua kususa na kujifanya maustadhi, huku akili haikubali uhalisia.

Mwingine ni Maalim Nash MC.
Huyo Nash ni mswahili mno.
 
Sifa za "we mkali mwanangu noma" na [emoji1477] zinawaponza sana vijana, wanajiona wanajua sana halafu hakuna wanachopata.

Kisha huamua kususa na kujifanya maustadhi, huku akili haikubali uhalisia.

Mwingine ni Maalim Nash MC.
Achana na maalim nash anadund kama kawa.
 
Nilipata miito miwili kwa pamoja, ama kwenda milima ya Himalaya kuwa Buddhist monk, ama kwenda Wall Street kwenye mifumo ya mabenki ya dunia.

Nikaamua kwenda Wall St.
Kiranga una link ya hizi ngoma za zamanj za wabongo wanao rap kizungu?
 
E Bwana dah....oooh.oi..oi....banana dah!...nakumbuka mbali sana.
 
Back
Top Bottom