Mwambusi, Yanga ni timu kubwa, kula kwenye VIHOTEL UCHWARA kunakupunguzia heshima yako

Mwambusi, Yanga ni timu kubwa, kula kwenye VIHOTEL UCHWARA kunakupunguzia heshima yako

Mbona lowassa alienda kula kwa mama ntilie wakati yeye alikuwa anagombea nafasi namba moja yenye hadhi nchini URAIS ... Hahaha sipo serious sana however waafrika tunapenda kujikweza sana lakini dogo ukifuatilia.maisha ya warren buffet billionaire mkubwa kabisa duniani.utashangaa....mfano.mdogo ulishawahi kukutana na mmiliki wa OILCOM..? Yuko simple sana sasa ngoja ukutane na wamiliki wa vikampuni uchwara mjini hapa ambavyo hata kodi havilipi.. Utakuta cheni kubwa, pete.mikono yote, simu mbili moja iphone nyingine samsung note.. Yaani mbwembwe tupu
 
Nimekuona si mara moja ukipata lunch kwenye kihoteli cha wasomali mtaa wa kongo , kariakoo .

Hiki kihoteli kisichokuwa hata na feni achilia mbali a/c si sawa kwa hadhi yako , hakuna haja ya wewe kocha msaidizi wa Yanga afrika kwenda kubanana na wamachinga kwenye foleni ya wali nyama wa 3500 /, pondamali atakupoteza , mbona yeye hali kwa wasomali ?

Ingekuwa simba tusingeshangaa lakini yanga mbona shida hizo hakuna ? Jiangalie mkuu na ikiwezekana jirekebishe .

.....Itaendelea ikibidi .
Mkuu usiogopeshwe na kelele za kandambil,, yule muhind hafanyi biashara kichaa, wengi wanalipwa deiwaka ila wanaogopa kulalamika watatimuliwa
 
Tatizo liko wapi? Tena hata hiyo 3500 ni nyingi, mi ngekuwa yeye ningekuwa nakula cha 1500 kabisa.

Maisha yenyewe ya Bongo hayatabiriki. Kesho akipigwa chini si mtamcheka hana kitu, pesa yote kamalizia kwa wasomali.
Kwa tunaojua shughul ya uwanjani msos wa 3500 haukidhi shughul ya uwanjani

Mimi ninaecheza mchangan for fun
Huwa sili hivo
 
N nyie makocha wenu wanaokula mlimani city mnafanya nini kiwanjani.......................
 
Kwani mwambusi ni mchezaji au kocha?

Chakula kina matter kwa kocha?
Huyu mwambusi kule mbeya ni sawa na mfalme , hawezi kuthubutu kula kwenye magenge ya Mwanjelwa , inakuwaje huku yanga ?
 
Nilikuwa duka fulani la mpemba maeneo ya Bunju, Dar es Salaam.

Ghafla nikaona basi la Simba SC likisimama na wakashuka wachezaji wakaja dukani kununua Maji ya Kandoro.

Mmoja aliamua kununua maji 6, kaweka kwenye mfuko wa rambo.
Hahahaah umetisha.!
 
maximo alikuwa anakula mpaka mishikaki ya barabarani,uajabu upo wapi
 
Mimi ni Mwanasimba mwenye matarajio ya kuongoza timu , wala sina kolabo yoyote na Yanga , lakini nimesononeka sana kwa huyu shujaa wa timu yenu kumuona mara nyingi akila uswahilini , kama shida ni hela basi alipwe malimbikizo yake , hawa makocha wa yanga na simba wanavumilia mengi sana ambayo wewe huyajui .
Chapati za kaduguda mlishamlipa hela yake? dogo umeingia Dar mwaka gani mbona mjuaji sana?
 
hahah
Nilikuwa duka fulani la mpemba maeneo ya Bunju, Dar es Salaam.

Ghafla nikaona basi la Simba SC likisimama na wakashuka wachezaji wakaja dukani kununua Maji ya Kandoro.

Mmoja aliamua kununua maji 6, kaweka kwenye mfuko wa rambo.


hahaha daah iachee simba yetu
 
Chapati za kaduguda mlishamlipa hela yake? dogo umeingia Dar mwaka gani mbona mjuaji sana?
Umeuliza swali zuri sana kuhusu Kaduguda , lakini umemaliza kwa majungu hivyo sitakujibu , kumuambia mtu anayejua eti anajifanya mjuaji ni kuhangaisha akili yako bure , anayejua anajua tu mkuu .
 
Back
Top Bottom