Mwamko Mpya Kuhusu Historia ya Bi. Titi Mohamed

Mwamko Mpya Kuhusu Historia ya Bi. Titi Mohamed

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
MWAMKO MPYA KUHUSU HISTORIA YA BI. TITI

Mwaka jana 2021 kuanzia mwezi October hadi kufika mwezi kama huu na siku kama hizi nilipokea wageni wengi nyumbani kwangu kutoka vyombo vya habari pamoja na CCM wakitafuta historia ya Bi. Titi.

Hakika haya ndiyo maajabu ya Allah kuwa atakapo jambo lake huwa.

Bi. Titi alinyang'anywa mtaa aliopewa kwa heshima yake katika kupigania uhuru wa Tanganyika na akafutwa katika historia ya TANU kama walivyofutwa wazalendo wengine wengi.

Lakini kwa njia ambazo naamini hata yeye mwenyewe zilimstaajabisha Bi. Titi akarudi katika mwanga akawa anasikika na kuonekana.

Mwaka huu yale ya mwaka jana yanajirudia katika kutafuta historia ya Bi. Titi Mohamed.

Vyombo vya habari vinataka mwaka huu pia kumwadhimisha Bi. Titi Mohamed na kazi kubwa inakuwa kwangu nimweleze Bi. Titi katika namna ambayo itavutia isiwe mambo kuwa yayo kwa yayo.

Ikiwa hivi historia ya Bi. Titi itachusha na kuchosha.

Nawaeleza watafiti wa historia ya Bi. Titi kuwa tusifanye makosa ya wanahistoria waliopita walioandika historia ya uhuru wa Tanganyika kwa kumtaja Nyerere peke yake kama vile TANU haikuwa na wapigania uhuru wengine ila Mwalimu peke yake.

Ukiangalia picha ya kwanza utaona ni Bi. Titi Mohamed na Julius Nyerere wakicheza dansi kusheherekea uhuru wa Tanganyika mwaka wa 1961.

Picha ya pili ni Bi. Halima bint Khamisi na Nyerere miaka mingi baada ya uhuru wakati Mwalimu sasa anaacha uongozi kama Rais.

Wengi watashangaa kusikia kuwa uongozi wa wanawake katika kupigania uhuru wa Tanganyika ulikuwa uchukuliwe na yeyote katika hawa akina mama wawili.

Uongozi uende kwa Bi. Halima au kwa Bi. Titi.

Lakini akina mama hawa kwa ujumla wao ukitaka kujua nguvu yao lazima nikufikishe Viwanja Vya Mnazi Mmoja kwenye mkutano wa TANU mwaka wa 1955 uone walipokuwa wanakaa na nikuhadithie yale waliyokuwa wakifanya katika vibweka kunogesha mkutano.

Angalia picha ya tatu mkono wa kushoto utaona sehemu kuna rangi nyeusi tupu.

Hayo ni mabaibui ya waliovaa wanawake na wamekaa sehemu maalum waliyotengewa wasichanganyike na wanaume.

Picha ya nne nimeiweka makhsusi ili haya mabaibui yaonekane na kufahamika yalikuwaje kwani hivi sasa hayapo kamwe.

Picha hiyo inamuonyesha kulia Bi. Chiku bint Said Kisusa, Bi. Titi Mohamed, na mwanzo kushoto ni Bi. Tatu bint Mzee na Julius Nyerere ni huyo katikati wanamsindikiza safari ya kwanza UNO Februari 1955.

Jana nilifanya kipindi na TBC nikahojiwa na Dioniz Kidai na hayo niliyoeleza hapo juu ndimo tulimopita katika kueleza historia ya Bi. Titi Mohamed na wazalendo wengine wanawake kutoka majimboni walipogania uhuru mfano wa Bi. Halima Selengia, Amina Kinabo, Mama bint Maalim, Lucy Lameck kutoka Moshi, Shariffa bint Mzee kutoka Lindi, Bi. Zarula bint Abdulrahman na Nyange Bint Chande kutoka Tabora, Bi. Fatuma Matola kutoka Mbeya na wengine wengi

1670130630041.png
1670130914704.png

1670130808274.png
1670130845226.png
 
MWAMKO MPYA KUHUSU HISTORIA YA BI. TITI

Mwaka jana 2021 kuanzia mwezi October hadi kufika mwezi kama huu na siku kama hizi nilipokea wageni wengi nyumbani kwangu kutoka vyombo vya habari pamoja na CCM wakitafuta historia ya Bi. Titi.

Hakika haya ndiyo maajabu ya Allah kuwa atakapo jambo lake huwa.

Bi. Titi alinyang'anywa mtaa aliopewa kwa heshima yake katika kupigania uhuru wa Tanganyika na akafutwa katika historia ya TANU kama walivyofutwa wazalendo wengine wengi.

Lakini kwa njia ambazo naamini hata yeye mwenyewe zilimstaajabisha Bi. Titi akarudi katika mwanga akawa anasikika na kuonekana.

Mwaka huu yale ya mwaka jana yanajirudia katika kutafuta historia ya Bi. Titi Mohamed.

Vyombo vya habari vinataka mwaka huu pia kumwadhimisha Bi. Titi Mohamed na kazi kubwa inakuwa kwangu nimweleze Bi. Titi katika namna ambayo itavutia isiwe mambo kuwa yayo kwa yayo.

Ikiwa hivi historia ya Bi. Titi itachusha na kuchosha.

Nawaeleza watafiti wa historia ya Bi. Titi kuwa tusifanye makosa ya wanahistoria waliopita walioandika historia ya uhuru wa Tanganyika kwa kumtaja Nyerere peke yake kama vile TANU haikuwa na wapigania uhuru wengine ila Mwalimu peke yake.

Ukiangalia picha ya kwanza utaona ni Bi. Titi Mohamed na Julius Nyerere wakicheza dansi kusheherekea uhuru wa Tanganyika mwaka wa 1961.

Picha ya pili ni Bi. Halima bint Khamisi na Nyerere miaka mingi baada ya uhuru wakati Mwalimu sasa anaacha uongozi kama Rais.

Wengi watashangaa kusikia kuwa uongozi wa wanawake katika kupigania uhuru wa Tanganyika ulikuwa uchukuliwe na yeyote katika hawa akina mama wawili.

Uongozi uende kwa Bi. Halima au kwa Bi. Titi.

Lakini akina mama hawa kwa ujumla wao ukitaka kujua nguvu yao lazima nikufikishe Viwanja Vya Mnazi Mmoja kwenye mkutano wa TANU mwaka wa 1955 uone walipokuwa wanakaa na nikuhadithie yale waliyokuwa wakifanya katika vibweka kunogesha mkutano.

Angalia picha ya tatu mkono wa kushoto utaona sehemu kuna rangi nyeusi tupu.

Hayo ni mabaibui ya waliovaa wanawake na wamekaa sehemu maalum waliyotengewa wasichanganyike na wanaume.

Picha ya nne nimeiweka makhsusi ili haya mabaibui yaonekane na kufahamika yalikuwaje kwani hivi sasa hayapo kamwe.

Picha hiyo inamuonyesha kulia Bi. Chiku bint Said Kisusa, Bi. Titi Mohamed, na mwanzo kushoto ni Bi. Tatu bint Mzee na Julius Nyerere ni huyo katikati wanamsindikiza safari ya kwanza UNO Februari 1955.

Jana nilifanya kipindi na TBC nikahojiwa na Dioniz Kidai na hayo niliyoeleza hapo juu ndimo tulimopita katika kueleza historia ya Bi. Titi Mohamed na wazalendo wengine wanawake kutoka majimboni walipogania uhuru mfano wa Bi. Halima Selengia, Amina Kinabo, Mama bint Maalim, Lucy Lameck kutoka Moshi, Shariffa bint Mzee kutoka Lindi, Bi. Zarula bint Abdulrahman na Nyange Bint Chande kutoka Tabora, Bi. Fatuma Matola kutoka Mbeya na wengine wengi
𝒏𝒊 𝒏𝒊𝒏𝒊 𝒌𝒊𝒍𝒊𝒔𝒂𝒃𝒂𝒃𝒊𝒔𝒉𝒂 𝒉𝒊𝒔𝒕𝒐𝒓𝒊𝒂 𝒚𝒂𝒐 𝒊𝒔𝒊𝒂𝒏𝒅𝒊𝒌𝒘𝒆 𝒏𝒂 𝒕𝒂𝒏𝒈𝒖 𝒎𝒘𝒂𝒏𝒛𝒐!! 𝒘𝒂 𝒖𝒂𝒏𝒅𝒊𝒌𝒂𝒋𝒊 𝒌𝒖𝒎𝒃𝒖𝒌𝒖𝒎𝒃𝒖 𝒛𝒂 𝒘𝒂𝒑𝒊𝒈𝒂𝒏𝒊𝒂 𝒖𝒉𝒖𝒓𝒖?!
 
Hiyo picha ya tatu kama hapo ndio palikuwa mnazi mmoja na nyumba za makuti je huko mwananyamala, kinondoni, temeke, ukonga, tabata, mbezi beach, tegeta kulikuwaje?
 
Hiyo picha ya tatu kama hapo ndio palikuwa mnazi mmoja na nyumba za makuti je huko mwananyamala, kinondoni, temeke, ukonga, tabata, mbezi beach, tegeta kulikuwaje?
Palikuwa shamba huko.
 
Bibi titi alitaka kupindua nchi..hivyo alichokipata alistahili.

Halafuu huu utaratibu wa kuvalisha wanafunzi wakike wa kiisalmu baibui sijui nani aliuanzisha unaleta utengano katika jamii yetu..ni utaratibu mbovu sana na waajabu.

Historia huandikwa na washindi..sio walioshindwa..hivyo mzee saidi kuwa mpole hata upambane vipi historia imeshaandikwa ya washindi..hiyo yako niyakujifariji tu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Bibi titi alitaka kupindua nchi..hivyo alichokipata alistahili.

Halafuu huu utaratibu wa kuvalisha wanafunzi wakike wa kiisalmu baibui sijui nani aliuanzisha unaleta utengano katika jamii yetu..ni utaratibu mbovu sana na waajabu.

Historia huandikwa na washindi..sio walioshindwa..hivyo mzee saidi kuwa mpole hata upambane vipi historia imeshaandikwa ya washindi..hiyo yako niyakujifariji tu.

#MaendeleoHayanaChama
Jiwe...
Hapana si kweli usemayo.

Kitabu cha Abdul Sykes kimebadili historia ya uhuru wa Tanganyika.

Ndiyo maana unaona leo kila uchao nahojiwa na vyombo vya habari kuhusu historia ya uhuru wa Tanganyika.

Kuelekea kumbukumbu ya uhuru wa Tanganyika ratiba yangu imejaa.

Tumefanya kipindi cha Bi. Titi viwili kwa vyombo tofauti na vinavyofuatia In Shaa Allah ni viwili vingine kipindi cha Mshume Kiyate na cha Julius Nyerere.

Vyote nitaviweka hapa.

Hawa ni TBC wanafunga mitambo kwa ajili ya mahojiano kuhusu historia ya uhuru wa Tanganyika.

1670177811977.png
 
Back
Top Bottom