Fanya harusi au party ya uwezo wako...usiogope watu watakuonajeKama huwezi kuchangia kila mtu, changia unaoweza.
Kwann liwe swala la muda wakati watu hawana ajira?Bangi inaweza kuwa regulated na ikaingizwa kwenye mfumo rasmi kama vileo vingine. Ni moja ya zao zuri la uchumi.
Ni suala la muda tu. Itaruhusiwa.
Kuoa si jambo la dharura kwa wahusika, hata aina ya kuoa, ndoa, na sherehe ni maamuzi yako. Kuchangisha michango ni unyonyaji, utumwa, kuwa omba omba, kujivika kilema, kusujudu, shortcut ya kuwa na nyumba, kiwanja, gari na etc.Najua Hamisi Mwinyijuma au Mwana FA ni miongoni mwa wasanii wachache wasomi tulionao hapa Tanzania.
Ukiwa msomi, tunatarajia uwe na fikra pana na za kina kwenye masuala mbalimbali ya kijamii na mazingira yanayokuzunguka, ukiachana na yale ya fani uliyosomea.
NATAKA KUSEMA NINI?
Nimeona video fupi ikisambaa inayomuonesha MwanaFA akizungumzia suala la michango ya harusi. Kwamba, yeye hachangii harusi kwani ni suala la mtu binafsi na linahitaji maandalizi. Yuko tayari kuchangia Msiba, si harusi.
Kwanza, huo ni mtazamo unaofikirisha lakini pia ni mtazamo wa watu wengi. Watu wamechoka na utaratibu wa kuchangia harusi. Mimi ni mmojawapo [emoji2]
Hata hivyo, nikiangalia mnyororo wa thamani uliopo kwenye hizi sherehe na ajira zilizozalishwa, nabaki kuona ni jambo zuri na lenye tija.
Ukichangia harusi, unatoa ajira kwa watu wengi sana. Kuanzia MC, watu wa mapambo, chakula, wapiga picha, maids, watoa burudani n.k.
Faida nyingine ni mzunguko wa fedha kuchochea uchumi wa eneo husika, kuimarisha undugu na ujamaa, kutengeneza kumbukumbu na mengine mengi.
Wapo wasiochangisha watu kwenye mambo ya sherehe, lakini hao ni wale wanaojiweza, vipi wale wasiojiweza?
USHAURI WANGU
Tusiache kuchangiana kama tunapendana na kushirikiana. Umoja ni nguvu. Sherehe za harusi sio suala binafsi tena, ni suala la kiuchumi na maisha ya watu wengi yanategemea hapo.
Mwezi wa 6 mwakani nafunga ndoa. Nitatoa kadi za michango. Mnichangie. Puuzeni maneno laini laini ya Hamisi.
Na mimi nasimama na wewe [emoji1666]Nasimama na Mwana FA.
Kwa nini usichangie mwanafunzi anayedaiwa ada ya elfu 50 au laki moja? Kwa nini usichangie omba omba au mgonjwa ambao wana uhitaji zaidi?Haikupi raha kuona mchango wako unatoa ajira kwa watu?
Umechanganya mambo. Hayo mambo ya mitaro, madaraja, umeme na mengine ni majukumu ya serikali kutokana na kodi zinazokusanywa.Kuoa si jambo la dharura kwa wahusika, hata aina ya kuoa, ndoa, na sherehe ni maamuzi yako. Kuchangisha michango ni unyonyaji, utumwa, kuwa omba omba, kujivika kilema, kusujudu, shortcut ya kuwa na nyumba, kiwanja, gari na etc.
Kuchangisha harusi na masherehe ni unyonyaji, tuanze kuchanga kuuguza, kusomesha, kujenga nyumba, hospitali, madaraja, macaravati, mitaro, kuvuta maji, nguzo za umeme, posho za waalimu, madarasa, vyoo.
Nyie ndiyo wale mko baa na msitu wa chupa za bia na sinia la kiti moto na ndizi halafu anapita omba omba mnampa Mia moja badala ya hata elfu mbili.Kuchangiana ni act of love.
Nakubaliana na wewe kwa kiasi fulani. Suala la bei kupandishwa ni law of demand & supply, haiwezi kuzuilika.Michango ya harusi imefanya gharama ya kufanya sherehe iwe juu sana with the assumption kuwa kila mtu anachangiwa.
Yaani vendors wameweka bei zisizo na uhalisia kiasi kwamba kama unataka fanya sherehe yako bila kuchangisha watu inakucost sana.
I hope itafika wakati tutaacha kuchangiana. Michango ibaki ndani ya familia ya karibu.