Mwana FA hajui mnyororo wa thamani katika sherehe za harusi, aelimishwe...

Mwana FA hajui mnyororo wa thamani katika sherehe za harusi, aelimishwe...

Bangi inaweza kuwa regulated na ikaingizwa kwenye mfumo rasmi kama vileo vingine. Ni moja ya zao zuri la uchumi.

Ni suala la muda tu. Itaruhusiwa.
Kwann liwe swala la muda wakati watu hawana ajira?
 
Najua Hamisi Mwinyijuma au Mwana FA ni miongoni mwa wasanii wachache wasomi tulionao hapa Tanzania.

Ukiwa msomi, tunatarajia uwe na fikra pana na za kina kwenye masuala mbalimbali ya kijamii na mazingira yanayokuzunguka, ukiachana na yale ya fani uliyosomea.

NATAKA KUSEMA NINI?

Nimeona video fupi ikisambaa inayomuonesha MwanaFA akizungumzia suala la michango ya harusi. Kwamba, yeye hachangii harusi kwani ni suala la mtu binafsi na linahitaji maandalizi. Yuko tayari kuchangia Msiba, si harusi.

Kwanza, huo ni mtazamo unaofikirisha lakini pia ni mtazamo wa watu wengi. Watu wamechoka na utaratibu wa kuchangia harusi. Mimi ni mmojawapo [emoji2]

Hata hivyo, nikiangalia mnyororo wa thamani uliopo kwenye hizi sherehe na ajira zilizozalishwa, nabaki kuona ni jambo zuri na lenye tija.

Ukichangia harusi, unatoa ajira kwa watu wengi sana. Kuanzia MC, watu wa mapambo, chakula, wapiga picha, maids, watoa burudani n.k.

Faida nyingine ni mzunguko wa fedha kuchochea uchumi wa eneo husika, kuimarisha undugu na ujamaa, kutengeneza kumbukumbu na mengine mengi.

Wapo wasiochangisha watu kwenye mambo ya sherehe, lakini hao ni wale wanaojiweza, vipi wale wasiojiweza?

USHAURI WANGU

Tusiache kuchangiana kama tunapendana na kushirikiana. Umoja ni nguvu. Sherehe za harusi sio suala binafsi tena, ni suala la kiuchumi na maisha ya watu wengi yanategemea hapo.

Mwezi wa 6 mwakani nafunga ndoa. Nitatoa kadi za michango. Mnichangie. Puuzeni maneno laini laini ya Hamisi.
Kuoa si jambo la dharura kwa wahusika, hata aina ya kuoa, ndoa, na sherehe ni maamuzi yako. Kuchangisha michango ni unyonyaji, utumwa, kuwa omba omba, kujivika kilema, kusujudu, shortcut ya kuwa na nyumba, kiwanja, gari na etc.

Kuchangisha harusi na masherehe ni unyonyaji, tuanze kuchanga kuuguza, kusomesha, kujenga nyumba, hospitali, madaraja, macaravati, mitaro, kuvuta maji, nguzo za umeme, posho za waalimu, madarasa, vyoo.
 
Kuna watu tumesha wachangia ila leo wanasema ni suala binafsi kwA kuwa tu wamesha toka kwenye hili jambo

Wazee hili si suala binafsi ni suala la kijamii kama ilivyo misiba na magonjwa tuendelee kusaidiana (kudumisha undugu) kuwa pamoja na kuleta ukaribu

Kwamba uache kunichangia (makusudi) kwenye sherehe alafu ukipata shida utegemee nijitoe kukusaidia (100%) unaumwa wewe?
Tusaidiane kwenye shida (misiba, magonjwa) na raha (sherehe) sema hii michango ya laki si pesa hapana

Michango ya birthday pia hapana, michango ya mke wa 2 hapana pia
 
Michango ya harusi imefanya gharama ya kufanya sherehe iwe juu sana with the assumption kuwa kila mtu anachangiwa.

Yaani vendors wameweka bei zisizo na uhalisia kiasi kwamba kama unataka fanya sherehe yako bila kuchangisha watu inakucost sana.

I hope itafika wakati tutaacha kuchangiana. Michango ibaki ndani ya familia ya karibu.
 
Ndio ukitaka mbwembwe jipande na ndoa zenyewe zisivyo dumu sasa kama ndoa ya juzi ya manara[emoji849][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Kuoa si jambo la dharura kwa wahusika, hata aina ya kuoa, ndoa, na sherehe ni maamuzi yako. Kuchangisha michango ni unyonyaji, utumwa, kuwa omba omba, kujivika kilema, kusujudu, shortcut ya kuwa na nyumba, kiwanja, gari na etc.

Kuchangisha harusi na masherehe ni unyonyaji, tuanze kuchanga kuuguza, kusomesha, kujenga nyumba, hospitali, madaraja, macaravati, mitaro, kuvuta maji, nguzo za umeme, posho za waalimu, madarasa, vyoo.
Umechanganya mambo. Hayo mambo ya mitaro, madaraja, umeme na mengine ni majukumu ya serikali kutokana na kodi zinazokusanywa.

Suala hili la kijamii na kiuchumi (socio-economy) tunaliweza. Ni letu.
 
michango imezidi sana aisee yaani tungekua kama wenzetu kenya wanaochangia harambee kwaajili ya kusomeshana , ujenzi nk tungekua mbali sana , kibaya zaidi hata hao wanaochangisha wanadai as if ni kitu cha lazima kabisa
 
Michango ya harusi imefanya gharama ya kufanya sherehe iwe juu sana with the assumption kuwa kila mtu anachangiwa.

Yaani vendors wameweka bei zisizo na uhalisia kiasi kwamba kama unataka fanya sherehe yako bila kuchangisha watu inakucost sana.

I hope itafika wakati tutaacha kuchangiana. Michango ibaki ndani ya familia ya karibu.
Nakubaliana na wewe kwa kiasi fulani. Suala la bei kupandishwa ni law of demand & supply, haiwezi kuzuilika.

Tunaweza kukubaliana namna ya kuchangiana na viwango elekezi, lakini kuona kwamba lote ni jambo lisilofaa hapana kwa kweli.

Hii 'culture' tayari imeshakuwa ni moja ya sekta ndogo ya kiuchumi.
 
Back
Top Bottom