Mwana FA hajui mnyororo wa thamani katika sherehe za harusi, aelimishwe...

Mwana FA hajui mnyororo wa thamani katika sherehe za harusi, aelimishwe...

Najua Hamisi Mwinyijuma au Mwana FA ni miongoni mwa wasanii wachache wasomi tulionao hapa Tanzania.

Ukiwa msomi, tunatarajia uwe na fikra pana na za kina kwenye masuala mbalimbali ya kijamii na mazingira yanayokuzunguka, ukiachana na yale ya fani uliyosomea.

NATAKA KUSEMA NINI?

Nimeona video fupi ikisambaa inayomuonesha MwanaFA akizungumzia suala la michango ya harusi. Kwamba, yeye hachangii harusi kwani ni suala la mtu binafsi na linahitaji maandalizi. Yuko tayari kuchangia Msiba, si harusi.

Kwanza, huo ni mtazamo unaofikirisha lakini pia ni mtazamo wa watu wengi. Watu wamechoka na utaratibu wa kuchangia harusi. Mimi ni mmojawapo [emoji2]

Hata hivyo, nikiangalia mnyororo wa thamani uliopo kwenye hizi sherehe na ajira zilizozalishwa, nabaki kuona ni jambo zuri na lenye tija.

Ukichangia harusi, unatoa ajira kwa watu wengi sana. Kuanzia MC, watu wa mapambo, chakula, wapiga picha, maids, watoa burudani n.k.

Faida nyingine ni mzunguko wa fedha kuchochea uchumi wa eneo husika, kuimarisha undugu na ujamaa, kutengeneza kumbukumbu na mengine mengi.

Wapo wasiochangisha watu kwenye mambo ya sherehe, lakini hao ni wale wanaojiweza, vipi wale wasiojiweza?

USHAURI WANGU

Tusiache kuchangiana kama tunapendana na kushirikiana. Umoja ni nguvu. Sherehe za harusi sio suala binafsi tena, ni suala la kiuchumi na maisha ya watu wengi yanategemea hapo.

Mwezi wa 6 mwakani nafunga ndoa. Nitatoa kadi za michango. Mnichangie. Puuzeni maneno laini laini ya Hamisi.

Mkuu natarajia kufunga ndoa mapema hivi karibuni! Tafadhali mchango wako ni wa muhimu sana ili kufanikisha jambo hili!
Tupendane mkuu...
 
Kuoa si jambo la dharura kwa wahusika, hata aina ya kuoa, ndoa, na sherehe ni maamuzi yako. Kuchangisha michango ni unyonyaji, utumwa, kuwa omba omba, kujivika kilema, kusujudu, shortcut ya kuwa na nyumba, kiwanja, gari na etc.

Kuchangisha harusi na masherehe ni unyonyaji, tuanze kuchanga kuuguza, kusomesha, kujenga nyumba, hospitali, madaraja, macaravati, mitaro, kuvuta maji, nguzo za umeme, posho za waalimu, madarasa, vyoo.
Wazaramo wanasema usipohusika kwenye ngoma yamwanangu nakwenye msiba wamzazi wako usinitumaini
 
Naunga mkono hoja ya Mwana FA. Hata mimi sichangii sherehe yoyote.
Nitoe pesa ya mchango,
Nitoe pesa ya nguo sijui sare,
Nitoe pesa ya zawadi,
Bado sijafanya make up,
Hehehehe

Tena usiombee waoane wakiwa washatiana mimba, hujakaa sawa kidogo mtoto kazaliwa upeleke zawadi bado arobaini ya mtoto ukinusurika kuchangishwa basi zawadi lazima, looooh!
 
Nitoe pesa ya mchango,
Nitoe pesa ya nguo sijui sare,
Nitoe pesa ya zawadi,
Bado sijafanya make up,
Hehehehe

Tena usiombee waoane wakiwa washatiana mimba, hujakaa sawa kidogo mtoto kazaliwa upeleke zawadi bado arobaini ya mtoto ukinusurika kuchangishwa basi zawadi lazima, looooh!
Upuuzi mtupu.
 
aiseee haya mambo mi huwaga sishiriki kabisa nachangia tu kufanikisha ila msiba hta mkoani naenda kwa gharama yeyote
kwa nn naona ni mambo ya showoff tu kelele gharama kibao za harusi final haina tija mi nilikataa since graduation ya form 4&6 mpaka chuo napenda mtu afanyiwe hata kumchangia kama uwezo ninao ila mm siwezi kabisa
hata siku nikioa nataka ile kimya kimya sherehe mi labda nshaondoka
 
Si anajiweza mkuu, sisi kina pangu pakavu atuache tuendelee saidiana mkuu asilete mawazo yake ya kibwanyenye kwetu (kumbuka Ana mgao wa bilioni kadhaa toka tigo)

Wewe na mimi wa dagaa za mia mia tukisema tufate mawazo ya bwanyenye mwana fa nakwambia tunaenda vunja undugu, urafiki na watu

Kutochangisha yeye haifanyi kitendo hiki kuwa haramu tuendelee changishana harusi ni sehemu ya kujamiiana pia sawa na misiba na magonjwa
Suala sio kujiweza, suala mnapenda show off
 
Back
Top Bottom