Mwana FA hajui mnyororo wa thamani katika sherehe za harusi, aelimishwe...

Mwana FA hajui mnyororo wa thamani katika sherehe za harusi, aelimishwe...

Nitoe pesa ya mchango,
Nitoe pesa ya nguo sijui sare,
Nitoe pesa ya zawadi,
Bado sijafanya make up,
Hehehehe

Tena usiombee waoane wakiwa washatiana mimba, hujakaa sawa kidogo mtoto kazaliwa upeleke zawadi bado arobaini ya mtoto ukinusurika kuchangishwa basi zawadi lazima, looooh!
Huu ulazima unatoka wapi?

Hii tabia ya kuchanga ili uchangiwe inaharibu wengi.
 
Marafiki/Ndg/Watu wa karibu yetu wanataka kuoa wanatamani kufanya sherehe nzuri ilhali hawana uwezo wa kufanikisha wanachokitaka wanaomba tuwasaidie kuwachangia waongezee walipokwama hilo ni tatizo?? binafsi sioni tatizo kwenye hilo
 
Mwezi wa 10 nilikuwa Nina kadi 2

Nimechanga moja ingine nimechinjia baharini

Nimeangalia mahusiano yangu na hao wahusika

Infact sipendi michango kabisa .

Unaweza shangaa kiutani utani mwezi mzima unatoa 250k hivi hivi

Kama itakuja tokea nikaoa nitajikusanya mwenyewe nimalize kila kitu bila kusumbua mifuko ya watu
 
Mimi sijawahi kupinga michango kwa shughuli yoyote ya kijamii.

Na kama inavyotajwa ni kweli ni jambo binafsi, lakini tuangalie zaidi Jamii kukutana na kufurahia pamoja...na si kusubiri kukutana wakati wa matatizo tu.

Muhimu ni kuwakumbusha Watu kukumbuka pia kuchangia shughuli kama matibabu n.k.

Pia shughuli hizi hutengeneza ajira kwa kada tofauti sambamba na kusisimua uchumi kwa wanaokodisha kumbi, wanaotengeneza na wanaouza Vinywaji, Nyama, Mchele n.k.

Sioni tatizo labda jamii tu wakumbushwe kuangalia mifuko ya wale wanaodaiwa michango ili wasiumie kwa kuwekewa viwango wasivyovimudu.
 
Mimi sijawahi kupinga michango kwa shughuli yoyote ya kijamii.

Na kama inavyotajwa ni kweli ni jambo binafsi, lakini tuangalie zaidi Jamii kukutana na kufurahia pamoja...na si kusubiri kukutana wakati wa matatizo tu.

Muhimu ni kuwakumbusha Watu kukumbuka pia kuchangia shughuli kama matibabu n.k.

Pia shughuli hizi hutengeneza ajira kwa kada tofauti sambamba na kusisimu uchumi kwa wanaokodisha kumbi, wanaotengeneza na wanaouza Vinywaji, Nyama, Mchele n.k.

Sioni tatizo labda jamii tu wakumbushwe kuangalia mifuko ya wale wanaodaiwa michango ili wasiumie wa kuwekewa viwango wasivyovimudu.
Umeiweka vizuri sana.

Halafu ukichunguza wanaopinga michango kwa mbwembwe humu, usikute ndio mahodari wa kuchangia mpaka vigodoro.

Tukubaliane kwenye utaratibu na viwango vya michango. Iwe ni hiari pia na sio deni.

Aidha michango iendelee ili tuzidi kusisimua uchumi wa mtu mmoja mmoja waliomo katika mnyonyoro wa thamani wa hizi sherehe.

Tufunge mjadala?
 
Kwani ukijigharamia hizo gharama za harusi hao uliowataja hawapati ajira sijui ma mc, wapishi nk?
 
aiseee haya mambo mi huwaga sishiriki kabisa nachangia tu kufanikisha ila msiba hta mkoani naenda kwa gharama yeyote
kwa nn naona ni mambo ya showoff tu kelele gharama kibao za harusi final haina tija mi nilikataa since graduation ya form 4&6 mpaka chuo napenda mtu afanyiwe hata kumchangia kama uwezo ninao ila mm siwezi kabisa
hata siku nikioa nataka ile kimya kimya sherehe mi labda nshaondoka
Mkuu mie harusi yangu Jumla tulikua watu 6, yaani mimi, wife, mashahidi 2(Mke na Mume), DAS na Msaidi wa DAS. Na sitakagi usumbufu kabisa linapokuja swala la michango iwe ndugu or jamaa wa karibu. Najituma na kutoa zaidi katika wagonjwa na Misiba, kwenye misiba hapo hadi nasafiri kabisa pia.

Hoja yangu ni kwamba, harusi sio bahati mbaya watu wajiandae wamalize mambo yao wenyewe. Uki'complicate ndio inakua gharama. Mimi harusi yangu jumla ili gharimu TZS 50,000 ya kuandikisha tuu, Mavazi, sijui viatu nilitumia ambavyo nilikua navaa siku zote same to wife.
 
Watu kushiriki tukio la harusi haiwapi mamlaka katika ndoa yako. Unawazaje?

Ni kweli kama mtu ana uwezo wa kulipia vyote hivyo bila kuchukua hata senti ya mtu ni jambo zuri, lakini sio wote wenye uwezo, ndipo hata wazo l a kuchangishana lilipoibuka.
Sherehe sio lazima mkuu. Anaweza funga ndoa vizuri kabisa bila ya sherehe kama uwezo ni mdogo.
 
Mi naona ni bora kuchangia harusi kuliko msiba, mtu akifa akazikwe tu na maisha yaendelee, harusi tuchangie tufurahie maisha
 
Najua Hamisi Mwinyijuma au Mwana FA ni miongoni mwa wasanii wachache wasomi tulionao hapa Tanzania.

Ukiwa msomi, tunatarajia uwe na fikra pana na za kina kwenye masuala mbalimbali ya kijamii na mazingira yanayokuzunguka, ukiachana na yale ya fani uliyosomea.

NATAKA KUSEMA NINI?

Nimeona video fupi ikisambaa inayomuonesha MwanaFA akizungumzia suala la michango ya harusi. Kwamba, yeye hachangii harusi kwani ni suala la mtu binafsi na linahitaji maandalizi. Yuko tayari kuchangia Msiba, si harusi.

Kwanza, huo ni mtazamo unaofikirisha lakini pia ni mtazamo wa watu wengi. Watu wamechoka na utaratibu wa kuchangia harusi. Mimi ni mmojawapo [emoji2]

Hata hivyo, nikiangalia mnyororo wa thamani uliopo kwenye hizi sherehe na ajira zilizozalishwa, nabaki kuona ni jambo zuri na lenye tija.

Ukichangia harusi, unatoa ajira kwa watu wengi sana. Kuanzia MC, watu wa mapambo, chakula, wapiga picha, maids, watoa burudani n.k.

Faida nyingine ni mzunguko wa fedha kuchochea uchumi wa eneo husika, kuimarisha undugu na ujamaa, kutengeneza kumbukumbu na mengine mengi.

Wapo wasiochangisha watu kwenye mambo ya sherehe, lakini hao ni wale wanaojiweza, vipi wale wasiojiweza?

USHAURI WANGU

Tusiache kuchangiana kama tunapendana na kushirikiana. Umoja ni nguvu. Sherehe za harusi sio suala binafsi tena, ni suala la kiuchumi na maisha ya watu wengi yanategemea hapo.

Mwezi wa 6 mwakani nafunga ndoa. Nitatoa kadi za michango. Mnichangie. Puuzeni maneno laini laini ya Hamisi.
Huyu jamaa nimshamba sana ndio maana wenzake wanasema anaringa,kupata kidegree kimoja anajiona ni professor ni bogus tu na misemo yake ya yakujifanya highly conscious..

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Mkuu mie harusi yangu Jumla tulikua watu 6, yaani mimi, wife, mashahidi 2(Mke na Mume), DAS na Msaidi wa DAS. Na sitakagi usumbufu kabisa linapokuja swala la michango iwe ndugu or jamaa wa karibu. Najituma na kutoa zaidi katika wagonjwa na Misiba, kwenye misiba hapo hadi nasafiri kabisa pia.

Hoja yangu ni kwamba, harusi sio bahati mbaya watu wajiandae wamalize mambo yao wenyewe. Uki'complicate ndio inakua gharama. Mimi harusi yangu jumla ili gharimu TZS 50,000 ya kuandikisha tuu, Mavazi, sijui viatu nilitumia ambavyo nilikua navaa siku zote same to wife.
Kibingwa zaidi mkuu
 
Najua Hamisi Mwinyijuma au Mwana FA ni miongoni mwa wasanii wachache wasomi tulionao hapa Tanzania.

Ukiwa msomi, tunatarajia uwe na fikra pana na za kina kwenye masuala mbalimbali ya kijamii na mazingira yanayokuzunguka, ukiachana na yale ya fani uliyosomea.

NATAKA KUSEMA NINI?

Nimeona video fupi ikisambaa inayomuonesha MwanaFA akizungumzia suala la michango ya harusi. Kwamba, yeye hachangii harusi kwani ni suala la mtu binafsi na linahitaji maandalizi. Yuko tayari kuchangia Msiba, si harusi.

Kwanza, huo ni mtazamo unaofikirisha lakini pia ni mtazamo wa watu wengi. Watu wamechoka na utaratibu wa kuchangia harusi. Mimi ni mmojawapo [emoji2]

Hata hivyo, nikiangalia mnyororo wa thamani uliopo kwenye hizi sherehe na ajira zilizozalishwa, nabaki kuona ni jambo zuri na lenye tija.

Ukichangia harusi, unatoa ajira kwa watu wengi sana. Kuanzia MC, watu wa mapambo, chakula, wapiga picha, maids, watoa burudani n.k.

Faida nyingine ni mzunguko wa fedha kuchochea uchumi wa eneo husika, kuimarisha undugu na ujamaa, kutengeneza kumbukumbu na mengine mengi.

Wapo wasiochangisha watu kwenye mambo ya sherehe, lakini hao ni wale wanaojiweza, vipi wale wasiojiweza?

USHAURI WANGU

Tusiache kuchangiana kama tunapendana na kushirikiana. Umoja ni nguvu. Sherehe za harusi sio suala binafsi tena, ni suala la kiuchumi na maisha ya watu wengi yanategemea hapo.

Mwezi wa 6 mwakani nafunga ndoa. Nitatoa kadi za michango. Mnichangie. Puuzeni maneno laini laini ya Hamisi.
Hata Mimi namuunga mkono ...sikuchangisha MTU harusi yangu.... Mkioana tuwachangie mnapoachana mnatuitaga kuchanga tushangilie kuachana kwenu !!?? Nilioa na sherehe nikafanya kwa kiwango cha kipato changu inatosha ..... Sikuacha madeni, magomvi kugombana na watu eti uliwachangia nao wakuchagie.... Ujinga sana
 
Back
Top Bottom