TANZIA Mwanachama wa JamiiForums & Mgombea Ubunge Lushoto(CHADEMA), Mohamedi Mtoi afariki ktk ajali

TANZIA Mwanachama wa JamiiForums & Mgombea Ubunge Lushoto(CHADEMA), Mohamedi Mtoi afariki ktk ajali

Du! Ni msiba mkubwa sana! kamanda tangulia mbele ya haki, sote twaja! poleni sana makamanda wote! ALUTA CONTINUA!
 
Kamanda Mtoi alikuwa kiongozi, mcheshi na mwenye hekima kubwa.
Huu msiba ni mkubwa na umetuhuzunisha sana.
Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahala pema.
 
Sikuwaza kupata taarifa mbaya kama hizi, ameenda mapema sana brother ukiwa unategemewa na wana Lushoto. R.I.P my homie
 
What exactly happened?

Sawa ni ajali, lakini ilitokeaje....tufahamishwe basis.

Gari imegonga mti? Imepinduka? Zimegongana uso kwa uso?

How? How?......kwa sababu huyu kamanda ni miongoni mwa wana JF ambao possibility yao kuingia bungeni ilikuwa ni over 90%!

Kwa kweli it pains, lakini hatuna jinsi. Kamanda katangulia mbele ya haki.

R.I.P kamanda....lakini tunakuhakikishia huko huko uliko, hamasa yetu ya mabadiliko nje ya CCM ndiyo imeongezeka zaidi!!

Aluta continua!
 
Nimeumizwa sana na kifo hiki!.

Ama kweli nimeamini yanayosemwa na watu, "wanaopendwa na wengi, hufa wangali vijana!".

Ila Tanga nako....!, na hizi ajali za kuelekea chaguzi!....

Nimeikumbuka ajali ya Marehemu Juma Jamaldin Akukweti, ambayo ilitokea kuelekea uchaguzi!, ilikuja kusemekana kuna mkono wa mtu katika kugombea jimbo!, na huyo mtumiwa, japo alilitwaa hilo jimbo, lakini hakuchukua round, tena yeye aliondoka kwa mateso makubwa!.

Kama ni ajali ya kawaida, Mungu amrehemu marehemu!, lakini kama ni mkono wa mtu, subirieni 'karma' reaction soon, karma haikopeshi wala haiongopi!.

Poleni sana wafiwa, poleni Chadema!, poleni wana jf, tumempoteza sio tuu mwana jf mwenzetu, bali mpashanaji habari mahiri!.

RIP Kamanda Mtoi!.

Pasco

inaumiza Sana
 
Mwehu baba yako aliyekufundisha adabu mbovu. Hapa topic ni msiba bangi na viroba mbele ya safari

usijitafutie umaarufu kwenye huu Uzi wa maombolezo. Anzisha Uzi wako ujimwage na matusi yako humo hatokuuliza MTU...
 
Saa nyingine unakataa kusikia hii habar lakini nimejiriridhisha KAMANDA huyu hatunaye. Kalale PEMA my school mate tutakuenzi kwa harakat zako za kupeleka upinzani nyumbani kwa ajili ya mabadiliko ya dhati.....Aisee inasumbua kichwa sana kuamini hili
 
R.I.P Pigo kwa Chadema na makamanda wapenda mabadiliko wote. Mtoi hakuwahi,hajawahi na hakuwa msaliti. Na alipambana mpaka tone la mwisho la damu yake. Mods kama itawapendeza na kama utaonekana umuhimu uanzishwe uzi maalum kwa ajili ya ku pay tribute kwa Kamanda Mtoi. Tujikumbus hebposts zake muhimu. Pia utaratibu wa kufikisha rambirambi kwa familia yake kama mwana JF.

indeed
 
Nimelia sana sana, tuliongea juzi. Kwanini afe yeye tu? Hapana aiseee. Nimelia sana tulikua pamoja, Mama yake ndio Mama yangu, familia yake ndio yangu, tukipokuwa shambalai tuliamua kuhamia wote kwenda Magamba school. Why?

pole sana kamanda
 
Japokuwa mimi si mwanachama wa CHADEMA lakini nilikuwa navutiwa sana na hoja zake ambazo zilikuwa ni za kweli makini, zenye uchambuzi wa kisayansi na madhubuti. Nilitaka sana ashinde ubunge ili mchango wake uweze kunufaisha Taifa kupitia bungeni. Hakuwa mdini alikuwa mzalendo wa kweli.

Kifo chake kimenihuzunisha sana.

Raha ya milele umpe ee bwana, na mwanga wa milele umuangazie, apumzike kwa amani Amen X 3
 
Back
Top Bottom