TANZIA Mwanachama wa JamiiForums & Mgombea Ubunge Lushoto(CHADEMA), Mohamedi Mtoi afariki ktk ajali

Du! Ni msiba mkubwa sana! kamanda tangulia mbele ya haki, sote twaja! poleni sana makamanda wote! ALUTA CONTINUA!
 
Kamanda Mtoi alikuwa kiongozi, mcheshi na mwenye hekima kubwa.
Huu msiba ni mkubwa na umetuhuzunisha sana.
Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahala pema.
 
Sikuwaza kupata taarifa mbaya kama hizi, ameenda mapema sana brother ukiwa unategemewa na wana Lushoto. R.I.P my homie
 
What exactly happened?

Sawa ni ajali, lakini ilitokeaje....tufahamishwe basis.

Gari imegonga mti? Imepinduka? Zimegongana uso kwa uso?

How? How?......kwa sababu huyu kamanda ni miongoni mwa wana JF ambao possibility yao kuingia bungeni ilikuwa ni over 90%!

Kwa kweli it pains, lakini hatuna jinsi. Kamanda katangulia mbele ya haki.

R.I.P kamanda....lakini tunakuhakikishia huko huko uliko, hamasa yetu ya mabadiliko nje ya CCM ndiyo imeongezeka zaidi!!

Aluta continua!
 

inaumiza Sana
 
Mwehu baba yako aliyekufundisha adabu mbovu. Hapa topic ni msiba bangi na viroba mbele ya safari

usijitafutie umaarufu kwenye huu Uzi wa maombolezo. Anzisha Uzi wako ujimwage na matusi yako humo hatokuuliza MTU...
 
Saa nyingine unakataa kusikia hii habar lakini nimejiriridhisha KAMANDA huyu hatunaye. Kalale PEMA my school mate tutakuenzi kwa harakat zako za kupeleka upinzani nyumbani kwa ajili ya mabadiliko ya dhati.....Aisee inasumbua kichwa sana kuamini hili
 

indeed
 
Nimelia sana sana, tuliongea juzi. Kwanini afe yeye tu? Hapana aiseee. Nimelia sana tulikua pamoja, Mama yake ndio Mama yangu, familia yake ndio yangu, tukipokuwa shambalai tuliamua kuhamia wote kwenda Magamba school. Why?

pole sana kamanda
 
Japokuwa mimi si mwanachama wa CHADEMA lakini nilikuwa navutiwa sana na hoja zake ambazo zilikuwa ni za kweli makini, zenye uchambuzi wa kisayansi na madhubuti. Nilitaka sana ashinde ubunge ili mchango wake uweze kunufaisha Taifa kupitia bungeni. Hakuwa mdini alikuwa mzalendo wa kweli.

Kifo chake kimenihuzunisha sana.

Raha ya milele umpe ee bwana, na mwanga wa milele umuangazie, apumzike kwa amani Amen X 3
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…