Afyayaakili
JF-Expert Member
- Sep 12, 2012
- 924
- 1,263
Mwanachuo Udom jela miaka sita
By Hadija Jumanne, Mwananchi
Imewekwa Friday, September 26 2014 at 09:45
Dar es Salaam. Mahakama ya Wilaya ya Ilala imemhukumu kifungo cha miaka sita jela, Melkiad Kabunduguru(28) baada ya kupatikana na hatia ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kukutwa na noti bandia.
Kabunduguru ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma(Udom) atatumikia kifungo hicho baada ya Mahakama kuridhika na ushahidi uliotolewa dhidi yake.
Katika shtaka la kwanza la Kabunduguru atatumikia kifungo cha miaka minne baada ya kupatikana na hatia ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu huku shtaka la pili la kukutwa na noti 50 za bandia za Sh5000 mshtakiwa atatumikia kifungo cha miaka miwili.
Akisoma hukumu hiyo jana, Hakimu Juma Hassani alisema mshtakiwa atatumikia vifungo hivyo kwa pamoja baada ya Mahakama kuridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani.
Akitoa hukumu hiyo jana, Hakimu Juma Hassani alidai kuwa mshtakiwa huyo atatumikia kifungo hicho ili iwe fundisho kwa vijana wengine wenye tabia za wizi.
Kabla ya kutoa hukumu hiyo, upande wa Jamhuri ukiongozwa na Mwendesha mashtaka, Felista Mosha uliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mshtakiwa ili iwe fundisho kwa vijana wengine wenye tabia za udanganyifu.
By Hadija Jumanne, Mwananchi
Imewekwa Friday, September 26 2014 at 09:45
Dar es Salaam. Mahakama ya Wilaya ya Ilala imemhukumu kifungo cha miaka sita jela, Melkiad Kabunduguru(28) baada ya kupatikana na hatia ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kukutwa na noti bandia.
Kabunduguru ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma(Udom) atatumikia kifungo hicho baada ya Mahakama kuridhika na ushahidi uliotolewa dhidi yake.
Katika shtaka la kwanza la Kabunduguru atatumikia kifungo cha miaka minne baada ya kupatikana na hatia ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu huku shtaka la pili la kukutwa na noti 50 za bandia za Sh5000 mshtakiwa atatumikia kifungo cha miaka miwili.
Akisoma hukumu hiyo jana, Hakimu Juma Hassani alisema mshtakiwa atatumikia vifungo hivyo kwa pamoja baada ya Mahakama kuridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani.
Akitoa hukumu hiyo jana, Hakimu Juma Hassani alidai kuwa mshtakiwa huyo atatumikia kifungo hicho ili iwe fundisho kwa vijana wengine wenye tabia za wizi.
Kabla ya kutoa hukumu hiyo, upande wa Jamhuri ukiongozwa na Mwendesha mashtaka, Felista Mosha uliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mshtakiwa ili iwe fundisho kwa vijana wengine wenye tabia za udanganyifu.