Mwanadamu pia ni Mungu

Mwanadamu pia ni Mungu

kwisha

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2021
Posts
1,779
Reaction score
4,982
Katika pita pita zangu, nimekutana na hoja ya pasta mmoja wa Kenya akisema kuwa kuna Mungu na pia kuna miungu, na miungu ni sisi wanadamu. Watu walicheka sana na kumuita mnafiki.

Kuna watu wengi wanashindwa kuelewa maana ya neno Mungu. Wanafikiri Mungu (Allah) ni jina la Yehova au Yahweh. Neno Mungu lina maana nyingi sana, lakini maana yake kuu ni "mwenye uwezo." Pia, neno Mungu lina asili kama lilivyo neno mwanadamu. Neno Mungu linarejelea yule aliye juu ya yote.

Swali langu rahisi likawa, kama mtu kwa kufanyika mwanadamu anachukua asili ya kibinadamu (anaitwa mwanadamu), je, mtu kwa kufanyika Mungu aitwe nani? Na achukue asili ya nani?

Hoja yangu siyo hiyo; hoja yangu ni kwamba mwanadamu anastahili kuitwa Mungu. Tukienda katika maandiko matakatifu, Yesu alimuita Shetani "Mungu wa dunia." Kwanini? Kwasababu ya uwezo na nguvu za Shetani, ndiyo maana anaitwa Mungu wa dunia. Je, Yesu alikufuru? Hapana.

Kwanini basi mwanadamu mwenye uwezo naye asiitwe Mungu?
 
Katika pita pita zangu, nimekutana na hoja ya pasta mmoja wa Kenya akisema kuwa kuna Mungu na pia kuna miungu, na miungu ni sisi wanadamu. Watu walicheka sana na kumuita mnafiki.

Kuna watu wengi wanashindwa kuelewa maana ya neno Mungu. Wanafikiri Mungu (Allah) ni jina la Yehova au Yahweh. Neno Mungu lina maana nyingi sana, lakini maana yake kuu ni "mwenye uwezo." Pia, neno Mungu lina asili kama lilivyo neno mwanadamu. Neno Mungu linarejelea yule aliye juu ya yote.

Swali langu rahisi likawa, kama mtu kwa kufanyika mwanadamu anachukua asili ya kibinadamu (anaitwa mwanadamu), je, mtu kwa kufanyika Mungu aitwe nani? Na achukue asili ya nani?

Hoja yangu siyo hiyo; hoja yangu ni kwamba mwanadamu anastahili kuitwa Mungu. Tukienda katika maandiko matakatifu, Yesu alimuita Shetani "Mungu wa dunia." Kwanini? Kwasababu ya uwezo na nguvu za Shetani, ndiyo maana anaitwa Mungu wa dunia. Je, Yesu alikufuru? Hapana.

Kwanini basi mwanadamu mwenye uwezo naye asiitwe Mungu?
Ni sawa mbona kunawanadamu wengi walikua miungu. Unamjua Nimlodi?
Mungu ni jina la cheo tuh, kuna watu walichonga miti wakaifanyia nakshinakshi wakasema ndo mungu wao wakaiinamia, wakaiabudu.
Kuna jamii zimetengeneza miungu ya dhahabu, miungu ya mawe na wanafanya ibada safi kabisa.

Mungu muumba ye hakufanywa na wanadamu, na sisi sote ni mali yake, amejitofautisha na miungu mingine kwa kujipa Jina Yehova. Kwakua kila mungu anajina lake.
Ibada zakuabudu watu au vitu, Yehova anaiita ibada ya sanamu na hapendezwi na ibada za aina hiyo. Kwakua yeye ndo alieumba kila kitu.
 
Back
Top Bottom