Aliye post hii thread yaonekana ni mwanafunzi wa hiyo shule, na tabia za ubakaji mashuleni zipo. Bila watu kama huyu kusema wazi tutajuaje ili vyombo husika visaidie haki ipatikane?
Hajatumia JF kuchafua heshima ya watu, bila kutaja jina la muathirika, vyombo vya dola vitaanzia uchunguzi? Unless wewe ni mmoja wa hao wabakaji sasa unaogopa kwa kuwa limesanuka na kuwekwa wazi.
Mleta mada, naomba ufunguke zaidi kama suala hili lilifikishwa kwa waalimu na je waalimu walifanya nini baada ya kupata taarifa.
Wana JF tusipende kutumia matusi kama kinga ya maovu yetu ili tusisemwe.