Mwanafunzi aliyehitimu kidato cha nne 2012 akutwa akisimamia ujenzi wa zahanati- Bukombe

commited

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2012
Posts
1,624
Reaction score
871
Mwanafunzi aliyehitimu kidato cha nne (2012), amekutwa akisimamia ujenzi wa zahanati ya wilaya ya Bukombe-Mkoani Geita.
ALipoulizwa kwa nini linta imepinda alijibu ni kwa sababu ya mbao zilizotumika zimepinda,

Mwenyekiti wa sisiemu katika wilaya hiyo, amesema haya ndiyo mambo yanaizamisha sisiemu shimoni...


Hapa ndipo tulipofikia watanzania....
CHANZO: TAARIFA YA HABARI, ITV (SAA 2.USIKU, 20/07/2013)
 
Baada ya Paul kagame kudai kwamba majeshi yanayolinda amani congo kuwa na mpango wa kushirikiana na wapinzani wake ili waishambulie Rwanda sasa imechukua sura mpya baada ya umoja wa mataifa kumwandikia barua kumtaka athibitishe madai hayo.itakumbukwa kwamba huyu jamaa amekukuwa akitapa sana kumtafutia wa kumfia siku za hivi karibuni.pengine tutasema ameona vyanzo vyake vya uharifu wa kuiba madini ya congo vimezibwa na sasa hana chakufanya na tarafa yake ya rwanda.
Source; redio one
 
Sijaelewa mwanafunzi kusimamia ujenzi, Lenta kupinda na mambo yanayoizamisha Sisiemu.. Ufafanuzi tafadhali
 
wewe nyumba yako ilisimamiwa na nan?.mbona wabunge wengi ni form 4 na dogo amevaa gwanda la chadema
 
Sijaelewa mwanafunzi kusimamia ujenzi, Lenta kupinda na mambo yanayoizamisha Sisiemu.. Ufafanuzi tafadhali

dogo wa bavicha na yupo jimboni kwa profesa kahigi chadema .magwanda
 
Engineer wa mkoa ameulizwa ni kwa nini anadai eti mkoa mzima hawana mafundi walisomea kwa hiyo wanatumia Local Fundis hicho kiingereza sikukielewa
 
Kagame ni mchovu tu mbona inajulikana bila kuiba madini ya Congo hamna uchumi wa Rwanda ndo maana anaichelea amani ya Mashariki mwa congo,nakumbuka alishawahi kuwekewa vikwazo na umoja wa mataifa pamoja na uingereza na Marekani kwa kushiriki kuvi support vikundi vya uasi vya congo(kwa wale wanofuatilia intern news) mwaka jana ndo mana hata kidogo hawezi mpenda Jakaya kwa sababu anamzuia kufanya yake Congo ,sema wabongo wengi ni wepesi wa kusahau na sometimes wanapenda ushabiki usiokuwa na tija katika masuala ya kitaifa!!

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Si habali mpya hiyo mbona kuna waliopata maziro na wamo BOT wakati tulioscore A tukihaha kutafuta kazi mpaka kesho. Tabia yao hiyo CCM.
 
Yaani wanachekesha kama sio kufurahisha.ccm pia inalaum watendaji wa mtaa
 
Kweli serikali yangu sikivu imeshindwa kusimamia sera na talatibu za ujenzi hasa kwa majengo ya serikali .kilicho nishangaza leo, mhitimu wa kidato cha nne asimamia ujenzi wa jengo la zahanati uko Geita. Kwa hali hii sijuwi ubora wa majengo ya umma kama unazingatia talatibu na sheria zilizowekwa.

Source ITV Habari
 
Dogo kapata mchongo safi sana Mulugo+kawambwa products-mpambanaji

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Kumbe nilisikia vizuri tu! Duh.. kwa mwendo huu wa Local Fundis mbona hospital zinapaswa kuwa nyingi, maana ajali za kubomoka majengo mbona zitaongezeka!@ Wa kusoma




Engineer wa mkoa ameulizwa ni kwa nini anadai eti mkoa mzima hawana mafundi walisomea kwa hiyo wanatumia Local Fundis hicho kiingereza sikukielewa
 
Dogo alnfanya nikacheka, et mbao ndio zmepindsha ukuta! Da! Alkuwa anapga ela, dili limeshatibuka!
 
Msishange sana! Bora hata huyu aliyefika Kidato cha Nne (hata kama alipata 0) kwani kuna habari ya kwamba miongoni mwa ajira 30 pale Bandarini, kuna mtu mwenye Elimu ya Darasa la Saba, na amepewa kitengo nyeti.
Nchi kuna wasomi wengi wasio na kazi, hapo hapo kuna watu wanafanya uhalifu hadharani kwa kuwa wapo chini ya mtu fulani.
Amini nawaambieni, ukipita ufagio wa chuma, kuna ofisi kadhaa za umma zitabaki wazi bila ya watumishi.
 
Kilichonichekesha ni yule nadhani Mhandisi Mkuu wa Wilaya ya Bukombe kusema kuwa hawajapata mafundi wenye vyeti kama waliosoma VETA ndo maana wameamua kuwatumia hao LOCAL FUNDIS.. Akiwa na maana kwamba FUNDIS ni PLURAL FORM ya FUNDI...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…