Mwanafunzi atengeneza gari linalotomia umeme jua, asema alitamani kuendesha gari ya bei nafuu tangu utotoni

Jackal

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2012
Posts
9,971
Reaction score
13,608
Mwanafunzi mmoja huko Eldoret, Kenya anayefahamika kama Samuel Karumbo ametengeneza gari inayotumia umeme wa jua.

Samuel anasema tangu utotoni amekuwa akitamani kuendesha gari ya bei nafuu.

Gari hio inatembea kilomita 50 kwa siku na ameiomba Serikali iwekeze zaidi kwenye ubunifu.
 
SAFI SANA.
Huyu ni zaidi ya zile assembly plants za kina Volvo Nissan etc
 
Linakwenda km 50 kwa siku
 
Huu ndio ubunifu mtu anakuja na kitu ambacho hakipo kabisa sio wale wabongo wenzangu wanachukua engine ya bajaji au diesel engine na kuzitengenezea bodi na kusema wametengeneza helcopta au gari, au wale wanachukua sumaku na ma diode ya redio na kusema wametengeneza kituo cha kurussha mawasiliano ya redio
 
Ungeweza kumpa credit zake jamaa bila kulazimika kuwaponda wengine bado ukaeleweka.. Unawaponda hao wengine kwani huyu hiyo solar panel kaiunda mwenyewe au nae kachukua ya wenzake?

We unahisi anaechukua engine ya bajaj akaunda helcopta ikipaa anakua hajatumia akili au hizo diode za redio akatengeneza kituo cha redio anakua hajatumia akili?
Jifunze kuthamini ubunifu wa mwenzako as long as haauna athari hasi kwa jamii ndo tabia ya kiume
 
SAFI SANA.
Huyu ni zaidi ya zile assembly plants za kina Volvo Nissan etc

Huwa zinakuuma sana kuona Tanzania hawaji kufanyia huko, wanapita na kwenda Rwanda.
 
Ni kweli mkuu,big up!
 
Mbona wakenya humu JF hawamsifii huyu jamaa?
 
Yaaa bora umemwambia yy anafikir uyo jamaa vyote kaviunda yy?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…