Mwanafunzi aumizwa vibaya baada ya kuchapwa fimbo 20 na walimu 6 Jangwani Sekondari

Mwanafunzi aumizwa vibaya baada ya kuchapwa fimbo 20 na walimu 6 Jangwani Sekondari

Mimi sikubaliani na adhabu ya fimbo kama ndio njia ya kutatua tatizo,mbona international school hawana huo ukiritimba na wanafanya poa zaidi ya wanaochapwa viboko 20+
International school Kuna mlinzi anaekagua mizigo ya wanafunzi wanapoingia shuleni, shule Zina fance kwahiyo hakuna kuvusha sim kimagendo. Maadili ya watoto yanaimarika kutokana na kutochangamana na Jamii Mara kwa Mara maana mtoto anakua shule likizo twisheni kwahiyo Hana muda na Jamii. Lakini bweni zetu hizi tunazijua wenyewe,

Watoto wanakua bweni likizo nyumbani na mtaani. Kwahiyo vurugu zote anakumbana nazo na zinamteka so akienda shule anataka aziendeleze.
 
  • Thanks
Reactions: Sax
Kumbe kufanyiwa ukatili ni sifa?

Ulivuliwa mpaka chupi?
sio ukatili, kuna umri ambao tabia ya mtoto isipokuwa regulated ataharibikiwa, leo kupitia walimu hao walivyonirekebisha nawakumbuka hadi leo kwani nisingekuwa nilivyo leo
 
Walimu 6 wa Jangwani Sekondari jijini Dar es salaam wamemhukumu kwa kumchapa makalioni fimbo 20 mwanafunzi wa kike wa kidato cha tatu na kumjeruhi vibaya kwa tuhuma za kuwa alionekana ameshika simu.

Mwalimu aliyesema hivyo alimvua nguo na kumpekua kila mahala na hakukuta simu. Alimchukua hadi ofisi ya walimu na kumlazimisha akiri lakini alikataa ndipo walimu 6 wakamshushia kipigo cha fimbo 20.

Mmoja alimchapa 5 wawili 4 kila mmoja, mmoja 3 na wawili 2 kila mmoja. Wapo walimu wa kiume na wa kike waliofanya kipigo hiki. Alipoona kipigo kina zidi aliropoka kuwa yeye hana simu bali aliye na simu ni mwenzake.

Huyo aliyetajwa kachukuliwa hatua japo mzazi alikuja kukiri binti yake kuwahi kuwa na simu.

Huyu binti aliyechapwa alihamishiwa shuleni hapo na kuishi bweni akitokea mkoani kutokana na tatizo la kiafya. Hali hiyo bado ilikuwa inamsumbua na zipo kumbukumbu katika hospitali za Dar na huko alikotoka lakini baadhi ya walimu wanasema anajifanyisha hivyo kushindikiza atolewe bweni azma ambayo wameipitisha pamoja na hicho kipigo.

Tatizo jingine ni imani kwa kuwa jitihadi za kumbadili kupitia ugonjwa zilipo shindikana wanasema haumwi.

Wapo wanafunzi walibadilishwa na kwenda upande wa hao walimu.

Tunaomba TAMISEMI, Polisi na Wizara ya Wanawake, Jinsia na Watoto wafuatilie suala hili. Huyu binti ni mgonjwa sasa akiwa mwanafunzi wa kutwa akipata tatizo njiani nani wa kuwajibika.

Mtoto wa kike anadhalilishwa fimbo 20 shule tena kwenye makalio.

Tupaze sauti.
Taabu
 
Wewe ndio ufuatilie maana mimi hutonidanganya kuhusu kayumba au international, nishapita kwote huko. Mbona mashoga wengi wanatokea mitaa ya waswahili kwa wingi ambako wanatokea watoto wengi wa kayumba?
Hawa watu wako delusional sana [emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Kuna mmoja hapo juu anasema alifurahia kupewa kipigo cha kikatili ikiwemo na kuingiziwa vidole mkunduni na kuchaniwa kaptula.

Huwezi amini mtu anafurahia kutwezwa utu wake. Anaona ni sifa sijui. [emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Duuh.
 
sio ukatili, kuna umri ambao tabia ya mtoto isipokuwa regulated ataharibikiwa, leo kupitia walimu hao walivyonirekebisha nawakumbuka hadi leo kwani nisingekuwa nilivyo leo
Vipi kuhusu madole waliyokuingizia mkunduni? na chupi wakakuchania!

Hiyo nayo ni moja ya njia ya kujenga maadili?
 
Wewe ni mzazi, mwanafunzi mwenzake, jirani au kiongozi? Fimbo 20 ndo zakugungua Uzi, watu tulikula fimbo 40 + kukata kuni meta mbili mbili na shule iliendelea.
Walimu wa sasa wana huruma
Wa zamani mwanafunzi.akiitwa kupigwa viboko anaacha hadi wosia kabla ya kipigo kueleza wenzie akifa daftari zake arithi nani.Sababu eneo la viboko chochote chaweza tokea

Hiyo ilisaidia utukutu kukoma mashuleni na watoto kusoma
 
Sasa hivi una muona hana akili, ila subiri mamlaka zichukue hatua ndiyo utajua kuwa jamaa ana akili au hana akili. Au subiri huyo mwanafunzi apatwe na madhila mabaya zaidi ndiyo utajua reaction ya watu. Atakaye teseka ni mwalimu/walimu waliohusika na hilo tukio. Walimu sijui hawajifunzi kutokana na matukio ya siku za nyuma. Pia nyakati zimebadilika sana. Kila kimebadilika sana, na mabadiliko huwezi kuyazuia wewe. Suala la fimbo sikatai ila fimbo 20 hapo Hapana. Times have changed. Hatuwezi kuendelea kuishi kwa kutumia akili na nadharia za karne ya 20. Sasa hivi ni karne ya 21 kaka. Dunia imebadilika kwenye kila eneo pamoja na kwenye namna ya kutoa adhabu. Sasa wamemchapa huyo mwanafunzi, nini wamenufaika? Na hii habari aliyoanzisha huyo jamaa itaelea kama upepo. Huna uwezo wa kuzuia siku hizi kutoa habari kwa sababu kila mmoja amepewa platform ya kutoa habari. Wasalam
Aisee, kwa mujibu wa maelezo ya mtoa mada baada ya mwanafunzi kupigwa ndoakasema Simu niyanani na ipo wapi.

It means kabla ya kupigwa hakuwa tayari kusema Simu iliko.

Mwanafunzi huyo kuwa nasimu shuleni watakaolaumiwa ni walimu kwa usimamizi mbovu, walimu hao wakitoa adhabu ili kukomesha iyo tabia wanaonekana wamekosea.

Nikuulize Swali jepesi,
Umeshawashutumu walimu wamekosea sasa tuambie Ungekuwa wewe ungefanyaje?

Ungemchapa fimbo mbili utegemee akwambie iliko simu?

Ungembembeleza akwambie

Ungemfukuza shule ili akawe malaya vizuri.

Ungefanya nn?
 
Aisee, kwa mujibu wa maelezo ya mtoa mada baada ya mwanafunzi kupigwa ndoakasema Simu niyanani na ipo wapi.

It means kabla ya kupigwa hakuwa tayari kusema Simu iliko.

Mwanafunzi huyo kuwa nasimu shuleni watakaolaumiwa ni walimu kwa usimamizi mbovu, walimu hao wakitoa adhabu ili kukomesha iyo tabia wanaonekana wamekosea.

Nikuulize Swali jepesi,
Ungekuwa wewe ungefanyaje?
Kwanini mwanafunzi kuwa na simu ni uhalifu?

Hilo nalo la msingi tuanze nalo!
 
Nikiwa kidato cha pili, niliwahi tembezewa stick 47 (Arobaini na saba) hadi nikazima maksudi staff. Reasons ni hizi.

1. Wizi wa attendance register uliokithiri.
2. Kutongoza Waalimu wa kike. (Wote walikua wanachomoa [emoji23]
3. Wizi wa viazi, mahindi ya kuchoma, karanga mashambani kwa walimu.
4. Kwenda shule nimelewa na kuvuta sigara.
5. Utoro sugu.

Ila Mungu alivyo, nina Bachelor's Degree ya Education. Hatari.
Bila hizo bakora ungekuje sasa! Vipi ukikuta mwanafunzi anafanya hayo kama Mwl unajisikiaje!
 
Unafananisha wanafunzi wa International na hawa wa kayumba?Una safari ndefu sana kujikomboa kifikra.Pole sana bro
How wa international wana sauti kuliko Mwl, akifanya kosa anaitwa mzazi kuambiwa mwanao hajaandika juzi wala kufanya maswali upo!
 
Hili nalo unataka ujibiwe??????? Mchana mwema.
Jibu swali, acha ubabaishaji.

Ndio maana walimu mnaonekana kama irrational psychopaths tu.

Hauwezi hata kueleza kwanini simu ni haramu, lakini unajua tu kupiga wanafunzi marungu.

Unapaswa kuwa na HEK'MA, sio unaenda enda tu kama zombi.
 
Jibu swali, acha ubabaishaji.

Ndio maana walimu mnaonekana kama irrational psychopaths tu.

Hauwezi hata kueleza kwanini simu ni haramu, lakini unajua tu kupiga wanafunzi marungu.

Unapaswa kuwa na HEK'MA, sio unaenda enda tu kama zombi.
Kwahiyo Mwalimu akifundisha watoto wawe wanachat darasani au wanapokea simu......halafu wakiferi muanze laumu walimu wanakula mishahara ya bure

Utterly nonsense tena unaonekana kama una bipolar mkuu
 
halafu wakiferi muanze laumu walimu wanakula mishahara ya bure
=WakifeLi.

Kuandika kwenyewe hujui, si ajabu hiyo shule unayoFUNDISHA unawajaza tu watoto wetu ujinga.

Pole mwalimu. Hizi sio zama za kuchapana kama wanyama.

Kuna UTARATIBU.
 
=WakifeLi.

Kuandika kwenyewe hujui, si ajabu hiyo shule unayoFUNDISHA unawajaza tu watoto wetu ujinga.

Pole mwalimu. Hizi sio zama kuchapana kama wanayama.

Kuna utaratibu.
hahaha mwalimu hajui tofauti ya L na R
 
Back
Top Bottom