Mwanafunzi Wangu Amenitoa Machozi

Mwanafunzi Wangu Amenitoa Machozi

Poleni walimu. Ila matatizo haya huwa mnajitakia wenyewe, yaani nyie kila mwaka wa uchaguzi hamkomi kutumiwa katika kampeni halafu mnaachwa huku mkiamini mambo yatabadilika. Tokea 1995, 2000,2005 and 2010, hamchoki tu!
Mko wengi na mna ushawishi katika jamii kama mkitumia nafasi zenu vizuri.
Kumbukeni, mliyempigia kura mara mbili ameshawaambia hayo madai yenu hayawezekani kabisaaaaaa!
Amkeni bana!

Nijuavyo walimu wengi wana mawazo huru na si rahisi kutumika. Hata hivyo katika kundi kubwa kama hili tutarajie si rahisi wote kuunga mkono wazo na mtizamo mmoja. Jamani tuendelee kuwaelimisha wale ambao bado hawajabadilika.
 
pole sana Mwalimu endelea kuwa mpole tu kama jina lako, iko siku MUNGU atasikia kilio cha waja wake
 
Mwalimu analalamika huku amevalia tshirt ya CCM iliyoandikwa "Maisha bora kwa kila Mtanzania".
 
CCM OYEEEE!.... CWT OYEEEE!.... TUCTA OYEEE!.... Asanteni sana, muda unakwenda namkabidhi MC aendelee.
 
mtajipoza na per diem ya tsh.35,000 za sensa kwa siku 14, si haba, serekale haina hela, kama hutaki kawe kibaka.
 
Oh poor teacher. I am sorry too. Lakini miaka miwili na nusu sio mbali, msijisahau.

Shida yao wakipewa posho la kuandikia daftari ya wapiga kura na kusimamia uchaguzi, wanasahau shida za miaka mitano iliyopita. Wacha wanyanyaswe tu hawana maana hawa ni makondoo full mtindo!
 
Poleni walimu. Juzi nilisafiri na Dc na DED wa halimashauri fulani njiani ilikuwa ni full kuwabeza walimu mara oh cwt wanaponza walimu ili kuwasahaurisha makato wanayokata kwenye mishahara ya walimu. Vilevile walimu wamezidi mno kukopa sehemu nyingi na kiasi kinachozidi mishahara yao. Kwa hiyo serkali itaanza kutrain watu wa makamo ili vodafasta wanaposumbua hao wazee wakabelof.My take: serkali itakuwa inafanya mambo ya dharula mpk lini?
 
Nyie si ndio baadhi yenu ni vinara wa kuisaidia CiCiMizi kuiba kura? Mshahara wa dhambi ni mauti. Mpaka mtakapojua kuwa CiCiMizi anawatumia kutenda dhambi, ndipo Mungu atasikia kilio chenu. Walimu wengi, hasa wa kike, ni wasaliti wa watanzania. Tatizo ni kuwa walimu wengi wa kike wameolewa na wenye nazo (mfano mzuri ni Teacher Salma na Mama Maria Nyerere).
Heshima yako Mkuu Kashaijabutege. Ila hapo kwenye Bold nahisi kama hujatenda haki, labda kama sio Mama Maria Nyerere ninayemfahamu mimi.
 
Last edited by a moderator:
Pole mwalimu, lakini ukweli unabakia kuwa fimbo ya mnyonge ni umoja. Walimu wangekuwa wamoja, Nchi hii ingekuwa mbali sana kimaendeleo.
 
Mbona umetoa maswali(zoezi) wakati umefundisha methali moja tu?

sasa hivi ndo hivo hivyo mpaka kieleweke methali moja zoezi hadi mwezi ujao,mara mtihani wa mwisho huo,mtoto anaandika bongo fleva kweli kazi ipo.
 
Hadithi nzima niya kuchonga kwa kuangalia uhalisia wa mazingira ya mwalimu na mwanafunzi wawapo shuleni hasa mwalimu anapokuwa anaingia darasani . Japo ukweli ni kwamba walimu hawalipwi vizuri.

Wanafunzi wa siku hizi wamepinda sana aisee.unaweza ukaambiwa kitu na mwanafunzi wa drs 4 mpaka ukashindwa hata kusema neno.Huenda kuna ukweli jambo kuinogesha imo mdau
 
Kaza moyo mwl mwenzangu wafundishe watoto m4c nao wamjue adui yetu ni nani hasa.2015 kinaeleweka mia.
 
pole mwalimu wangu,nami imeniuma sana hapa maana ninajua mliponitoa.
hawa watoto pengine walisikia hotuba ya mkuu wa nchi alivyowaponda,kuwa ualimu si muhimu kwani ata mikiacha kufundisha mitaala itabaki watakuja wengine.
mtoto hapo amewafungua macho dawa ni kuungana tu kudai haki yenu tena barabara.
tena mimi ninakushangaa bado una hamu ya kufundisha mpaka unatoa na zoezi? masikini wenzio walishaacha siku nyingi japo kweli mnaangamiza taifa la watu wa chini na kutoa nafasi kwa vitoto wa vigogo wanasoma shule nzuri au nje ya nchi kuendelea kututawala!.
Mimi nikupe dawa ya tatizo mwalimu
1.acha kupigia kura CCM
2.acha kutumiwa na serikali wakati wa uchaguzi
3.wafundishe watoto adui wao na kuwachukia viongozi wezi ikiwezekana nenda mbali wafundishe ata kupora mali za viongozi mafisadi ili kurejesha ata nusu ya zile walizo iba.
4.hamasisha waalimu wenzako kuingia barabarani kudai haki yenu maana mezani hamtapata kamwe hawa viongozi mliowaweka madarakani hawana huruna nanyi kabisa.
pole mwalimu wangu
 
Aiseeeeeee nimemwonesha mama yake rakurwa haya maelezo kasheka sana kasema kesho atamwadisia shost yake mke wa bonifasi
 
Threshold yangu ya huruma huwa iko mbali lakin leo nimejisikia kuguswa. Methali ya Hamisi ina maana kwenu.
 
Heshima yako Mkuu Kashaijabutege. Ila hapo kwenye Bold nahisi kama hujatenda haki, labda kama sio Mama Maria Nyerere ninayemfahamu mimi.

Mkuu Gerrard kwa kipindi hicho Mwalimu Nyerere naye alikuwa miongoni mwa "waliokuwa nazo"; ingawa sina maana ya kwamba alikuwa fisadi. Maana yangu ni kuwa hata Mama Maria Nyerere naye hakupata ile "pinch" ya ualimu waliyoipata walimu wa nyakati zake. Yes, Nyerere hakuwa fisadi, lakini ile kuwa Rais tu ilimfanya Mama Maria asionje machungu halisi ya ualimu. Ukweli unabaki pale kuwa walimu wengi wa kike, ambao hutamba na magari na majumba ya kifahari ya waume zao, ni wasaliti counterparts wao, yaani walimu wa kiume.
 
  • Thanks
Reactions: SG8
Back
Top Bottom