Mwanajeshi Mstaafu wa Marekani adai Nchi za Afrika zirudishwe kwenye Utawala wa Kikoloni kwa kushindwa kujisimamia zenyewe

Mwanajeshi Mstaafu wa Marekani adai Nchi za Afrika zirudishwe kwenye Utawala wa Kikoloni kwa kushindwa kujisimamia zenyewe

Mhaya

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2023
Posts
1,831
Reaction score
5,489
Erik Prince, afisa wa zamani wa Jeshi la Wanamaji la Marekani na mwanzilishi wa kampuni ya binafsi ya kijeshi ya 'Blackwater', hivi karibuni alitoa maoni yake kwamba nchi za Kiafrika zinapaswa kurudishwa kwenye ukoloni kwa sababu viongozi wake wana ufisadi na ubinafsi.




Prince alitoa mtazamo huu katika klipu fupi iliyochapishwa kwenye mtandao wa X na ‘Africa Facts Zone,’ akipendekeza kwamba ikiwa mataifa ya Afrika yanashindwa kujitawala, ni wakati wao kuvamiwa tena.

"Ni wakati wetu wa kurudisha kofia ya kifalme na kusema tutatawala hizo nchi ikiwa hazina uwezo wa kujitawala... Unaweza kusema Afrika nzima hawana uwezo wa kujitawala na kunufaisha raia wao kwa sababu viongozi wa serikali zao wanapora mali na kuziweka kwenye mifuko yao kisha wanakwenda kufanya manunuzi (kula bata) katika mji wa Paris, nchini Ufaransa badala kusaidia raia wake" Erik Prince Alisema.

Kwa mtu kama Erik Prince ambaye amewahi kuhudumu katika nafasi ya juu ya jeshi la wanamaji nchini Marekani na kuwa mwanzilishi wa kampuni binafsi ya kijeshi (Blackwater) kuzungumza kauli kama hii inaweza kuwa tishio kwa serikali za Afrika na raia wake hata kama alipitiwa katika mazungumzo.

Licha ya nchi za Afrika kuwa na mapungufu yake kama ilivyo kwa nchi zingine duniani haitoi uhalali kwa nchi za magharibi kurudisha ukoloni wao katika bara hilo kwani ni kinyume na mkataba ulioazimiwa mwaka 1960 na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu kuondoa ukoloni na kuziacha nchi zote duniani kujitawala na kuwa wamiliki halali wa maliasili zao.

Nini maoni yako kuhusu kauli ya Erik Prince?
 
Wapigania uhuru waliwapotosha waafrika.
Walipigania maslai yao binafsi na sio ya waafrika wote thus baada ya uhuru wapigania uhuru na familia zao ndio wanafaidi matunda ya Uhuru
Waafrika wote wana mapungufu ya akili kichwani, sio suala la wapigania uhuru pekee.

Taja jambo moja la maana ambalo Waafrika tunaongoza, ukichana na kushikwa nyege. Sasa unalaumu wapigania uhuru wakati race nzima mbovu kiakili
 
Bora ya wakoloni kuliko wawekezaji wawekezaji ni wezi wakoloni walikuja kuijenga Africa sema wapigania uhuru hawakuwaelewa wakoloni walibase kwenye upande wa negative zaidi kuliko faida ya ukoloni Africa
 
Waache unyonyaji wao wa nguvu kupitia World Bank,IMF na World Trade Order.Uliona wapi mteja anapanga bei ya mali ghafi?
Wakiona viongozi wanazungumza kuhusu Pan Africanism watafanya kila njama wapindue huo utawala na kuweka vibaraka wao kwa kutumia CIA.Mifano ni mingi tokea enzi za Patrice Lumumba,Kwame Nkrumah,Samuel Doe na miaka ya karibuni Muamar Gadaffi.
Kijana mwanamapinduzi Ibrahim Traore wa Burkina Faso ameonyesha njia tutarajie wamuache.
Ruto alijaribu kujitutumua ameitwa na kutishiwa ameufyata.Huwezi kumsikia tena akifungua mdomo kuhusu utumiaji wa dola wala unfair World Trade Order.
Nchi 10 zilizokuwa chini ya utawala wa Ufaransa zimechukua hatua ya kujitoa kwenye mkataba wa unyonyaji wa kutuma mapato yao Ufaransa.Na Ufaransa iwagaie inavyoona sawa.
Umoja wa Afrika (AU) akianza kiongozi yeyote kuzungumzia Umoja wa kiuchumi anapigwa vita haraka sana.
Marekani na huyo mwanajeshi ni mamba.Tokea lini mamba akamuonea huruma anayemuwinda na kutaraji Kumla?
 
Let them come!

Itakuwa bora na nafuu kwa mlala hoi kuliko mkoloni mweusi asiye jali maslahi ya wenzake.
 
Mbona wazungu wakitupa msaada mfano wa kujenga barabara, kwa nini fedha zinafujwa na viongozi mpaka wasimamizi na barabara inajengwa chini ya kiwango kama kweli tuna uwezo wa kujitawala?
 
Waache unyonyaji wao wa nguvu kupitia World Bank,IMF na World Trade Order.Uliona wapi mteja anapanga bei ya mali ghafi?
Wakiona viongozi wanazungumza kuhusu Pan Africanism watafanya kila njama wapindue huo utawala na kuweka vibaraka wao kwa kutumia CIA.Mifano ni mingi tokea enzi za Patrice Lumumba,Kwame Nkrumah,Samuel Doe na miaka ya karibuni Muamar Gadaffi.
Kijana mwanamapinduzi Ibrahim Traore wa Burkina Faso ameonyesha njia tutarajie wamuache.
Ruto alijaribu kujitutumua ameitwa na kutishiwa ameufyata.Huwezi kumsikia tena akifungua mdomo kuhusu utumiaji wa dola wala unfair World Trade Order.
Nchi 10 zilizokuwa chini ya utawala wa Ufaransa zimechukua hatua ya kujitoa kwenye mkataba wa unyonyaji wa kutuma mapato yao Ufaransa.Na Ufaransa iwagaie inavyoona sawa.
Umoja wa Afrika (AU) akianza kiongozi yeyote kuzungumzia Umoja wa kiuchumi anapigwa vita haraka sana.
Marekani na huyo mwanajeshi ni mamba.Tokea lini mamba akamuonea huruma anayemuwinda na kutaraji Kumla?
Asia wao wametokaje kiuchumi.
Pan-Africanism wanachojua ni lawama tu
 
africa ina hazina ya mali za kutisha .wametawala afrika miaka kadhaa wamevuna mali kadhaa na kujenga inchi zao sasa wanashangaa mwenye mali ameshindwa kujisimamia na kuwa omba omba.kama tusingekuwa na viongoz walafi afrika ingekuwa zaidi ya ulaya koz tunakila kitu kuanzia mafuta,madini,gesi na ardhi .kiujumla ulafi na ufisadi ni necha ya mwafrika tu.mfano angalia tu tabia za waamerika weusi pamoja na kuwa mbali na afrika tabia zao ni mbovu
 
Back
Top Bottom