Mwanajeshi wa Marine (USA) aliamua kuacha kazi jeshini na kuanza kazi mpya kama mwalimu wa high school

Mwanajeshi wa Marine (USA) aliamua kuacha kazi jeshini na kuanza kazi mpya kama mwalimu wa high school

Dogoli kinyamkela

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2024
Posts
618
Reaction score
1,440
Mwanajeshi wa Marine (USA) aliamua kuacha kazi jeshini na kuanza kazi mpya kama mwalimu wa high school, sasa kabla mwaka wa masomo haujaanza aliumia mgongo na akatakiwa avae plaster cast(piopi zile wanazovaa waliovunjika), akafungwa plaster cast iliyozunguka sehemu ya juu ya mwili wake kuzunguka mgongo na kifua, luckily ile cast ikakaa vizuri sana akivaa shati huwezi kugundua.

Siku yake ya kwanza akapangiwa kufundisha darasa lenye wanafunzi watukutu shuleni(na akajua kuwa kapangiwa wanafunzi watukutu), hawa wanafunzi wakajua mwalimu wao mpya ni mwanajeshi wa zamani wa marine (askari waliofundishwa kupigana kwenye maji na nchi kavu), kwakua ni watukutu wakamsubiri kwa hamu ili wamzingue waone atawafanya nini.

Wakajikusanya darasani kumsubiri kwa hamu, kama kawaida askari unatakiwa ujiongeze, akaingia darasani akakutana na kelele na vurugu za ajabu (akagundua wanampima) moja kwa moja akaenda kufungua dirisha moja la darasa hadi mwisho bila kuongea na mtu akavuta kiti akaa, sudden upepo mkali ukaanza kuingia kupitia dirishani tai yake ikaanza kupepea, muda huohuo kwa utulivu akavuta stapler (mashine yenye pini za kubania karatasi) , akashika stapler na tai yake inayopepea akatafakari kama sekunde kadhaa namna gani aizuie isipepee alafu akaigongea pini juu ya kifua chake pini ikatoboa tai na kifua, na akarudisha stapler mezani kama hakijatokea kitu.

Baada ya wanafunzi kuona tukio hilo la kutisha ghafla wote wakakaa kimya (completely quiet)

Since then wanafunzi walimpa heshima bila jamaa kusema neno hata moja na mwaka mzima wa masomo uliisha salama.
1734589446348.jpg
 
Baada y hili tukio kuliweka Kuna wadau nikawakumbusha mbali nao wakaleta waliyo poitia nakuwekea apo chini pitia Kuna vitu utajifunza👇🏽👇🏽👇🏽
 
Nkakumbuka baada ya kumaliza shule, Kuna ile program ya mafunzo ya jeshi Kwa mujibu wa Sheria.

Bas, nilijiunga na kambi (Makutupora). Kulikua na bustani, wanalima mboga, na matunda kubwa saana.

Siku Moja Muda wa kula, Mwanajeshi mmoja aliyekuwa anatusimamia, alituambia

"nimesikia Jana watu wengi, hawakwenda kumwagilia bustani, hvyo bustani haikumwagiliwa vizur, Leo msiende nitamwagilia Mimi"

Basi ile kauli, ni kama sisi hatukuelewa maana yake, hvyo kweli jioni hyo, hatukuenda kumwagilia kabisa. 😂

Hvyo usiku kwenye saa 5 hv wakat tupo kombania tunahesabu namba, ili ku hakiki idadi ya watu tuliopo kabla ya muda wa kulala.

Afande akatuambia, naona Leo hamjaenda kumwagilia kabisa, nyie madogo mnaleta dharau, ndo pale tukajua Nini alimaanisha mchana 😀😀😀.

Alichokifanya yule jamaa, aliagiza watu kama 15, walikuwa wamekaa msar wa mbele, wakachote maji katika ndoo Kila mmoja. Zikaletwa zimejaa maji, . Kimoyomoyo nikajua Leo, tunakula nua usiku huu,

Bas wakat anaongea na sisi, akielezea Jin's gani tunaweza kumsababishia adhabu Kali Kali kutoka Kwa MP, akachukua ndoo mbili zenye maji akazitia mchanga, kia's, af akajimwagia yeye kuanzia kichawani. Nikajua sasa sisi tumeisha, kama soldier kaamua kujipiga nua ( kujimwagia maji) sasa sisi itakuwaaje.😀😀

Baada ya kumaliza, akatuambia haya, nendeni mkalale,.. oyaaa hatukuamini, Yan tulienda kimya kimya hakuna mtu anaongea na mwezake...! 😂😂
 
nikiwa Jkt nilikua doja siku moja tukakamatwa na wenzagu tumedoji tukaambiwa tukroo sasa tukawa tunakroo huku tunakwepa matope afande akaona tunatania alikua kavaa nguo safi kuliko sisi lakini akalala chini akatuonyesha demo namna ya ku crawl akakroo kwenye maji machafu na alikua msafi zaidi yetu ila akaamua kuchafuka ili kuonyesha mfano kilichotukuta baada ya demo ilikua ni nusu ya kifo
 
Hatukuenda lakin,

nakukumbuka Kuna siku tulitoka mkesha saa 9:00 usiku, tukaambiwa nendeni mkachukue ndoo muende bustani kumwagilia.

Sis tukajua ni utani, si tukaenda kulala, aloo, tulikuja amshwa kibabe saana 😂😂😂😂.

Asee nilienda umalizia usingz katkat ya matuta, mbaya zaid nikaja amshwa na kukoswa kumwagiwa maji na waliokuwa wanamwagilia.

Asee kambin Kuna experience ya tofaut na maisha ya uraian.
 
Kuna jamaa, Alifanya kosa wakati wa chai. alipewa gogo atembee nalo kuanzia saa 4 asbh. Mpka saa 12 jion.

Yan anatembea kama hatua Tano af anapiga goti, ana Fanya kama kabeba RPG analipua 😂😂😂.

Sisi tukiwa kwenye kwata yeye kabeba gogo, tukiwa mess wakat wa kula analiweka pembeni, akimaliza tuu kula analo begani, tukienda bustani yeye ana gogo.

Yule jamaa alikuwa hoi balaa mpka inafika jion.
 
Tulipewa nguzo ya umeme tulizungukunga nayo uwanja mzima watu wawili tu ndio tangu siku Hiyo nikasema mwanangu Awezi kuja kufanya hizi kazi sitaki labda aje mm nimekufa
 
Tulikuwa tumebeba mabegi yetu mdogo mdogo tunalekea maeneo.
Ghafla raia miyeyusho anauliza " Waha vipi mbona mnatembeza vyombo kimya kimya " ilhali anaona kabisa Hawa ni wanajeshi.

Watu was pembeni wanacheeeka.
Jamaa Akazidi kuona sifa.
Akaongeza kusema
"Waha vipi mnakopesha au biashara ngumu ?"

Mmoja wetu Alikuwa kavalia kiraia akamnyaka kimangala.

Tukamlaza chali yaani tulizunguka round mbili mbili kupita juu yake ....sidhani Kama hakung'oka meno Wala kupata nyufa kwenye mifupa.

Kicheko kilikata na palikuwa kimyaaa.
#Chai
 
Tulikuwa tumebeba mabegi yetu mdogo mdogo tunalekea maeneo.
Ghafla raia miyeyusho anauliza " Waha vipi mbona mnatembeza vyombo kimya kimya " ilhali anaona kabisa Hawa ni wanajeshi.

Watu was pembeni wanacheeeka.
Jamaa Akazidi kuona sifa.
Akaongeza kusema
"Waha vipi mnakopesha au biashara ngumu ?"

Mmoja wetu Alikuwa kavalia kiraia akamnyaka kimangala.

Tukamlaza chali yaani tulizunguka round mbili mbili kupita juu yake ....sidhani Kama hakung'oka meno Wala kupata nyufa kwenye mifupa.

Kicheko kilikata na palikuwa kimyaaa.
#Chai
Chai Tena mkuu 😄😄😄😄😄 asubui yte hii
 
Back
Top Bottom