MwanaKJJ Jumatano: Jaji Kaijage Anapata Shida Kusimamia Uchaguzi TZ?

MwanaKJJ Jumatano: Jaji Kaijage Anapata Shida Kusimamia Uchaguzi TZ?

Nakumbuka Rais wa nchi hii aliwahi kutamka hadharani ni namna gani alitamani angekuwa IGP

Kitu ambacho sikumbuki ni ikiwa Rais alitamka hayo baada ya kuona Jeshi la Polisi likishindwa kupambana na uhalifu kero na sugu dhidi ya raia na mali zao au baada ya Jeshi la Polisi "kushindwa"
kushughulikia watu!

Kuna kauli nyingine pia nakumbuka lakini wacha nijipe muda kukumbuka sawasawa!
Au ile ya "wapigwe tu hamna namna'',ni moja kati ya kauli isiyo ya kiungwana kabisa,kwa hili inadhihirisha wazi raia hawana haki ya kupata wanachotaka mpaka Rais aamue,hili halina ubishi hata NEC na jeshi la polisi.
 
Naona usingizi umeanza kukutoka, Hata hivyo mimi wala simlaumu Jaji Kaijage.. Tatizo pale ni yule Kada anayeitwa Kailima na kapewa madaraka makubwa sana pengine hata kumzidi Mkuu wa tume, ukimsikia akiongea ni kama vile anajiona yeye ndiye Mungu au massiah ajaye, Wanatuharibia nchi kwa sababu ya kuweka makada kwenye sehemu nyeti!
Umeniwakilisha vyema Mkuu.
 
Waweza kuwa sahihi
Nina chuki kubwa na Narcisists walioko madarakani JMT lakini zaidi sana wale ambao hujitoa akili kuwasifia machizi hao
Wewe ni mmoja wao
Nakuchukia sana

Chuki inakuangamiza wewe mwenyewe; so jitahidi ujiponye. Ila kama inakufanya ujisikie vizuri keep it.
 
Mzee sijui kama unaelewa top officials wa serikalini wavofanya kazi kwa hofu na kujipendezeka awamu hii. Vituko tunavyovishuhudia huku unatamani kulia na kucheka kwa wakati mmoja. Watu wako terrified, wako terrorized hadi mtu hata amuzi dogo tuu anawaza what if mkuu akija kuniuliza hapa... Yani siku hizi nyekundu inaweza kuwa njano mchana wa saa saba

Why don't they quit? Hili ndio jambo sitaki kusikia watu wanalitetea.. wewe mtu mzima, umesoma, una gololi zako mbili bado unafanya kazi kwa kuogopa kwani ni lazima uwe na nafasi hiyo? Mbona watu wengi wanaishi tu nje ya serikali?
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Nilivyoandika jana kuna watu wanaona sikusema kwa ukali sana. Wapo wanaosema naogopa kumnyoshea kidole Rais Magufuli kwa sababu nilimuunga mkono kugombea kwake kuelekea Uchaguzi Mkuu 2015. Inachonishangaza ni kuwa hata watu wanaojua uandishi wangu wanafikiria kwa sababu fulani sijajiunga kwenye jukwaa la wanaotaka watafute uhalali wao wa kisiasa kwa kuonesha wanampinga Magufuli. Hili sina tatizo nalo na ndio maana ya uhuru wa fikra na maoni.

Hata hivyo, hatari ambayo ipo sasa kwa wanaharakati, wanasiasa, wanasiasa watarajiwa na watu wengine ni kuamua kufumba macho na kuwa wakali zaidi kwa kukosoa vitu na watu sahihi na kuwataka wawajibike. Rais Magufuli anabeba lawama zote za yale mambo ambayo yeye ndio mwamuzi wa mwisho na ambayo yanaweza kutatuliwa ama kwa ushauri wake au kwa maagizo yake rasmi (executive orders).

Kwa sasa, naamini kabisa siasa zetu zinaweza kubadilika kabisa, zikawa zakiungwana, zisizo na ulazima wa kumwaga damu na zisizojenga uhasama endapo vyombo hivi viwili chini ya viongozi wao wawili vitang’ang’aniwa na kulazimisshwa vifanye kazi yao inavyopaswa.

Hapa nazungumzia Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Jeshi la Polisi la Tanzania. Hili ni wazi kwa watu wengi lakini labda uzito wake ndio wengi bado hatujaupata inavyopaswa na badala yake tunakimbilia kumdai Rais. Wapo watu wengi sana ukiwasoma pamoja na ujuzi wao wote na hata uzoefu wao wote, wanaonekana hawaamini kabisa wanapaswa kuving’ang’ania vyombo hivi viwili.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi inaundwa kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 74 na utendaji wake kazi unaongozwa na sheria na kanuni mbalimbali husika. Ni kweli kwamba, Mwenyekiti na wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi huteuliwa na Rais; lakini hili si jambo geni. Nchi nyingi tu duniani tena za kidemokrasia zina mfumo ambapo Rais au Waziri Mkuu anateua wajumbe wa Tume za Uchaguzi. Suala kubwa kwa tume za uchaguzi si nani hasa anayeteua bali zaidi ni jinsi gani ziko huru kutoka kwa yule anayewateua.

Ni kweli kabisa, kwa mfumo wetu ulivyo, Tume ya Uchaguzi inamtegemea sana Rais. Hili hata hivyo, halimaanishi haiko huru kufanya kazi zake. Tatizo kubwa kwenye tume yetu ya Uchaguzi ni kukosekana kwa weledi (unprofessionalism) na hivyo kufanya kazi kinyume na kifungu cha 11 cha Ibara hiyo ya 74. Kiongozi yeyote wa tume (Mwenyekiti, Mjumbe au maafisa wa uchaguzi) wanaposikiliza, wanapofuata maagizo ya viongozi wa serikali au ya chama fulani cha kisiasa kama CCM kinyume na matakwa ya sheria na miongozo yao wanavunja Katiba.

Yaliyotokea kwenye Uchaguzi Mdogo wa Kinondoni; chombo pekee kinachopaswa kubeba lawama zote za mapungufu yote yaliyotokea pale ni Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Hii si mara ya kwanza kwa tume hii kuonekana inashindwa kuendesha uchaguzi kwa amani; na inaonekana kuzidiwa na misukumo na mihemuko ya kisiasa. Watendaji wake wanashinikizo kubwa la kusimamia haki na wakati mwingine inaonekana wanafanya kazi kwa woga au hofu fulani. Wapo waliojifunza kwa wenzao ambao waliwahi kuonekana kuadhibiwa au wengine kuzawadiwa.

Inawezekana vipi, tume miaka zaidi ya ishirini sasa ya kuendesha chaguzi mbalimbali bado inapata shida kuweka utaratibu mzuri kwa mawakala, wanasiasa, na hata kusimamia uchaguzi bila watu kuonekana wameonewa? Hivi ni kweli wote humo ndani ya tume hakuna mtu mwenye weledi na usomi wa kujaribu kutabiri (expect) matatizo mbalimbali yanayoweza kutokea kama jambo moja au la pili likitokea. Hivi ni kweli, tume haijaona jinsi gani masuala ya mawakala yanavyosumbua.

Hivi kwanini mawakala wa vyama vya siasa wanasubiri hadi siku moja kabla ya uchaguzi ndio wapate kukubaliwa? Kuna ubaya gani, kwa watu wenye akili timamu kusema tutengeneze utaratibu utakaohakikisha kuwa wiki moja kabla ya uchaguzi wowote – uwe mdogo au mkuu – kila chama kiwe kimeshapata kila kinachohitajika kuhakikisha kuwa mawakala n.k wanajulikana na wamepata utambulisho wote? Kwanini tusubiri hadi dakika za mwisho kama siyo kutengeneza mazingira ya watu kuonekaan wameonewa na kulazimisha watu wengine wajaribu kuweka shinikizo lisilo la lazima?

Leo hii tunawalaumu upinzani kwa kuandamana kudai mambo ya mawakala wao? Tuliwataka wafanye nini? Wakinge mikono na kuomba kama zawadi? Wote tumeona jinsi gani serikali na vyombo vyake vilivyotumiwa kwenye chaguzi hizi hasa Kinondoni; kweli kabisa tunataka Mahakama ndio ije baadaye kutengua uchaguzi huu huu halafu watu warudie tena kama vichaa wasiojifunza lolote? Binafsi naamini CHADEMA itakuwa na msingi mzuri tu wa kwenda mahakamani kupinga kuchaguliwa kwa Mtulia na sitoshangaa wakashinda! Lakini kwanini tufike huko?

Tatizo la utendaji wa Tume ya Uchaguzi ni kubwa mno, linatia aibu na linatufanya tujihoji kama tunaweza kuendesha uchaguzi sisi wenyewe bila kulazimisha uhasama, vurugu, na hisia za kuonewa. Niliuliza juzi; hivi kweli ni vigumu sana kwa Watanzania kuendeshsa uchaguzi kwa amani, kwa utulivu, na katika mazingira ya ushindani na siyo uadui? Kwanini tuendessha uchaguzi kama wale wengine wanaogombea wanatoka sayari ya Zebaki au Zuhura na hivyo hawastahili kabisa kuaminiwa au kupewa nafasi? Ni ukiritimba gani huu tulio nao kwenye fikra za kiutawala?

Hivi, kwa mfano CHADEMA wangeshinda Kinondoni katika mazingira ya uhuru, haki na usawa; hivi Kinondoni ingegeuka jangwa? Au wana CCM wa Kinondoni wangegeuka misukule? Si huyo huyoaliyegombea CCM alikuwa CUF na alishinda 2015 na Kinondoni watu waliendelea kuishi, kufanya shughuli zao na maisha yaliendelea? Au tu ni dalili kuwa inawezekana ipo haja ya kuanza kuandika tena na kusimuliza vile visa vya Ujinga wa Mwafrika? Kweli kabisa, tunashindwa kuendesha uchaguzi sisi kwa wasomi wetu, na watendaji wetu ambao waliapa kuendesha uchaguzi kwa haki na bila upendeleo wakizingatia Katiba?

Nani aliyesema kuwa tunahitaji amani zaidi siku ya kutumbukiza makaratasi kwenye masanduku kuliko mchakato mzima wakufikia siku hiyo. Kama uchaguzi ungekuwa ni kutumbukiza karatasi tu; sisi kampeni zinawekwa za nini? si lengo ni kushawishi watu kwa hoja. Sasa kama watu hawawezi kushawishi kwa hoja na badala yake wanatawaliwa na vihoja; kwanini isiamuliwe tu hakuna tena kampeni kama kampeni zinaudhi sana baadhi ya watu?

Matatizo yaliyomshinda Jaji Lubuva tunaona leo yanajirudia na kuwa ni magumu kushughulikiwa na Jaji Kaijage. Ina maana hawa majaji wanaweza kuwa ni mahiri wa sheria, lakini inawezekana ni viongozi wabovu. Kwanini mambo ambayo yanawezekana kama mtu akiwa thabiti yaonekane kuwa magumu hivyo? Kama wanaona hawawezi kufanya kazi bila kuingiliwa au mashinikizo mengine si waamue kujiuzulu kuliko kujiabisha kwa kuendesha mfumo ambao unadharaulisha kabisa dhana nzima ya haki, usawa, na ushindani wa kisiasa? Yaani, kama marefarii wa mpira wa miguu wangekuwa wanapata shida kama hizi; kweli kuna mechi ingekuwa inachezwa? Kama refarii angesikiliza mashabiki na wamiliki wa timu, kweli wangeweza kuchezesha mchezo wowote?

Tatizo la pili; ni Jeshi la Polisi. Sijasema tatizo ni Askari Polisi. Nimesema Jeshi la Polisi. Suluhisho langu kuhusiana na hili hapo kesho, likipokelewa na wenye kupokea na wakalifanyia kazi nawahakikishia kwa asilimia 90 litabadili kabisa mahusiano kati ya Jeshi na vyama vya upinzani na litatengeneza mazingira mapya kabisa ya kisiasa.

Itaendelea Kesho
Mkubwa hakosei ila umempaka mafuta kwa mgongo wa chupa naamini atakuelewa
 
NDUGU MEXENE MELLO et al.,
Naomba mnipige ban ya miaka miwili mpaka 2020.siwezi kuendelea kusoma maoni ya / comment ya wana Lumumba wapumbafu na machoko.
Ila endeleeni kushangilia, wakati bado unakuja .Magufuri kaweka vyombo vya habari kwapani, mahakama kwapani, jeshi la polisi kwani, bunge kwapani,shughuli za kisiasa na democrasia kwapani, taasisi za kidini kwapani nadhani uchunguzi kakobe mmeusikia. Shangilieni ,imbeni mtakavyo weza, tukaneni vyama pinzani mtakavyo weza, nunueni madiwani na wabunge mtakavyo weza ,ueni upinzani kadiri nguvu zenu zitakavyo weza.Ule mwisho badoo, Magufuri akianza kuuwa watu wake ndani ya ccm akihisi wanamuhujumu na wengine ndani ya chama chake , ndipo ule wakati uliotabiriwa utakuwa umewadia. Mtatafuta pa kukimbilia mtakosa, mtalia na kusaga meno ,mtaomboleza lakini hamtaona msaada wala hakuta kuwa na kimbilio. Endeleeni kushangilia, endeleeni kusifia.....siku zaja.
 
Naona usingizi umeanza kukutoka, Hata hivyo mimi wala simlaumu Jaji Kaijage.. Tatizo pale ni yule Kada anayeitwa Kailima na kapewa madaraka makubwa sana pengine hata kumzidi Mkuu wa tume, ukimsikia akiongea ni kama vile anajiona yeye ndiye Mungu au massiah ajaye, Wanatuharibia nchi kwa sababu ya kuweka makada kwenye sehemu nyeti!
Upuuzi huyo. Keenge tu kama ndugu yake. Analipwa kujinyeeea.
 
Why don't they quit? Hili ndio jambo sitaki kusikia watu wanalitetea.. wewe mtu mzima, umesoma, una gololi zako mbili bado unafanya kazi kwa kuogopa kwani ni lazima uwe na nafasi hiyo? Mbona watu wengi wanaishi tu nje ya serikali?
Mzee MWANAKIJIJI hapa umepotoka, mamlaka ya Rais nafikiri unayafahamu vizuri sana, changanya na uafrica wetu sasa
 
Au ile ya v"wapigwe tu hamna namna'',ni moja kati ya kauli isiyo ya kiungwana kabisa,kwa hili inadhihirisha wazi raia hawana haki ya kupata wanachotaka mpaka Rais aamue,hili halina ubishi hata NEC na jeshi la polisi.
Hapana, hilo nalikumbuka sawa sawa na lilitoka kwa Mzee Pinda! Ninalosema mimi lilitoka kwa Mkulu mwenyewe siku Lowassa alipozungumzia Masheikh wanaoshikiliwa kule Zanzibar!

Mkulu akaunganisha hilo pamoja na la Kibiti na kuchomokea suala la Manji "kukamatwa na sare za JWTZ" huku Mkulu akitoa kauli ya kuashiria sare hizo za kijeshi huenda zina connection na mauaji ya kule Kibiti (Manji ana jeshi; au?).

Mwisho wa yote Mkulu akatoa kauli kuashiria atashangaa endapo Jeshi la Polisi halitamkamata na kumhoji mtu "hatari" kama Lowassa!

Ile kauli yangu ya kwamba nimesahau kidogo ni mbwembwe tu za uandishi lakini nakumbuka vyema kauli kadhaa za Mkulu zinazoashiria kuagiza Jeshi la Polisi kushughulikia watu badala ya issue ingawaje Mzee Mwanakijiji haoni ni namna gani Rais anaweza kuhusishwa moja kwa moja na yanayoendelea huku akijitia uziwi kusikia kauli mbalimbali za Rais zinazo-encourage watendaji wa serikali kuenenda in unprofession way!

MM wala haoni ni namna gani wala hailekei kwamba Rais anakerwa na mambo ya hovyo yanayofanywa na watendaji wa serikali na taasisi zake!

MM anajitia kutojua kwamba kwa mambo kadhaa yaliyotokea nchi hii, Rais alitakiwa awe ameshamfukuza kazi Waziri wa Mambo ya Ndani! Na kwavile Rais hajafanya na wala haielekei kwamba atafanya hivyo; bado MM anajitia kutojua kwamba kwa kutochukua hatua, basi yote hayo ni kama yanaungwa mkono na Rais lakini hata kama anaunga mkono bado ni dhambi kumuhusisha Mheshimiwa Mkuu!

Na kama tunataka kumuhusisha rais; according to MM's new arguing style; tunatakiwa ku-justify in one way or another kwamba ingawaje yanatokea under Mkulu's nose; hayo si mapya kupata kutokea duniani let alone Tanzania!

Kwamba; yalipata kutokea enzi za akina Chief Mangungo, yakatokea enzi za Mwarabu! Yalitokea enzi za Mjerumani na Mwingereza! Yakatokea enzi za Mwalimu, Mwinyi, Mkapa na Kikwete!

Kwahiyo tusimsimange Mkulu kwa mambo yaliyopata kutokea hata mbele ya macho ya mitume!
 
Hapana, hilo nalikumbuka sawa sawa na lilitoka kwa Mzee Pinda! Ninalosema mimi lilitoka kwa Mkulu mwenyewe siku Lowassa alipozungum Masheikh wanaoshikiliwa kule Zanzibar!

Mkulu akaunganisha hilo pamoja na la Kibiti na kuchomokea suala la Manji "kukamatwa na sare za JWTZ" huku Mkulu akitoa kauli ya kuashiria sare hizo za kijeshi huenda zina connection na mauaji ya kule Kibiti (Manji ana jeshi; au?).

Mwisho wa yote Mkulu akatoa kauli kuashiria atashangaa endapo Jeshi la Polisi halitamkamata na kumhoji mtu "hatari" kama Lowassa!

Ile kauli yangu ya kwamba nimesahau kidogo ni mbwembwe tu za uandishi lakini nakumbuka vyema kauli kadhaa za Mkulu zinazoashiria kuagiza Jeshi la Polisi kushughulikia watu badala ya issue ingawaje.Utata ni kwamba kipindi huyu bwana watu wengi walimchukulia kama mtu asiye na mapungufu na watu wakamnadi na kumpamba ipasavyo humu,sasa anatilinganya mambo watu humu kukanusha wanaona soni kwa hiyo maneno yanapinduliwapinduliwa tu.
 
Huyu mzee nilikuwa namheshim sana lakini nini sijui kilimkuta mzee naomba rudisha akili yako ya zamani
 
Hivi waliojiandikisha kupiga kura walikuwa wangapi, na waliopiga kura walikuwa wangapi? Je tunaolalamika tulikuwa miongoni mwa wapiga kura?
only a fool will think this way

kwamba tusijadili kisa hatukupiga kura
 
Nimesoma makala hii kutoka kwa nguli na mwanafalsafa wa JF, ndugu Mzee Mwanakijiji na hakika nimebaki kuwa puzzled na mashaka makubwa. Mara nyingi topic za namna hii huwa napita kimya kwa sababu wengi ya wachangiaji ni sehemu ya tatizo la mfumo wa nchi hii..! Lakini kabla sijaendelea, nilijiuliza yafuatayo;-
  1. Je mwandishi anajua anachokisema?
  2. Je mwandishi alishindwaje kutofautisha kati ya mfumo/system, udikiteta, Democrasia and Illiteracy?
  3. Is he biased?
  4. Je mwandishi huyu ni zao la kodi ya wananchi?..etc
  5. Je hawa ndo aina ya political analyst wa Nchi hii?
Ndugu mwandishi ukipata muda njoo ujibu maswali/ hypothesis hapo juu ili tuwekane sawa. baada ya kusema hayo, naomba nijikite kwenye hoja kama ifuatavyo;-

Mosi, mwandishi hayuko focused. ameshindwa kueleweka anatetea nini, kwa manufaa ya nani na kwa ajili gani. truth be told, hii article tungeipeleka kwa serious editors...Isingeliona jua! Nilitarajia mwandishi achambue tatizo la mfumo (system) na jinsi yanayotokea kwa sasa kuwa ndo engineering ya mfumo wenyewe. Mfumo wa siasa wa Tanzania goes back to history wakati wa Nyalali commission kuhusu siasa za vyama vingi. Report inaonyesha about 80% walipinga kuwepo kwa vyama vingi...huku asilimia 20% tu ikikubali uwepo wa multiparty system in Tanzania. Hii inamaanisha nini? It means, bado watu hawana elimu ya kutosha kuhusu democrasia na uwepo vyama vingi nchini. Such illiteracy bado iko kubwa miongoni mwa viongozi wa serikali including RAIS na Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi. with such analysis, ndo maana tunaona chuki, uonevu, mauaji dhidi ya wapinzani..

The Political Parties Act [CAP 258 R.E. 20024, Ibara ya 4(1) inasema kuwa Kutakuwa na Msajili wa Vyama vya Siasa katika ofisi ya Waziri Mkuu au katika ofisi nyingine kama Rais anavyoweza kuamua na atachaguliwa na Rais.There shall be a Registrar of Political Parties in the office of the Prime Minister or in such other office as the President may determine who shall be appointed by the President.Hali kadhalika, sheria ya tume ya uchaguzi inasema katika ibara ya 6(1) kuwa There shall be a Director of
Elections who shall be appointed by the President from amongst the names of senior civil servants of the United Republic recommended by the Commission.

as i quote you...Jaji Kaijage Anapata Shida Kusimamia Uchaguzi tz? The answer is yes! kwa sababu zifuatazo;-

  1. Is biased, kwa kuwa ni mteule wa Rais
  2. Hayuko independent kwa sababu iliyoainishwa hapo juu
  3. Is Illiterate kwa sababu ni sehemu ya ile 80% percent ya Nyalali Commission
  4. Ni mwanachama wa CCM...(I have evidence)
Rule against biases: Mwandishi yuko biased. I quote..."Wapo wanaosema naogopa kumnyoshea kidole Rais Magufuli kwa sababu nilimuunga mkono kugombea kwake kuelekea Uchaguzi Mkuu 2015. Inachonishangaza ni kuwa hata watu wanaojua uandishi wangu wanafikiria kwa sababu fulani sijajiunga kwenye jukwaa la wanaotaka watafute uhalali wao wa kisiasa kwa kuonesha wanampinga Magufuli". Kwa Introduction ya namna hii, umekosa credibility ya kuendelea kufanya submission na kuna-invalidate article nzima na kuwa redundant. labda nikuulize swali, whom are you fighting with?

Mwalimu Nyerere akiwahutubia ma-judge wa kipindi hicho huko tabora, aliwahi kusema kuwa "Mahakama zetu katika kila ngazi lazima ziwe huru na mkono wa mtendaji wa serikali (executives). Uhuru wa kweli unahitaji kwamba raia yeyote anajiamini kuwa kesi yake haitakuwa na uamuzi wa upendeleo, hata kama ni kesi dhidi ya waziri mkuu."....Je msajili yuko huru? je mahakama ziko huru? Free from whom?...Maybe from executives?...probably yes..probably no!

Issue nyingine yenye ukakasi ni pale mwandishi aliposema kuhusu as i quote..."Jeshi la Polisi. Sijasema tatizo ni Askari Polisi". Nijuavyo mimi askari polisi ni sehemu ya jeshi la polisi na hawatenganishiki.

HENCEFORTH, one may conclude that;-

  1. Article yako haina mashiko
  2. You lack skills on analyzing political issues
  3. Hauko focused
  4. Hukufanya Research wakati unaandiika article hii
Cheers, Prof
 
Kuna watu wanasema ati kwa vile Rais kasema kauli zake basi watumishi wanaondoa ufahamu kabisa. Ilitarajiwa baada ya Rais kusema alichosema Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi alipaswa kutoa maagizo ya kuwataka watendaji wote kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sharia na Katiba na bila upendeleo. Angewataka wahakikishe aliyeshinda kwa halali ndio anatangazwa.

Tumezoea kulea tabia za uzembe na watu kutozingatia maadili yao ya kazi ndio maana tunazitolea udhuru. Mtu amepewa majukumu na anajua majukumu yake halafu anasema "anaingiliwa". Hivi huko wanakojifunza, hawajifunza kujiuzulu? Ina maana Tanzania watumishi wote hawana ujasiri wa kusema "mimi hili sifanyi"? Au ndio watu wanasema "njaa" kwa hiyo njaa imewaondoa kabisa weledi?

Ukikubali hili; unafikiri itakuwaje?
Mkuu maisha magumu sana,
Hata huko Marekani na Nchi zilizo endelea ukiona yeyote anajiuzulu jua ana uhakika na maisha yake kiusalama na kiuchumi.

Sasa nitajiuzulu vipi nikiwa sina uhakuka na ugali wa kesho??
 
w
Na. M. M. Mwanakijiji

Nilivyoandika jana kuna watu wanaona sikusema kwa ukali sana. Wapo wanaosema naogopa kumnyoshea kidole Rais Magufuli kwa sababu nilimuunga mkono kugombea kwake kuelekea Uchaguzi Mkuu 2015. Inachonishangaza ni kuwa hata watu wanaojua uandishi wangu wanafikiria kwa sababu fulani sijajiunga kwenye jukwaa la wanaotaka watafute uhalali wao wa kisiasa kwa kuonesha wanampinga Magufuli. Hili sina tatizo nalo na ndio maana ya uhuru wa fikra na maoni.

Hata hivyo, hatari ambayo ipo sasa kwa wanaharakati, wanasiasa, wanasiasa watarajiwa na watu wengine ni kuamua kufumba macho na kuwa wakali zaidi kwa kukosoa vitu na watu sahihi na kuwataka wawajibike. Rais Magufuli anabeba lawama zote za yale mambo ambayo yeye ndio mwamuzi wa mwisho na ambayo yanaweza kutatuliwa ama kwa ushauri wake au kwa maagizo yake rasmi (executive orders).

Kwa sasa, naamini kabisa siasa zetu zinaweza kubadilika kabisa, zikawa zakiungwana, zisizo na ulazima wa kumwaga damu na zisizojenga uhasama endapo vyombo hivi viwili chini ya viongozi wao wawili vitang’ang’aniwa na kulazimisshwa vifanye kazi yao inavyopaswa.

Hapa nazungumzia Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Jeshi la Polisi la Tanzania. Hili ni wazi kwa watu wengi lakini labda uzito wake ndio wengi bado hatujaupata inavyopaswa na badala yake tunakimbilia kumdai Rais. Wapo watu wengi sana ukiwasoma pamoja na ujuzi wao wote na hata uzoefu wao wote, wanaonekana hawaamini kabisa wanapaswa kuving’ang’ania vyombo hivi viwili.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi inaundwa kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 74 na utendaji wake kazi unaongozwa na sheria na kanuni mbalimbali husika. Ni kweli kwamba, Mwenyekiti na wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi huteuliwa na Rais; lakini hili si jambo geni. Nchi nyingi tu duniani tena za kidemokrasia zina mfumo ambapo Rais au Waziri Mkuu anateua wajumbe wa Tume za Uchaguzi. Suala kubwa kwa tume za uchaguzi si nani hasa anayeteua bali zaidi ni jinsi gani ziko huru kutoka kwa yule anayewateua.

Ni kweli kabisa, kwa mfumo wetu ulivyo, Tume ya Uchaguzi inamtegemea sana Rais. Hili hata hivyo, halimaanishi haiko huru kufanya kazi zake. Tatizo kubwa kwenye tume yetu ya Uchaguzi ni kukosekana kwa weledi (unprofessionalism) na hivyo kufanya kazi kinyume na kifungu cha 11 cha Ibara hiyo ya 74. Kiongozi yeyote wa tume (Mwenyekiti, Mjumbe au maafisa wa uchaguzi) wanaposikiliza, wanapofuata maagizo ya viongozi wa serikali au ya chama fulani cha kisiasa kama CCM kinyume na matakwa ya sheria na miongozo yao wanavunja Katiba.

Yaliyotokea kwenye Uchaguzi Mdogo wa Kinondoni; chombo pekee kinachopaswa kubeba lawama zote za mapungufu yote yaliyotokea pale ni Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Hii si mara ya kwanza kwa tume hii kuonekana inashindwa kuendesha uchaguzi kwa amani; na inaonekana kuzidiwa na misukumo na mihemuko ya kisiasa. Watendaji wake wanashinikizo kubwa la kusimamia haki na wakati mwingine inaonekana wanafanya kazi kwa woga au hofu fulani. Wapo waliojifunza kwa wenzao ambao waliwahi kuonekana kuadhibiwa au wengine kuzawadiwa.

Inawezekana vipi, tume miaka zaidi ya ishirini sasa ya kuendesha chaguzi mbalimbali bado inapata shida kuweka utaratibu mzuri kwa mawakala, wanasiasa, na hata kusimamia uchaguzi bila watu kuonekana wameonewa? Hivi ni kweli wote humo ndani ya tume hakuna mtu mwenye weledi na usomi wa kujaribu kutabiri (expect) matatizo mbalimbali yanayoweza kutokea kama jambo moja au la pili likitokea. Hivi ni kweli, tume haijaona jinsi gani masuala ya mawakala yanavyosumbua.

Hivi kwanini mawakala wa vyama vya siasa wanasubiri hadi siku moja kabla ya uchaguzi ndio wapate kukubaliwa? Kuna ubaya gani, kwa watu wenye akili timamu kusema tutengeneze utaratibu utakaohakikisha kuwa wiki moja kabla ya uchaguzi wowote – uwe mdogo au mkuu – kila chama kiwe kimeshapata kila kinachohitajika kuhakikisha kuwa mawakala n.k wanajulikana na wamepata utambulisho wote? Kwanini tusubiri hadi dakika za mwisho kama siyo kutengeneza mazingira ya watu kuonekaan wameonewa na kulazimisha watu wengine wajaribu kuweka shinikizo lisilo la lazima?

Leo hii tunawalaumu upinzani kwa kuandamana kudai mambo ya mawakala wao? Tuliwataka wafanye nini? Wakinge mikono na kuomba kama zawadi? Wote tumeona jinsi gani serikali na vyombo vyake vilivyotumiwa kwenye chaguzi hizi hasa Kinondoni; kweli kabisa tunataka Mahakama ndio ije baadaye kutengua uchaguzi huu huu halafu watu warudie tena kama vichaa wasiojifunza lolote? Binafsi naamini CHADEMA itakuwa na msingi mzuri tu wa kwenda mahakamani kupinga kuchaguliwa kwa Mtulia na sitoshangaa wakashinda! Lakini kwanini tufike huko?

Tatizo la utendaji wa Tume ya Uchaguzi ni kubwa mno, linatia aibu na linatufanya tujihoji kama tunaweza kuendesha uchaguzi sisi wenyewe bila kulazimisha uhasama, vurugu, na hisia za kuonewa. Niliuliza juzi; hivi kweli ni vigumu sana kwa Watanzania kuendeshsa uchaguzi kwa amani, kwa utulivu, na katika mazingira ya ushindani na siyo uadui? Kwanini tuendessha uchaguzi kama wale wengine wanaogombea wanatoka sayari ya Zebaki au Zuhura na hivyo hawastahili kabisa kuaminiwa au kupewa nafasi? Ni ukiritimba gani huu tulio nao kwenye fikra za kiutawala?

Hivi, kwa mfano CHADEMA wangeshinda Kinondoni katika mazingira ya uhuru, haki na usawa; hivi Kinondoni ingegeuka jangwa? Au wana CCM wa Kinondoni wangegeuka misukule? Si huyo huyoaliyegombea CCM alikuwa CUF na alishinda 2015 na Kinondoni watu waliendelea kuishi, kufanya shughuli zao na maisha yaliendelea? Au tu ni dalili kuwa inawezekana ipo haja ya kuanza kuandika tena na kusimuliza vile visa vya Ujinga wa Mwafrika? Kweli kabisa, tunashindwa kuendesha uchaguzi sisi kwa wasomi wetu, na watendaji wetu ambao waliapa kuendesha uchaguzi kwa haki na bila upendeleo wakizingatia Katiba?

Nani aliyesema kuwa tunahitaji amani zaidi siku ya kutumbukiza makaratasi kwenye masanduku kuliko mchakato mzima wakufikia siku hiyo. Kama uchaguzi ungekuwa ni kutumbukiza karatasi tu; sisi kampeni zinawekwa za nini? si lengo ni kushawishi watu kwa hoja. Sasa kama watu hawawezi kushawishi kwa hoja na badala yake wanatawaliwa na vihoja; kwanini isiamuliwe tu hakuna tena kampeni kama kampeni zinaudhi sana baadhi ya watu?

Matatizo yaliyomshinda Jaji Lubuva tunaona leo yanajirudia na kuwa ni magumu kushughulikiwa na Jaji Kaijage. Ina maana hawa majaji wanaweza kuwa ni mahiri wa sheria, lakini inawezekana ni viongozi wabovu. Kwanini mambo ambayo yanawezekana kama mtu akiwa thabiti yaonekane kuwa magumu hivyo? Kama wanaona hawawezi kufanya kazi bila kuingiliwa au mashinikizo mengine si waamue kujiuzulu kuliko kujiabisha kwa kuendesha mfumo ambao unadharaulisha kabisa dhana nzima ya haki, usawa, na ushindani wa kisiasa? Yaani, kama marefarii wa mpira wa miguu wangekuwa wanapata shida kama hizi; kweli kuna mechi ingekuwa inachezwa? Kama refarii angesikiliza mashabiki na wamiliki wa timu, kweli wangeweza kuchezesha mchezo wowote?

Tatizo la pili; ni Jeshi la Polisi. Sijasema tatizo ni Askari Polisi. Nimesema Jeshi la Polisi. Suluhisho langu kuhusiana na hili hapo kesho, likipokelewa na wenye kupokea na wakalifanyia kazi nawahakikishia kwa asilimia 90 litabadili kabisa mahusiano kati ya Jeshi na vyama vya upinzani na litatengeneza mazingira mapya kabisa ya kisiasa.

Itaendelea Kesho
WEWE NI MNAFIKI TU HATA UJIFANYE KUFUMBA MACHO, ULISHASIKIA TANGAZO TANGAZO KUWA MKURUGENZI NAMLIPA MSHAHARA, NAMPA GARI NA NYUMBA LEO ATANGAZE WA UPINZANI??????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????? HALAFU LEO UNAJICHETUA UONEKANE UNASIMAMA UPANDE WA HAKI. MFYUUUUUUUUUUUUUUUUUUU
 
Nimesoma makala hii kutoka kwa nguli na mwanafalsafa wa JF, ndugu Mzee Mwanakijiji na hakika nimebaki kuwa puzzled na mashaka makubwa. Mara nyingi topic za namna hii huwa napita kimya kwa sababu wengi ya wachangiaji ni sehemu ya tatizo la mfumo wa nchi hii..! Lakini kabla sijaendelea, nilijiuliza yafuatayo;-
  1. Je mwandishi anajua anachokisema?
  2. Je mwandishi alishindwaje kutofautisha kati ya mfumo/system, udikiteta, Democrasia and Illiteracy?
  3. Is he biased?
  4. Je mwandishi huyu ni zao la kodi ya wananchi?..etc
  5. Je hawa ndo aina ya political analyst wa Nchi hii?
Ndugu mwandishi ukipata muda njoo ujibu maswali/ hypothesis hapo juu ili tuwekane sawa. baada ya kusema hayo, naomba nijikite kwenye hoja kama ifuatavyo;-

Mosi, mwandishi hayuko focused. ameshindwa kueleweka anatetea nini, kwa manufaa ya nani na kwa ajili gani. truth be told, hii article tungeipeleka kwa serious editors...Isingeliona jua! Nilitarajia mwandishi achambue tatizo la mfumo (system) na jinsi yanayotokea kwa sasa kuwa ndo engineering ya mfumo wenyewe. Mfumo wa siasa wa Tanzania goes back to history wakati wa Nyalali commission kuhusu siasa za vyama vingi. Report inaonyesha about 80% walipinga kuwepo kwa vyama vingi...huku asilimia 20% tu ikikubali uwepo wa multiparty system in Tanzania. Hii inamaanisha nini? It means, bado watu hawana elimu ya kutosha kuhusu democrasia na uwepo vyama vingi nchini. Such illiteracy bado iko kubwa miongoni mwa viongozi wa serikali including RAIS na Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi. with such analysis, ndo maana tunaona chuki, uonevu, mauaji dhidi ya wapinzani..

The Political Parties Act [CAP 258 R.E. 20024, Ibara ya 4(1) inasema kuwa Kutakuwa na Msajili wa Vyama vya Siasa katika ofisi ya Waziri Mkuu au katika ofisi nyingine kama Rais anavyoweza kuamua na atachaguliwa na Rais.There shall be a Registrar of Political Parties in the office of the Prime Minister or in such other office as the President may determine who shall be appointed by the President.Hali kadhalika, sheria ya tume ya uchaguzi inasema katika ibara ya 6(1) kuwa There shall be a Director of
Elections who shall be appointed by the President from amongst the names of senior civil servants of the United Republic recommended by the Commission.

as i quote you...Jaji Kaijage Anapata Shida Kusimamia Uchaguzi tz? The answer is yes! kwa sababu zifuatazo;-

  1. Is biased, kwa kuwa ni mteule wa Rais
  2. Hayuko independent kwa sababu iliyoainishwa hapo juu
  3. Is Illiterate kwa sababu ni sehemu ya ile 80% percent ya Nyalali Commission
  4. Ni mwanachama wa CCM...(I have evidence)
Rule against biases: Mwandishi yuko biased. I quote..."Wapo wanaosema naogopa kumnyoshea kidole Rais Magufuli kwa sababu nilimuunga mkono kugombea kwake kuelekea Uchaguzi Mkuu 2015. Inachonishangaza ni kuwa hata watu wanaojua uandishi wangu wanafikiria kwa sababu fulani sijajiunga kwenye jukwaa la wanaotaka watafute uhalali wao wa kisiasa kwa kuonesha wanampinga Magufuli". Kwa Introduction ya namna hii, umekosa credibility ya kuendelea kufanya submission na kuna-invalidate article nzima na kuwa redundant. labda nikuulize swali, whom are you fighting with?

Mwalimu Nyerere akiwahutubia ma-judge wa kipindi hicho huko tabora, aliwahi kusema kuwa "Mahakama zetu katika kila ngazi lazima ziwe huru na mkono wa mtendaji wa serikali (executives). Uhuru wa kweli unahitaji kwamba raia yeyote anajiamini kuwa kesi yake haitakuwa na uamuzi wa upendeleo, hata kama ni kesi dhidi ya waziri mkuu."....Je msajili yuko huru? je mahakama ziko huru? Free from whom?...Maybe from executives?...probably yes..probably no!

Issue nyingine yenye ukakasi ni pale mwandishi aliposema kuhusu as i quote..."Jeshi la Polisi. Sijasema tatizo ni Askari Polisi". Nijuavyo mimi askari polisi ni sehemu ya jeshi la polisi na hawatenganishiki.

HENCEFORTH, one may conclude that;-

  1. Article yako haina mashiko
  2. You lack skills on analyzing political issues
  3. Hauko focused
  4. Hukufanya Research wakati unaandiika article hii
Cheers, Prof
Yaani kuna watu mpka unatamani uwe unakutana nao nje y jf mzungumze mawili matatu.
Uchambuzi mzuri. Hongera profesa. Unautendea haki "uprofesa".
 
Back
Top Bottom